Agano la Kale 2022
Januari 24–30. Musa 7: “Bwana Aliwaita Watu Wake Sayuni”


“Januari 24–30. Musa 7: ‘Bwana Aliwaita Watu Wake Sayuni,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Agano la Kale 2022 (2021)

“Januari 24–30. Musa 7,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2022

Picha
watu wakijumuika katika njia za upendo

Mpendane Nyinyi kwa Nyinyi, na Emma Donaldson Taylor

Januari 24–30

Musa 7

“Bwana Aliwaita Watu Wake Sayuni”

Anza maandalizi yako kwa kusoma Musa 7. Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia inaweza kukusaidia kuelewa sura hii, na maoni hapa chini yanaweza kukupa mawazo juu ya jinsi ya kuifundisha kwa watoto.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Chukua dakika chache kuwaruhusu watoto kupitia nawe yale wanayoyajua juu ya nabii Henoko—pamoja na kitu chochote walichojifunza katika somo la wiki iliyopita. Ikiwa inasaidia, onyesha picha kutoka muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Watu Binafsi na Familia.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

Musa 7:18

Mungu anatutaka sisi tupendane.

Aya hizi zinaelezea tabia ya watu wa Sayuni. Unawezaje kusaidia watoto kuanza kukuza sifa hizi?

Shughuli Yamkini

  • Shiriki hadithi za watu wa Henoko kutoka “Henoko Nabii” (katika Hadithi za Agano La Kale), au acha watoto wasimulie hadithi kwa maneno yao kwa kutumia picha ya Henoko muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia. Pia unaweza kuimba na watoto mstari wa pili wa “Follow the Prophet” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 110–11) ili kurejelea hadithi.

  • Wasaidie watoto wafikirie vitendo vinavyohusiana na kifungu “moyo mmoja na nia moja” (Musa 7:18). Fafanua kuwa kifungu hiki kinamaanisha kuwa watu wa Henoko walipendana na walikuwa wenye wema kwa kila mmoja wao. Waalike watumie ukurasa wa shughuli wa wiki hii kuonyesha njia wanazoweza kuonyesha upendo.

  • Imbeni wimbo kuhusu kupendana kila mmoja, kama vile “Upendo Nyumbani“ (Nyimbo za Kanisa, na. 294). Leta picha zinazoonyesha misemo muhimu kwenye wimbo ili kuwasaidia watoto kujifunza maneno. Waombe watoto kushiriki njia ambazo wanaweza kuonyeshana upendo katika Msingi na katika nyumba zao. Kisha acha watoto waigize mawazo yao.

Picha
msichana akishiriki tunda na mwanamke mzee

Tunapaswa kujitahidi kuwa “wa moyo mmoja na nia moja” (Musa 7:18).

Musa 7:28–33

Mungu huwajali watoto Wake.

Unaweza kusaidia watoto kujifunza kwamba Baba wa Mbingu na Yesu Kristo hujali sana kuhusu sisi na matendo yetu.

Shughuli Yamkini

  • Wasaidie watoto wafikirie mambo ambayo hufanya Baba wa Mbinguni afurahi. Soma Musa 7:28 pamoja na watoto, na uwaeleze kwamba Baba wa Mbinguni alikuwa na huzuni kwa sababu watu walikuwa waovu sana (ona mistari ya 32–33).

  • Acha watoto wachore uso wenye furaha upande mmoja wa karatasi na uso wa huzuni upande mwingine. Taja matendo kadhaa mazuri, kama kutoa sala, na zingine mbaya, kama kusema uwongo, na waombe watoto wachukue uso wenye furaha au uso wenye huzuni kuonyesha jinsi Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wangehisi juu ya kila chaguo.

  • Waalike watoto kucheza mchezo ambao wataigiza mambo wanayoweza kufanya ambayo yanamfanya Baba wa Mbinguni afurahi. Waombe watoto wengine kukisia ni nini kinafanywa na watoto hao. Shiriki na kila mmoja wa watoto jambo ambalo umewaona wakifanya ambalo linafanya Baba wa Mbinguni afurahi.

Musa 7:59–67

Yesu atakuja tena duniani.

Katika maono yake, Henoko aliona siku za mwisho, pamoja na Ujio wa Pili wa Mwokozi. Je, utawezaje kuwasaidia watoto kutazamia Ujio wa Pili?

Shughuli Yamkini

  • Waambie watoto wafikirie kuwa mgeni maalum anakuja kuwatembelea. Wangefanya nini kujiandaa kwa ziara hiyo? Shiriki maneno ya Bwana kwa Henoko katika Musa 7:60: “Nitakuja katika siku za mwisho.” Je, ni njia zipi ambazo tunaweza kuzitumia kuandaa kwa ujio mwingine wa Yesu?

  • Onyesha picha za nyakati ambazo Mwokozi aliwatokea watu (ona Kitabu cha Sanaa ya Injili, na. 60, 82, 83, na 84). Je, Watu wanafanya nini kwenye picha? Je, Watu wangehisije walipokutana na Yesu? Acha watoto washirikiane jinsi wanavyohisi juu ya kumwona Yesu wakati atakapokuja.tena.

  • Imbeni wimbo kuhusu Ujio wa Pili wa Mwokozi, kama vile “He Sent His Son” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 82–83), na waulize watoto kwamba itakuwaje wakati Yesu atakaporudi tena.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

Musa 7:18–21, 62–63, 68–69

Tunaweza kuunganishwa kama watu wa Sayuni walivyokuwa.

Unaposoma juu ya Sayuni, tafakari juu ya mifano ya umoja ambayo umeiona. Unawezaje kusaidia watoto kujifunza kuunganika kama watu wa Henoko?

Shughuli Yamkini

  • Waulize watoto kutafuta maneno ambayo yanawaelezea watu wa Henoko, pia hujulikana kama Sayuni, wanaposoma Musa 7:18. Andika maneno haya kama vichwa vya habari juu ya ubao, na uwaombe watoto waandike, chini ya kila kichwa cha habari, vitu wanavyoweza kufanya ili kuwa kama watu wa Henoko. Baada ya kushiriki, waulize watoto jinsi ya kufanya nyumba zao kuwa kama Sayuni. Pia wanaweza kutafuta mawazo katika 4 Nefi 1:15–18.

  • Waombe watoto wengine kuhesabu ni mara ngapi neno “Sayuni” limeonekana katika Musa 7:18–21, 62–63, 68–69. Kila wakati neno linapoonekana, wasaidie watoto kutambua kile ambacho kifungu kinasema kuhusu Sayuni (tazama pia Mwongozo wa Maandiko, “Sayuni,” scriptures.ChurchofJesusChrist.org). Ni kwa jinsi gani tunaweza kuwa zaidi kama watu walioelezewa katika mistari hii?

  • Tumia ukurasa wa shughuli ya wiki hii kusaidia watoto kufikiria juu ya njia ambazo wanaweza kuwa “wa moyo mmoja na akili moja” (ona Musa 7:18).

Musa 7:28–37

Mungu analia kwa ajili ya watoto Wake.

Unawezaje kusaidia watoto kugundua kuwa Mungu anatujali na matendo yetu?

Shughuli Yamkini

  • Waulize watoto nini kinaweza kumfanya Mungu kulia (ona Musa 7:28–31). Waalike watoto kutafuta Musa 7:32–33, 37 kwa ajili ya majibu. Mistari hii inatufundisha nini sisi kuhusu jinsi Mungu anavyohisi juu ya watoto Wake? Je, tunajuaje kuwa Mungu anatupenda? Shiriki ushuhuda wako wa upendo wa Mungu kwetu.

  • Rusha begi la maharagwe au mpira kwa mtoto. Muombe amalizie kifungu “naweza kumfanya Mungu afurahi kwa … ”na kisha rusha kitu kwa mtoto mwingine. Rudia mpaka kila mtoto awe amejumuishwa.

Musa 7:60–67

Yesu Kristo atakuja tena katika siku za mwisho.

Unaposoma juu ya ujio wa Pili katika Musa 7:60–67, fikiria jinsi ya kuwafundisha watoto kuhusu hilo kwa njia ya kufurahisha.

Shughuli Yamkini

  • Soma pamoja Musa 7:60–67, na wasaidie watoto kutambua vitu ambavyo Bwana anasema vitatokea katika siku za mwisho. Waulize ni kipi kati ya matukio haya wanayatarajia na kwa nini.

  • Waalike watoto wazungumze juu ya wakati ambapo walimngojea mtu atembelee au arudi nyumbani. Watoto walihisije? Walifanya nini ili kuwa tayari? Je, tunawezaje kujiandaa kumuona tena Yesu?

  • Onyesha picha ya Ujio wa Pili wa Mwokozi (kwa mfano ona Kitabu cha Sanaa ya Injili, na. 66). Acha watoto wachore picha yao wenyewe ya Ujio wa Pili, kwa kuzingatia mambo waliyoyasoma katika Musa 7:60–67.

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Ni kwa jinsi gani unaweza kuwahimiza watoto na familia zao kuendelea kujifunza kutoka katika Agano la Kale nyumbani? Kwa mfano, watoto wangeweza kushiriki kitu fulani walichochora au kupaka rangi katika darasa la Msingi kama sehemu ya somo la jioni la nyumbani.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Wasaidie watoto kuwa makini. “Unapowafundisha watoto, waruhusu kujenga, kuchora, kupaka rangi, kuandika, na kubuni. Vitu hivi ni zaidi ya shughuli za kufurahisha—ni muhimu katika kujifunza” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 25).

Chapisha