Agano la Kale 2022
Desemba 27–Januari 2. Musa 1; Ibrahimu 3: “Hii ni Kazi Yangu na Utukufu Wangu”


“Desemba 27–Januari 2. Musa 1; Ibrahimu 3: ‘Hii Ni Kazi Yangu na Utukufu Wangu,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Agano la Kale 2022 (2021)

“Desemba 27–Januari 2. Musa 1; Ibrahimu 3,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2022

Picha
picha ya nyota angani

Desemba 27–Januari 2

Musa 1; Ibrahimu 3

“Hii ni Kazi Yangu na Utukufu Wangu”

Unaposoma kile Mungu alichowaambia Musa na Ibrahimu, fikiria juu ya kile Anachoweza kusema kwa watoto unaowafundisha. Je, Utawasaidiaje kuhisi upendo Wake kwao?

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Wakati mwingine wimbo unaweza kuwasaidia watoto kukumbuka kile wanachojifunza. Piga au imba kwa kufumba mdomo noti chache za mziki za “Mie Mwana wa Mungu” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 2–3),na waache watoto wafikirie wimbo. Wasaidie watoto wafikirie njia ambazo wazazi wao na wengine “huwaelekeza, huwaongoza” na huwasaidia kutafuta njia.”

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

Musa 1:1–4, 6

Mimi ni mtoto wa Mungu.

Unajifunza nini kutoka Musa 1:1–4, 6 kuhusu uhusiano wako na Baba wa Mbinguni? Unawezaje kuwasaidia watoto kujifunza maana ya kuwa mtoto wa Mungu?

Shughuli za Yakini

  • Soma kwa watoto kile ambacho Mungu alimwambia Musa: “Wewe ni mtoto wangu” (Musa 1:4). Mwalike mtoto aje mbele ya chumba, na uwaombe watoto warudie nawe, “[Jina la mtoto], wewe ni mtoto wa Mungu.” Rudia maneno kwa kila mtoto katika darasa.

  • Onyesha picha kadhaa za watoto, na uulize darasa ikiwa watoto hawa wote ni watoto wa Mungu. Sisitiza kwamba kila mtu ni mtoto wa Mungu. Wafanye watoto wachukue zamu kuangalia katika kioo, na ushuhudie kwamba wao ni watoto wa Mungu pia.

  • Imbeni““Mimi Mwana wa Mungu” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 2–3) pamoja na watoto. Wafanye wapake rangi ukurasa wa shughuli wa wiki hii, na wautumie kuukuraha huo kurejelea ukweli ambao wimbo huu unafundisha.

    Picha
    Yesu Kristo kati ya nyota

    Kristo na Uumbaji, na Robert T. Barrett

Ibrahimu 3:22-28

Niliishi na Baba wa Mbinguni kabla sijazaliwa.

Kujua juu ya maisha yetu kabla ya hapa duniani kunaweza kutia moyo kufanya chaguzi kulingana na ukweli wa milele. Unaposoma Ibrahimu 3:22-28, fikiria jinsi utakavyofundisha watoto juu ya utambulisho chao cha milele.

Shughuli Yamkini

  • Tumia “Kuhusu Agano la Kale” (katika Hadithi za Agano la Kale) kufundisha watoto juu ya maisha yetu kabla ya hapa duniani. Baada ya hapo, waalike watoto kurudia hadithi kwa kukusimulia wewe. Je, ni kwa nini Baba wa Mbinguni ametuleta hapa duniani? Wasaidie watoto kugundua jibu unavyosoma kwao Ibrahimu 3:25.

  • Imba pamoja na watoto wimbo kuhusu mpango wa Mungu kwetu(kama vile “I will Follow God’s Plan” [Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 164–65]). Wasaidie kuelewa kweli za milele zilizofundishwa katika mistari ya wimbo.

Musa 1:39

Baba wa Mbinguni ananitaka mimi kuishi na Yeye tena.

Ni jinsi gani kweli katika Musa 1:39 zimebariki maisha yako? Je! Unaweza kufanya nini kusaidia watoto kupata baraka hizo pia?

Shughuli Yamkini

  • Waonyesha misemo ya “hii ni kazi yangu” na “uzima wa milele” katika Musa 1:39, na uwasaidie watoto kuirudia misemo. Waambie watoto juu ya kazi unazofanya kila siku. Wafundishe kuwa kazi ya Baba wa Mbingu ni kutusaidia kupata uzima wa milele, ambayo inamaanisha kuwa kama Yeye na kuishi naye tena.

  • Alika mzazi aje darasani na azungumze kuhusu anavyohihisi wakati mtoto anarudi nyumbani baada ya kuwa mbali (kwa mfano, shuleni au misheni), au shiriki hisia ambazo umekuwa nazo wakati wa uzoefu huu. Tumia mfano huu kufundisha watoto jinsi gani Baba wa Mbinguni anataka turejee kwake.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

Musa 1:4, 30, 37–39; Ibrahimu 3:22–28

Mimi ni mtoto wa Mungu, na anataka kunisaidia mimi kurejea Kwake.

Musa 1:4, 37–39 na Ibrahimu 3:22–28 fundisha kweli zenye thamani kuhusu uhusiano wetu na Mungu na kusudi lake la kututuma duniani. Tafakari jinsi utakavyowasaidia watoto kujifunza kweli hizi.

Shughuli Yamkini

  • Soma na Watoto Musa 1:4, 37–39 na Ibrahimu 3:24–25. Wape nafasi za kuuliza maswali na kushiriki maneno au misemo inayopendwa kutoka aya hizi. Tunajifunza nini kutoka kwenye mistari hii kuhusu Baba wa Mbinguni? kuhusu sisi wenyewe?

  • Waonyeshe watoto picha kadhaa za uumbaji za Baba wa Mbinguni. Soma Musa 1:30, na eleza kwamba Musa alimuuliza Mungu juu ya madhumuni ya viumbe hivi. Wasaidie watoto kutafuta kwenye mstari wa 39 kupata jibu la Mungu. Shuhudia kwamba kusudi la Mungu ni kumsaidia kila mtoto kupata uzima wa milele.

  • Wasaidie watoto wafikirie hali ambazo watalazimika kuchagua ikiwa watafanya au kutokufanya “mambo yote yale ambayo Bwana Mungu wao atawaamuru” (Ibrahimu 3:25). Waweke wafanye mazoezi au wajadili majibu yamkini ya hali hizo. Je, Mwokozi anawezaje kutusaidia wakati tunafanya chaguzi mbaya?

Musa 1:12–26

Naweza kuhimili vishawishi vya Shetani.

Unapojifunza Musa 1:12–26, tafuta vitu ambavyo Musa alifanya kumpinga Shetani. Ni kwa jinsi gani mfano wa Musa unaweza kuwasaidia watoto wanapokabiliana na majaribu?

Shughuli Yamkini

  • Fupisha uzoefu wa Musa katika Musa 1:12–26 kwa maneno yako mwenyewe, au muombe mmoja wa watoto afanye hivyo (tazama pia video “I Am a Son of God” [ChurchofJesusChrist.org]). Alika watoto watafute vifungu hivi ili kujifunza jinsi Musa alivyoweza kumshinda Shetani. Kama wanahitaji msaada, waelekeze kwenye mistari ya 13, 15, 18, 20–22, 26.)

  • Lete sanduku la vifaa (au picha za vifaa), na uweke lebo kila kifaa na njia ambayo tunaweza kukataa majaribu (kama kuomba, kuimba wimbo, kusoma maandiko, au kutumikia wengine). Acha kila mtoto achukue kifaa na azungumze juu ya hali wakati hatua iliyoandikwa kwenye lebo ya kifaa hicho inaweza kutusaidia kupinga majaribu. Someni pamoja mistari ya 25–26, na ushuhudie kwamba Mungu atatusaidia wakati tunapokabiliana na majaribu.

Ibrahimu 3:22–28

Niliishi na Baba wa Mbinguni kabla sijazaliwa.

Mistari hii inayoelezea maono ya Ibrahimu juu ya maisha yetu kabla ya kuja hapa duniani inaweza kuwasaidia watoto kujibu maswali “Nilitoka wapi?” na “Kwa nini nipo hapa?” Je, ni kwa jinsi gani unaweza kuwasaidia kutafuta majibu?

Shughuli Yamkini

  • Kwenye ubao, andika maswali yanayohusiana na Ibrahimu 3:22–28, kama vile Ni nini kilitokea katika maisha yetu kabla ya kuzaliwa? Nani alikuwepo? Kwa nini dunia iliumbwa? Waalike watoto kusoma mistari kutafuta majibu.

  • Ikiwa kuna mtoto mchanga katika wadi, waalike wazazi wamlete darasani na washiriki hisia zao juu ya kumkaribisha mtoto huyu ulimwenguni. (Unaweza pia kuonyesha picha ya mtoto mchanga.) Ongea na watoto juu ya wapi roho ya mtoto huyu ilikuwa kabla ya yeye kuja duniani. Kwa nini ni muhimu kwa mtoto huyu kujifunza kwamba yeye ni mtoto wa Mungu?

  • Imbeni nyimbo kuhusu mpango wa Mungu kwa ajili yetu, kama vile “I Know My Father Lives” au “I Will Follow God’s Plan” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto 5, 164–65). Waalike watoto kuchora picha zinazoendana na maneno. Acha watumie picha zao kufundishana kweli kutoka kwenye nyimbo.

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Fikiria njia ambazo kujifunza ambako kumetokea katika darasa lako la Msingi kunaweza kutia moyo, kuunga mkono, au kuimarisha mafunzo yanayotokea katika nyumba za watoto. Kwa mfano, unaweza kuwaalika watoto kushiriki ukurasa wa shughuli ya wiki hii na familia zao.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Watoto hujifunza kwa njia nyingi. Watoto wanafurahia kujifunza kupitia uzoefu mpya na tofauti tofauti. Tumia shughuli zinazowasaidia kusogea sehemu moja hadi nyingine, kutumia milango yao yote ya fahamu, na kujaribu vitu vipya. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 25–26.)

Chapisha