Agano la Kale 2022
Januari 17–23. Mwanzo 5; Musa 6: “Wafundisheni Watoto Wenu Vitu Hivi kwa Uwazi”


“Januari 17–23. Mwanzo 5; Musa 6: ‘Wafundisheni Watoto Wenu Vitu Hivi kwa Uwazi,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano la Kale 2022 (2021)

“Januari 17–23. Mwanzo 5; Musa 6,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2022

Picha
Adamu na Hawa nje ya Bustani ya Edeni

Pazuri mno kuliko paradiso, na Kendal Ray Johson

Januari 17–23

Mwanzo 5; Musa 6

“Wafundisheni Watoto Wetu Vitu Hivi kwa Uwazi”

Kabla hujasoma nyenzo yoyote ya ziada, soma na utafakari Mwanzo 5 na Musa 6, na uandike misukumo yako ya kiroho. Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia na muhtasari huu vinaweza kukupa mawazo kuhusu jinsi ya kuwasaidia wale unaowafundisha kugundua kweli zinazowahusu.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Jinsi gani unaweza kuwatia moyo washiriki wa darasa kushiriki utambuzi na uzoefu waliokuwa nao walipokuwa wakijifunza Mwanzo 5 na Musa 6? Ungeweza kuyaandika majina Adamu na Henoko ubaoni na waombe washiriki wa darasa waandike kitu fulani ambacho mmoja wa manabii hawa alifanya au kufundisha ambacho kilikuwa na maana kwao.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Musa 6:26–39

Bwana anatuita kufanya kazi yake licha ya mapungufu yetu.

  • Kuna uwezekano mkubwa kwamba mtu fulani katika darasa lako amehisi—au anahisi—upungufu kuhusu wajibu nyumbani au kanisani. Kujenga imani ya washiriki wa darasa kwamba Bwana anaweza kuwasidia, ungeweza kwaomba wasome uzoefu wa Henoko unaopatikana katika Musa 6:26–39. Jinsi gani Mungu alimsaidia Henoko kufanya kazi yake licha ya woga wa Henoko? Waombe washiriki wa darasa kufikiria kuhusu mifano mingine ya watu walioshinda unyonge wao na wakakamilisha kazi ya Bwana, iwe ni kutoka katika maandiko au maisha yao wenyewe. Ni mifano gani tunaweza kushiriki? (Ona pia Kutoka 4:10–16; Yeremia 1:4–10; 2 Nefi 33:1–4; Etheri 12:23–29).

  • Wengi wa mitume na manabii wa leo wameelezea wasiwasi wao unaofanana na wa Henoko wakati walipoelezea jinsi ilivyokuwa kupokea miito yao. Uzoefu wao ungeweza kuongeza uelewa wa washirika wa darasa wa Musa 6:26–39. Fikiria kurejea upya video “On the Lord’s Errand: maisha ya Thomas S. Monson” (churchofJesusChrist.org; kati ya dakika 35:46 na 39:40) au hotuba ya mshiriki wa Akidi ya wale Kumi na wawili aliyeitwa hivi karibuni (kwa mfano, ona shuhuda za Mzee Ronald A. Rasband, Mzee Gary E. Stevenson, na Mzee Dale G. Renland [Liahona, Nov. 2015, 89–94]). Waache washiriki wa darasa washiriki kile kinachowavutia kuhusu mifano hii. Tunaweza kujifunza nini kutoka kwa viongozi hawa kuhusu hisia zetu za upungufu? Kauli kutoka kwa Rais Thomas S. Monson katika “Nyenzo za Ziada” inaweza pia kusaidia kama sehemu ya mjadala huu.

Musa 6:48–65

Imani, toba, ubatizo, na kumpokea Roho Mtakatifu kunatuandaa kurudi kwa Mungu.

  • Muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia unapendekeza kusoma Musa 6:48–62 kutafuta kile kila mmoja wetu lazima ajue na atende ili kukombolewa. Labda washiriki wa darasa wangeweza kushiriki utambuzi wowote ambao ulikuja kutokana na kujifunza kule majumbani mwao. Au mnaweza kujadili Musa 6:48–62 pamoja darasani. Jinsi gani tunaweza kumjibu mtu fulani anayeuliza kwa nini imani, toba, ubatizo, na kumpokea Roho Mtakatifu ni muhimu? Jinsi gani Bwana anajibu swali hili katika mistari 53–65, na tunajifunza nini kutokana na jibu lake?

    Picha
    familia ikisoma maandiko

    Wazazi wanapaswa kuwafundisha watoto wao injili.

Musa 6:51–63

“Wafundisheni Watoto Wenu Vitu Hivi kwa Uwazi.”

  • Katika Musa 6:51–63 Tunajifunza juu ya kweli za injili ambazo Bwana alizifundisha kwa Adamu na kumtaka kuzifundisha kwa uzao utakaokuja. Pengine washiriki wa darasa wangeweza kutengeneza orodha ya kweli hizi kwa kujifunza vifungu vidogo vya mistari, kama vile mistari 51–52, 53–57, 58–60, 61–63. Kwa nini kweli hizi ni za thamani kwa vizazi vinavyoinukia vya leo? Nini ungetaka vijana wajue kuhusu mwokozi kutokana na mistari hii? Washiriki wa darasa wanaweza kuwa radhi kushiriki mawazo au uzoefu ili kusaidiana wao kwa wao kufundisha kweli hizi kwa matokeo yanayotakiwa kwa watoto na vijana. Nini kingine tunaweza kujifunza kutoka katika maelekezo ya Bwana kwa wazazi katika Mosia 4:14–15 na Mafundisho na Maagano 68:25–28; 93:40–50?

  • Kuongezea kwenye kile Musa 6 inachofundisha kuhusu wajibu wa wazazi kwafundusha watoto wao, unaweza kuwaomba washiriki wa darasa kuangalia moja au zaidi ya video zifuatazo: “Parenting: Touching the hearts of our Youth,” “Proclamation Series: Children,” or “Mother in Israel” (ChurchofJesusChrist.org). Tunajifunza nini kutokana na video hizi kuhusu kufundisha injili kwa watoto wetu? Kama unawafundisha vijana, ungeweza kuwaomba kushiriki jinsi wanavyoweza kuwasaidia wazazi wao katika juhudi zao za kufundisha injili nyumbani.

Picha
ikoni ya nyenzo za ziada

Nyenzo za Ziada

“Aitwaye na Bwana, Bwana humstahilisha.”

Rais Thomas S. Monson alifundisha: “Baadhi yenu wanaweza kuwa na aibu kiasili au kujifikiria mwenyewe una mapungufu katika kukubali wito. Kumbuka kwamba kazi hii siyo yako na yangu peke yangu. Hii ni kazi ya Bwana, na wakati tunapokuwa katika kazi ya Bwana, tuna haki ya usaidizi wa Bwana. Kumbuka kwamba aitwaye na Bwana, Bwana humstahilisha.” (“Duty Calls, Ensign, Mei 1996, 44).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Roho Mtakatifu ni Mwalimu. Jukumu lako kama mwalimu ni muhimu, lakini kumbuka kwamba Roho Mtakatifu ni mwalimu wa kweli. Wasaidie washiriki wa darasa kujifunza kutoka kwa Roho na kushiriki na kila mmoja kile wanachojifunza.

Chapisha