Agano la Kale 2022
Januari 24-30. Musa 7: “Bwana Aliwaita Watu Wake Sayuni”


“Januari 24-30. Musa 7: ‘Bwana Aliwaita Watu Watu Wake Sayuni,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano la Kale 2022 (2021)

“Januari 24-30. Musa 7,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2022

Picha
watu wengi wakijumuika katika njia za upendo

Mpendane, na Emma Donaldson Taylor

Januari 24-30

Musa 7

“Bwana Aliwaita Watu Wake Sayuni”

Unaposoma na kutafakari Musa 7, andika misukumo ya kiroho unayopokea. Kwa kufanya hivi, unaonyesha kwamba wewe unathamini mwongozo kutoka kwa Bwana na kwamba unataka kupokea zaidi mwongozo Wake.

Andika Misukumo Yako

Katika historia yote, watu wamekuwa wakijaribu kufanikisha kile Henoko na watu wake walichotimiza: kujenga jumuiya iliyo bora mahali ambapo hakuna umaskini wala vurugu. Kama watu wa Mungu, na sisi tunashiriki hamu hii. Tunaita kujenga Sayuni, na inajumuisha—ikiongezea kwenye kuwajali maskini na kukuza amani—kufanya maagano, kukaa pamoja katika haki, na kuwa wamoja na kila mtu na pamoja na Yesu Kristo, “mfalme wa Sayuni” (Musa 7:53). Kwa sababu kazi ya kujenga Sayuni inaendelea katika siku yetu, ni vyema kuuliza, Je, ni kwa jinsi gani Henoko na watu wake walifanya hilo? Je, ni kwa jinsi gani wao walikuja kuwa “wa moyo mmoja na wazo moja” (Musa 7:18) licha ya uovu ulio wazunguka? Miongoni mwa maelezo mengi ya kina Musa 7 inatufundisha kuhusu Sayuni, la thamani zaidi kwa Watakatifu wa Siku za Mwisho laweza kuwa hili: Sayuni sio mji tu—ni hali ya moyo na roho. Sayuni, kama Bwana alivyofundisha, ni “walio safi moyoni” (Mafundisho na Maagano 97:21). Hivyo pengine njia iliyo bora zaidi kuanza kujenga Sayuni ni kuanza katika mioyo yetu wenyewe na majumbani.

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

Musa 7:16–21, 27, 53, 62–69

Jitihada za Henoko ndiyo mpangilio wa ujenzi wa Sayuni katika maisha yetu wenyewe.

Kwa sababu Musa 7 ni kumbukumbu ya jinsi wafuasi wa Mungu walivyojenga Sayuni kwa mafanikio, inaweza kutuelekeza na kutupa mwongozo wa kiungu leo tunapojitahidi kufanya vivyo hivyo. Zingatia kutumia jedwali kama hili ili kuandika kumbukumbu ya kile unachojifunza kuhusu Sayuni kutoka Musa 7:16–21, 27, 53, 62–69.

Mstari

Je, unajifunza nini wewe kuhusu Sayuni?

Hii inapendekeza nini kuhusu jitihada zako za kujenga Sayuni?

Mstari

7:18

Je, unajifunza nini wewe kuhusu Sayuni?

Watu wa Sayuni walikuwa “wa moyo mmoja na wazo moja”?

Hii inapendekeza nini kuhusu jitihada zako za kujenga Sayuni?

Tunahitaji kuwa wamoja kama familia na kama Kanisa.

Mstari

7:21

Je, unajifunza nini wewe kuhusu Sayuni?

“Baada ya muda, [Sayuni] ilichukuliwa kwenda mbinguni.”

Hii inapendekeza nini kuhusu jitihada zako za kujenga Sayuni?

Kujenga Sayuni ni mchakato wa pole pole.

Mstari

Je, unajifunza nini wewe kuhusu Sayuni?

Hii inapendekeza nini kuhusu jitihada zako za kujenga Sayuni?

Mstari

Je, unajifunza nini wewe kuhusu Sayuni?

Hii inapendekeza nini kuhusu jitihada zako za kujenga Sayuni?

Musa 7:18–19, 53

Watu wa Mungu wanapaswa kujitahidi kuwa “wa moyo mmoja na wazo moja”?

Musa 7:18–19 imeorodhesha tabia muhimu za watu ambao Bwana aliwaita Sayuni. Je ni kwa nini unadhani tabia hizi ni za lazima ili kujenga Sayuni? Je, ni kwa jinsi gani Sayuni, kama inavyoelezwa katika mlango huu, ni tofauti na vikundi vingine vya muungano au taasisi ulimwenguni? Unapotafakari swali hili, ungeweza kufikiri kuhusu maneno haya ya Yesu Kristo katika mstari wa 53: “Mimi ni Masiya, Mfalme wa Sayuni.” Je, inamaanisha nini kuwa na Yesu Kristo kama Mfalme? Je, ni kwa jinsi gani Yeye hutusaidia sisi kukuza tabia za Sayuni?

Ona pia Wafilipi 2:1–5; 4 Nefi 1:15–18; Mafundisho na Maagano 97:21; 105:5.

Picha
watu wakisalimiana

Tujitahidi kuwa “wa moyo mmoja na wazo moja” (Musa 7:18).

Musa 7:21, 23–24, 27, 69

Je, ni nini kilitokea kwenye mji wa Henoko?

Vifungu vya maneno “twaliwa juu” (Musa 7:21, 23), “inuliwa juu” (Musa 7:24), “wakanyakuliwa” (Musa 7:27), na “imekimbia” (Musa 7:69) vinataja Sayuni na watu wa Heneko walibadilishwa na kutwaliwa mbinguni. Watu ambao wamebadilishwa “wamebadilika ili kwamba wasionje maumivu au mauti” kama wenye mwili wenye kufa (Mwongozo wa Maandiko, “Viumbe Waliobadilishwa,” “Zion,” scriptures.ChurchofJesusChrist.org; ona pia 3 Nefi 28:4–9, 15–18, 39–40).

Musa 7:28–69

Mungu hulia kwa ajili ya watoto Wake.

Baadhi ya watu humwona Mungu kama kiumbe wa mbali na asiye guswa na hisia kwa yale yanayotokea kwetu. Lakini Henoko aliona ono ambamo ndani yake Mungu alilia kwa ajili ya watoto Wake. Unaposoma Musa 7:28–40, tafuta sababu za Mungu kulia. Katika sehemu iliyobakia ya ono la Henoko, lililoelezewa katika Musa 7:41–69, ni ushahidi gani unaupata kwamba Mungu ni “mwenye huruma na mkarimu milele”? (Musa 7:30; ona mstari wa 43, 47, na 62 kwa ajili ya mifano).

Musa 7:62

Katika siku za mwisho Mungu atakusanya wateule Wake.

Mstari wa 62 unaelezea matukio ya siku za mwisho. Zingatia vifungu vya maneno kama hivi vinaweza kumaanisha nini: “haki nitaishusha chini kutoka mbinguni,” “ukweli nitausogeza mbele kutoka duniani,” “haki na ukweli nitasababisha kuifagia nchi kama vile kwa gharika.” Je, vifungu hivi vya maneno vinakufundisha nini wewe kuhusu kazi ya Mungu katika siku hizi za mwisho?

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

Musa 7:18–19.Ili kusaidia washiriki wa familia kupata taswira ya kile kinachomaanishwa kuwa “wa moyo mmoja,” pengine ungeweza kutengeneza moyo wa karatasi na ukate katika vipande vya fumbo, vipande vya kutosha kwa kila mshiriki wa familia kuwa na kimoja. Washiriki wa familia wangeweza kuandika majina yao juu ya vipande vyao na kisha wafanye kazi pamoja ili kuunganisha moyo huo. Wakati wakikamilisha fumbo mnaweza kuongelea kuhusu mambo mnayopenda kuhusu kila mwanafamilia.

Musa 7:28–31, 35.Tunajifunza nini kuhusu Mungu kutoka kwenye aya hizi?

Musa 7:32.Je, ni kwa nini Mungu alitupatia sisi haki ya kujiamulia? Je, tunaweza kusema nini kwa mtu ambaye anahisi amri za Mungu zinaweka kikomo cha haki yetu ya kujiamulia? Kusoma 2 Nefi 2:25–27 kunaweza kuongeza kwenye mjadala huu.

Musa 7:59–67.Familia yako inaposoma Musa 7:59–67, jaribu kuweka alama au kutambua vitu ambavyo Bwana alimwambia Henoko kuhusu siku za mwisho—kwa mfano, kwamba Mungu “atawakusanya wateule [Wake]” (mstari wa 62) na kwamba kutakuwa na “dhiki kubwa miongoni mwa waovu” (mstari wa 66). Je, tunawezaje kuwa na imani na matumaini licha ya uovu katika siku za mwisho? Kama sehemu ya mjadala, zingatia kusoma maneno haya kutoka kwa Mzee Ronald A. Rasband: “Jipeni moyo, akina kaka na akina dada. Ndio, tunaishi katika nyakati zenye hatari kubwa, lakini tukibaki katika njia ya agano, hatuhitaji kuogopa. Ninawabariki kuwa mnapofanya hivyo, hamtatatizwa na nyakati ambamo tunaishi au na shida zinazowakabili. Ninawabariki ili mchague kusimama katika sehemu takatifu na wala msiondoshwe. Ninawabariki ili muamini katika ahadi za Yesu Kristo, kwamba Yeye yu hai na kwamba anatulinda, anatujali na anasimama pamoja nasi” (“Msifadhaike,” Liahona, Nov. 2018, 21).

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “Love at Home,” Kitabu cha Nyimbo za Kanisa, na. 294.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Kuwa makini. Unapokuwa makini na kile kinachotokea katika maisha ya watoto wako, utapata fursa nzuri sana za kufundisha. Maoni na maswali ya watoto wako kwa siku nzima yanaweza pia kuelekeza kwenye nyakati zinazowezekana kufundisha. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi,16.)

Picha
Picha ya rangi ya Henoko na watu wakiangalia juu kuelekea kwenye mwangaza

Mji wa Sayuni Ulitwaliwa , na Del Parson

Chapisha