Agano la Kale 2022
Januari 10–16. Mwanzo 3–4; Musa 4–5: Anguko la Adamu na Hawa


“Januari 10–16. Mwanzo 3–4; Musa 4–5: Anguko la Adamu na Hawa,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano la Kale 2022 (2021)

“Januari 10–16. Mwanzo 3–4; Musa 4–5,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2022

Picha
Adamu na Hawa, wakitembea pamoja

Adamu na Hawa, na Douglas M. Fryer

Januari 10–16

Mwanzo 3–4; Musa 4–5

Anguko la Adamu na Hawa

Unapojiandaa kufundisha kuhusu Mwanzo 3–4 na Musa 4–5, fikiri kuhusu maswali gani au shughuli zinaweza kuwasaidia washiriki wa darasa kuelewa vyema Anguko la Adamu na Hawa.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Washiriki wa darasa wangeweza kwa kifupi kuangalia upya Mwanzo 3–4 au Musa 4–5, kuchagua mstari ambao upo dhahiri kwao, na kuushiriki na yule aliyeketi karibu nao. Kisha watu wachache wangeweza kushiriki utambuzi na darasa.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Musa 4:1–13; 5:1–12

Tunahitaji uhuru wa kuchagua na upinzani ili tuweze kukua.

  • Kwa sababu uhuru wa kuchagua—haki iliyotolewa na Mungu kufanya chaguzi—ni sehemu muhimu ya maisha ya duniani, sisi wakati mwingine hatulipi umuhimu suala hilo. Kuongeza kwa kina shukrani ya washiriki wa darasa kwa ajili ya zawadi hii, wangeweza kusoma na kujadili Musa 4:1–4. Mistari hii inafundisha nini kuhusu umuhimu wa uhuru wa kuchagua? Kwa nini mpango wa Mungu ungeharibiwa kama tusingekuwa na uhuru wa kuchagua? Dondoo katika “Nyenzo za Ziada” zinaweza kutoa baadhi ya utambuzi.

  • Pengine washiriki wa darasa walijifunza ujumbe wa Rais Dallin H. Oaks “Upinzani katika Vitu Vyote” (Liahona, Mei 2016, 114–17) kama sehemu ya mafunzo yao binafsi au kifamilia wiki hii. Muda wote wa wiki, unaweza kufikiria kuwaalika watu wachache kuja wamejiandaa kushiriki kitu fulani kutoka katika ujumbe wake ambacho kiliwasaidia kuelewa Anguko la Adamu na Hawa (ona hususani sehemu ya I na II). Kwa nini Baba wa Mbinguni anaturuhusu tupate uzoefu wa “upinzani katika vitu vyote”? (ona 2 Nefi 2:11–16). Unaweza kuwaomba washiriki wa darasa kusoma Mafundisho na Maagano 29:39–40 na kujadili kwa nini majaribu ya Shetani ni muhimu katika mpango wa Mungu. Jinsi gani Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wanatusaidia tunapokabiliana na majaribu?

    Picha
    Hawa akishikilia tunda

    Kuondoka Edeni, na Annie Henrie Nader

Musa 4: 4–12; 5:13–33

Shetani anatafuta “kutudanganya na kutupofusha”.

  • Musa 4:4–12; 5:13–33 inaweza kuwasaidia washiriki wa darasa lako kutambua baadhi ya njia ambazo kupitia hizo Shetani anatujaribu kufanya uovu. Unaweza kuwaomba nusu ya darasa kusoma Musa 4:4–12 na nusu nyingine kusoma Musa 5:13, 18–33. Wanaposoma, wangeweza kuorodhesha njia Shetani alizomjaribu Adamu na Hawa na watoto wao. Jinsi gani anajaribu kwa kutumia vitu sawa na hivi leo? Jinsi gani Baba wa Mbinguni anaweza kutusaidia kupinga uongo wa Shetani?

Mwanzo 3:1–7; Musa 4:22–31; 5:4–15

Upatanisho wa Yesu Kristo unatoa matumaini na ukombozi kutokana na Anguko.

  • Tunavyoelewa zaidi athari za Anguko, ndivyo zaidi tunavyokuwa na shukrani kwa upatanisho wa Yesu Kristo. Washiriki wa darasa wangeweza kutafuta athari za Anguko katika Mwanzo 3:1–7; Musa 4:22–31 na kuorodhesha kile wanachopata ubaoni. Kisha wangeweza kutafuta Musa 5:4–12, 14–15 kujifunza kuhusu mpango wa Mungu wa kutukomboa kutokana na athari hizo (ona pia 2 Nefi 2:19–25; Alma 12:22–34) na orodhesha kile wanachokipata ubaoni. Wangeweza pia kushiriki kile kinachowavutia kuhusu shuhuda za Adamu na Hawa za Yesu Kristo zinazopatikana katika mistari 10–12. Jinsi gani tunahisi kuhusu mpango wa Mungu baada ya kusoma maandiko haya?

  • Hadithi ya Adamu na Hawa ya matumaini na ukombozi inaweza kuwatia moyo washiriki wa darasa wakati maisha yanapokuwa magumu. Fikiria kuwaomba kutafuta maneno na virai katika Musa 5:7–12 ambavyo vinaeleza tumaini ambalo Adamu na Hawa walihisi wakati walipojua kwamba Mwokozi angeweza kuwakomboa. Lini tumehisi tumaini sawa na lile Adamu na hawa walilohisi? Fikiria kuwaomba washiriki wa darasa kushiriki nyimbo zao za kanisa wanazozipenda kuelezea tumaini ambalo linakuja kupitia upatanisho wa Mwokozi. Mngeweza kuimba baadhi ya hizi nyimbo pamoja.

Picha
ikoni ya nyenzo za ziada

Nyenzo za Ziada

Tunaweza kujichagulia wenyewe.

Mzee Dale G. Renlund alifundisha:

“Lengo la Baba yetu wa Mbinguni katika malezi siyo kufanya watoto Wake kutenda kile kilicho sahihi; ni kufanya watoto Wake wachague kufanya kile kilicho sahihi na hatimaye kuwa kama Yeye. Kama Yeye angetaka tu sisi tuwe watiifu, Angetumia zawadi na adhabu za papo hapo kushawishi tabia zetu.

“Lakini Mungu hapendezwi na watoto Wake kuwa tu ‘wanyama’ waliofunzwa na watiifu ambao hawataweza kutafuna kwenye ndara Zake katika sebule ya selestia. Hapana, Mungu anataka watoto Wake wakue kiroho na kujiunga Naye katika kazi ya familia” (“Chagueni Hivi Leo,” Liahona, Nov. 2018, 104.).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Zidisha ushiriki wa washiriki wa darasa. Shughuli nyingi zinaweza kufanywa kama darasa, katika vikundi vidogo, au katika jozi. Tumia mbinu mbalimbali ili kuruhusu watu kushiriki wale ambao wasingeweza kwa njia nyingine kupata nafasi. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 33–34.)

Chapisha