Agano la Kale 2022
Januari 3–9. Mwanzo 1–2; Musa 2–3: Ibrahimu 4–5: “Hapo Mwanzo Mungu Aliziumba Mbingu na Nchi”


“Januari 3–9. Mwanzo 1–2; Musa 2–3; Ibrahimu 4–5: ‘Hapo Mwanzo Mungu Aliziumba Mbingu na Nchi’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano la Kale 2022 (2021)

“Januari 3–9. “Mwanzo 1–2; Musa 2–3; Ibrahimu 4–5,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2022

Picha
picha ya dunia na mwezi

Januari 3–9

Mwanzo 1–2; Musa 2–3; Ibrahimu 4–5

“Hapo Mwanzo Mungu Aliziumba Mbingu na Nchi”

Ili kujiandaa kufundisha, kwanza soma na kutafakari Mwanzo1–2; Musa 2–3; na Ibrahimu 4–5, na andika misukumo yako ya kiroho. Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia na mawazo hapo chini yanaweza kukusaidia kuelewa na kufundisha maandiko katika sura hizi.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Mungu alirudia mara kwa mara kutangaza kwamba vitu alivyovifanya wakati wa Uumbaji vilikuwa “vizuri” (ona Musa 2:4, 10, 12, 18, 21, 25, 31). Waombe washiriki wa darasa kushiriki vitu vizuri walivyovipata waliposoma maandiko nyumbani wiki hii. Nini kilikuwa kizuri kuhusu vitu walivyogundua?

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Mwanzo 1; Musa 2; Ibrahimu 4

“Mungu Aliziumba Mbingu na Nchi.”

  • Washiriki wa darasa wanaweza kuwa wametambua mifanano na tofauti miongoni mwa maelezo ya Uumbaji katika vitabu vya Mwanzo, Musa, na Ibrahimu. Watie moyo washiriki wa darasa kushiriki kile tafsiri ya Joseph Smith katika Musa 2 inachoongeza kwenye uelewa wetu wa maelezo ya Uumbaji katika Mwanzo 1. Je ni umaizi gani wa ziada tunaoupata kutoka Ibrahimu 4? Kuruhusu watu zaidi kushiriki, ungeweza kutia moyo darasa kufanya ufananisho huu katika jozi au makundi madogo. (Baadhi ya mistari ambayo ina tofauti muhimu imeandikwa kwenye “Nyenzo za Ziada.”) Tunanufaika vipi kutokana na kuwa na maelezo mengi? Ni nini maelezo haya yanapendekeza kuhusu kile Mungu anachotaka sisi tujue kuhusu Uumbaji?

  • Wakati Mungu alipowaumba Adamu na Hawa, Aliwapa mamlaka juu ya nchi na vyote alivyoumba juu yake (ona mwanzo 1:28; Musa 2:28; Ibrahimu 4:28). Jinsi gani Mafundisho na Maagano 59:16–21 na 104:13–18 inatusaidia kuelewa vizuri inamaanisha nini kutumia mamlaka kwa haki juu ya nchi?

  • Siku chache kabla ya darasa, unaweza kuwaomba washiriki wa darasa kuleta picha walizozipiga au walizonazo majumbani mwao ambazo zinawakumbusha juu ya uzuri wa uumbaji wa Mungu. Jinsi gani kujifunza kuhusu kazi ya uumbaji wa Mungu kunaathiri hisia zetu kuhusu Yeye, sisi wenyewe, na nchi? Washiriki wa darasa wangeweza pia kushiriki ujumbe gani wanahisi Mungu anao kwa ajili yetu katika maelezo haya ya Uumbaji katika Mwanzo 1; Musa 2; na Ibrahimu 4. Kuimba au kusikiliza wimbo kuhusu Uumbaji, kama vile “For the Beauty of the Earth” (Nyimbo za Kanisa, namba 92) kungeweza kuwasaidia washiriki wa darasa kuhisi shukrani kwa ajili ya uumbaji wa Mungu.

    Picha
    mfarishi ukifafanua hatua tofauti za uumbaji

    Uumbaji, na Joan Hibbert Durtschi

Mwanzo 1:26–28; Musa 2:26–28; Ibrahimu 4:26–28

Sisi tumeumbwa kwa mfano wa Mungu.

  • Kwa nini ni muhimu kwetu kuelewa kwamba tumeumbwa kwa mfano wa Mungu? Unawezaje kuwasaidia washiriki wa darasa kutafakari ukweli huu? Wangeweza kusoma Mwanzo 1:26–28; Musa 2:26–28; Ibrahim 4:26–28; au aya ya pili ya “Familia: Tangazo kwa Ulimwengu” (ChurchofJesusChrist.org). Jinsi gani ukweli huu unaathiri jinsi tunayojiona wenyewe, wengine, na Mungu? Washiriki wa darasa wangeweza kupata umaizi zaidi katika nyimbo kama vile “O My Father” au “Mimi ni Mtoto wa Mungu” (Nyimbo za Kanisa, na. 292, 301).

  • Katika video “Uumbaji Mkuu wa Mungu” (ChurchofJesusChrist.org), Rais Russell M.Nelson anatoa ushuhuda wa mwili wa kimiujiza wa binadamu (ona pia “Thanks Be to God,” Liahona, Mei 2012, 77–80). Fikiria kushiriki video hii kabla ya kusoma Mwanzo 1:26–28; Musa 2:26–28; au Ibrahimu 4:26–28 kama darasa. Jinsi gani ushuhuda wa Rais Nelson unazidisha shukrani zetu kwa ajili ya kweli katika mistari hii?

Mwanzo 1:27–28; Musa 3:18, 21–25; Ibrahimu 5:14–19

Ndoa kati ya mwanamume na mwanamke imetakaswa na Mungu.

  • Mitazamo mingi juu ya ndoa katika ulimwengu leo imechepuka mbali na ukweli wa milele. Kusaidia darasa lako lijifunze kuhusu mtazamo wa Mungu kuhusu ndoa, unaweza kuwaomba wasome Mwanzo 1:27–28; Musa 3:18, 21–25; au Ibrahimu 5:14–19 na waorodheshe ubaoni kweli wanazopata. Wangeweza kuongeza kwenye orodha yao kweli wanazopata katika ““Familia: Tangazo Kwa Ulimwengu” (ChurchofJesusChrist.org). Kwa nini kweli hizi ni muhimu kwetu?

Picha
ikoni ya nyenzo za ziada

Nyenzo za Ziada

Kufananisha hadithi za Uumbaji.

Mwanzo

Musa

Ibrahimu

Mwanzo

Mwanzo 1:1

Musa

Musa 2:1

Ibrahimu

Ibrahimu 4:1

Mwanzo

Mwanzo 1:16

Musa

Musa 2:16

Ibrahimu

Ibrahimu 4:16

Mwanzo

Mwanzo 1:26–27

Musa

Musa 2:26–27

Ibrahimu

Ibrahimu 4:26–27

Mwanzo

Mwanzo 1:30

Musa

Musa 2:30

Ibrahimu

Ibrahimu 4:30

Mwanzo

Mwanzo 2:5

Musa

Musa 3:5

Ibrahimu

Ibrahimu 4:30

Mwanzo

Mwanzo 2:5

Musa

Musa 3:5

Ibrahimu

Ibrahimu 5:5

Mwanzo

Mwanzo 2:7

Musa

Musa 3:7

Ibrahimu

Ibrahimu 5:7

Mwanzo

Mwanzo 2:9

Musa

Musa 3:9

Ibrahimu

Ibrahimu 5:9

Mwanzo

Mwanzo 2:17–19.

Musa

Musa 3:17–19

Ibrahimu

Ibrahimu 5:13–14

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Wasaidie wanafunzi walinganishe maandiko na wao wenyewe. “Kweli zilezile za injili ambazo zilimtia moyo na kumuidhinisha Ibrahimu, Esta, Lehi, na Joseph Smith zinaweza kuwasaidia wale unaowafundisha kukabiliana na changamoto za kisasa” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 21). Watie moyo wanafunzi kutumia kanuni wanazozipata katika maandiko kwenye hali zao wenyewe.

Chapisha