Agano la Kale 2022
Januari 24–30. Musa 7: “Bwana Akawaita Watu Wake Sayuni”


“Januari 24–30. Musa 7: “Bwana Akawaita Watu Wake Sayuni,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano la Kale 2022 (2021)

“Januari 24–30. Musa 7,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2022

Picha
watu wengi wakichangamana katika njia za upendo

Pendaneni, na Emma Donaldson Taylor

Januari 24–30

Musa 7

“Bwana Akawaita Watu Wake Sayuni”

Unaposoma Musa 7, fikiria kuhusu watu unaowafundisha na jinsi unavyoweza kuwasaidia kuelewa kile sura hii inachofundisha kuhusu Sayuni na kanuni zingine za injili.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Wakati mwingine swali rahisi na dakika chache za kutafakari zinatosha kusaidia watu kushiriki kile wanachojifunza nyumbani. Pengine ungeweza kuwapa washiriki wa darasa muda mfupi wa kurejea tena Musa 7, kupata mstari ambao unawafanya kuhisi shukrani kwa ajili ya kweli zilizorejeshwa katika kitabu cha Musa, na kisha kuushiriki.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Musa 7:16–21, 27, 53, 62–69

Tunaweza kuijenga Sayuni katika wakati wetu.

  • Ipi ingekuwa njia bora ya kuwasilisha wazo la Sayuni katika darasa lako? Moja ya wazo lingekuwa kuwasiliana na washiriki wa darasa wiki moja kabla ya darasa na kuwaomba kuleta kitu kutoka nyumbani ambacho wanahisi kinawakilisha tabia za watu wa Sayuni, kama ilivyoelezwa katika Musa 7:18. Mnapojadiliana mstari huu pamoja, washiriki wa darasa wangeweza kueleza umuhimu wa kitu walichokileta.

    Picha
    watu wakisalimiana

    Tunapaswa kujitahidi kuwa “wa moyo mmoja na wazo moja” (Musa 7:18).

  • Video “We Come Together and Unite as One” (ChurchofJesusChrist.org) ingeweza kukusaidia kuanza majadiliano kuhusu jinsi tunavyoweza kuwa “wa moyo mmoja na wazo moja” (Musa 7:18) katika kata zetu na familia. Fikiria kuwaomba washiriki wa darasa kufikiria kuhusu wakati walipohisi umoja miongoni mwa familia zao au wakati wakiwahudumia wengine katika Kanisa au jumuiya. Watu walifanya nini kujenga umoja katika hali hizi? Nini tunaweza kujifunza kuhusu Sayuni na umoja kutoka Musa 7? (Ona hususani mistari 16–21, 27, 53, 62–69). Haya ni baadhi ya maandiko mengine ambayo yangeweza kusaidia: Wafilipi 2:1–4; 4 Nefi 1:15–18; Mafundisho na Maagano 97:21; 105:5.

Musa 7:28–44

Mungu analia kwa ajili ya watoto Wake.

  • Baadhi ya watu wanaweza kumwona mungu kama yuko mbali, asiyefikiwa, na hata asiyejali. Jinsi gani unaweza kutumia ono la Henoko kusaidia darasa lako kuelewa kwamba Mungu anahusika katika maisha yetu na anatujali? Unaweza kuwaomba washiriki wa darasa kusoma Musa 7:28–44 na kutengeneza orodha ya baadhi ya sababu Mungu alikuwa analia. Mistari hii inakufundisha nini kuhusu jinsi Mungu anavyohisi kuhusu watoto Wake? Maelezo kwenye “Nyenzo za Ziada” yanaweza kuchangia kwenye mjadala huu.

  • Muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia unapendekeza kutafakari kile Musa 7:28–31 inachofundisha kuhusu Mungu. Kwa wale waliofanya hili nyumbani wanaweza kuwa tayari kushiriki mawazo yao na darasa. Au ungeweza kuwaomba washiriki wa darasa kutafakari mistari hii na kuijadili katika darasa.

Musa 7:59–67

Bwana atarudi tena katika siku za mwisho.

  • Jinsi gani unaweza kuwasaidia washiriki wa darasa lako kugundua kile Musa 7:59–67 inachofundisha kuhusu Ujio wa Pili wa Mwokozi? Pengine ungeweza kuorodhesha kweli mbili au tatu au matukio kutoka katika mistari hii ubaoni na watake washiriki wa darasa kutafuta katika mistari na kuongeza kwenye orodha. Kwa nini ni baraka kuwa na kumbukumbu ya ono la Henoko—moja ya utabiri wa mwanzo kabisa wa Ujio Wa Pili?

Picha
ikoni ya nyenzo za ziada

Nyenzo za Ziada

Mungu analia kwa ajili ya watoto Wake.

Mzee Jeffrey R. Holland alifundisha:

“Katikati ya ono kuu la binadamu ambalo mbingu ililifunua kwa yeye kuona, Henoko, akiangalia vyote baraka na changamoto za maisha ya kufa, anageuza macho yake kuelekea kwa Baba na anafadhaishwa kumwona akilia. Anasema kwa mshangao na kustaajabu kwa huyu kiumbe mwenye uwezo mkubwa mno katika ulimwengu: ‘Yawezekanaje wewe kulia?’ …

“Kuangalia kuelekea matukio ya takribani siku yoyote, Mungu anajibu: ‘Tazama ndugu zako hawa; wao ni kazi ya ustadi wa mikono yangu mwenyewe. … Niliwapa amri, kwamba yawapasa kupendana, na kwamba yawapasa kunichagua Mimi, Baba yao; lakini tazama, wao hawana urafiki na jamaa zao, nao wanaichukia damu yao wenyewe. … Kwa sababu hiyo mbingu zote hazipaswi kulia, zikiwaona hawa watakaoteseka?’ [Musa 7:29–33, 37].

“Onesho lile moja, lililoribitiwa linafanya zaidi kufundisha uasilia wa kweli wa Mungu kuliko maandiko yoyote ambayo theolojia ingeweza kutoa. … Ni picha gani isiyofutika ya ahadi za Mungu katika maisha yetu! Ni hasira gani kwa mzazi wakati watoto Wake hawamchagui Yeye wala ‘injili ya Mungu Aliyoituma! [Warumi 1:1]. Jinsi gani ilivyo rahisi kumpenda mtu fulani ambaye kwa kipekee anatupenda sisi!” (“Fahari ya Mungu,” Liahona, Nov. 2003, 72).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Wahimize washiriki wa darasa kujifunza maandiko nyumbani. Njia moja unayoweza kuwahimiza kujifunza maandiko nyumbani ni kutoa muda kwa washiriki wa darasa kushiriki uvumbuzi na umaizi kutoka kwenye kujifunza kwao binafsi na kama familia. (Ona Kufundisha Katika Njia ya Mwokozi, 29.)

Chapisha