Agano la Kale 2022
Januari 3–9. Mwanzo 1–2; Musa 2-3; Ibrahimu 4–5: “Hapo Mwanzo Mungu Aliziumba Mbingu na Nchi”


“Januari 3–9. Mwanzo 1–2; Musa 2–3; Ibrahimu 4–5: ‘Hapo Mwanzo Mungu Aliziumba Mbingu na Nchi,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Agano la Kale 2022 (2021)

“Januari 3–9. Mwanzo 1–2; Musa 2–3; Ibrahimu 4–5,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2022

Picha
picha ya dunia na mwezi

Januari 3–9

Mwanzo 1–2; Musa 2–3; Ibrahimu 4–5

“Hapo Mwanzo Mungu Aliziumba Mbingu na Nchi”

Unaposoma Mwanzo 1–2, Musa 2–3, na Ibrahimu 4–5, fikiria juu ya watoto unaowafundisha, na tafakari ni kweli gani unaweza kuwasaidia kuelewa kutoka katika sura hizi.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Waalike watoto kushiriki kitu ambacho Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wameumba ambacho wanashukuru. Kuonyesha picha kwenye muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia ingeweza kuwapa mawazo.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

Musa 2

Yesu aliumba dunia.

Kujua juu ya Uumbaji kunaweza kuwasaidia watoto kuhisi upendo wa Mungu na kuongeza kuthamini kwao ulimwengu. Ni kwa jinsi gani unaweza kuufanya Uumbji uwe wa kutia moyo?

Shughuli Yamkini

  • Waonyeshe watoto picha za vitu ambavyo vinawakilisha vipindi tofauti vya Uumbaji (kama ilivyoelezewa katika Musa 2; pia ona “Yesu Kristo Aliumba Dunia,” katika Hadithi za Agano la Kale), na uwasaidie watoto kufikiria matendo yanayoendana sanjari na picha. Kwa mfano, wanaweza kutengeneza ngumi kuwakilisha nchi kavu au kupunga mikono yao kama mawimbi ya maji (ona Musa 2:9–10). Shiriki ushuhuda wako kwamba Yesu Kristo alifanya vitu hivi kwa sababu Yeye na Baba wa Mbinguni wanatupenda sisi.

  • Imbeni wimbo kuhusu vitu ambavyo Yesu Kristo aliviumba kwa ajili yetu, kama vile “The World Is So Lovely” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto,233). Waombe watoto kuchora picha za uumbaji ulioelezewa katika wimbo.

    Picha
    mfarisi unaoonyesha hatua tofauti za uumbaji

    Uumbaji, na Joan Hibbert Durtschi

Musa 2:26-27

Niliumbwa kwa mfano wa Mungu.

Wakati watoto wanaelewa kuwa waliumbwa kwa mfano wa Mungu, wanaweza kukuza hali ya unyenyekevu na heshima kwa miili yao wenyewe na ya wengine.

Shughuli Yamkini

  • Wasaidie watoto kurudia “Mimi, Mungu, nimemuumba mwanadamu kwa mfano wangu mimi” mara kadhaa (Musa 2:27). Fafanua kuwa Baba wa Mbingu aliumba miili yetu iwe sawa na wa kwake. waalike watoto kuonyesha sehemu ya miili yao kama unavyoipa jina, au kuimba wimbo juu ya miili yetu, kama vile“Head, Shoulders, Knees, and Toes” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto,275).

  • Waalike watoto waigize vitu ambavyo wanaweza kufanya na miili yao, wakati watoto wengine wakibashiri kile kinachofanywa. Waalike watoto kushiriki kwa nini wanashukuru kwa miili yao.

  • Chora picha ya mwili kwenye karatasi, na tengeneza fumbo la kuunganisha vipande kwa kuikata katika vipande kadhaa. Gawa vipande hivyo, na waacha watoto wafanye kazi kwa pamoja ili kuviweka pamoja kuunda mwili. Waombe watoto kushiriki vitu ambavyo wanaweza kufanya na kila sehemu iliyokatwa. Shiriki ushuhuda wako kwamba miili yetu imeumbwa kwa mfano wa Mungu.

Musa 3:2–3

Siku ya Sabato ni takatifu.

Watoto wanaokuza tabia ya kuitakasa siku ya Sabato wakiwa wadogo ni rahisi zaidi kuitii amri hii wakati maisha yanapokuwa magumu na yenye kuhitaji zaidi.

Shughuli Yamkini

  • Soma Musa 3:2–3, na waombe watoto wasikilize kile ambacho Mungu alifanya siku ya saba. Leta picha (au chora michoro rahisi) ya vitu tunavyofanya siku ya Jumapili ili iwe siku takatifu na vitu vya kufanya katika siku zingine. Acha watoto wachanganue picha hizo katika mafungu mawili, fungu moja kwa ajili ya Jumapili na moja kwa ajili ya siku zingine. Shuhudia kwa nini ni muhimu kuitakasa siku ya Sabato.

  • Siku chache kabla ya darasa, mualike mmoja wa watoto na wazazi wake wajiandae kushiriki vitu wanavyofanya katika familia zao ili kuitakasa siku ya Sabato. Waalike watoto wengine kushiriki yale ambayo familia zao hufanya.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

Musa 2

Yesu Kristo aliumba dunia chini ya uongozi wa Baba wa Mbinguni.

Unaweza kutumia Musa 2 kuwasaidia watoto kuona kwamba dunia iliumbwa kwa kusudi kama sehemu ya mpango wa Mungu. Unaposoma sura hizi, ni mawazo gani yanayokuja akilini ambayo yanaweza kusaidia kuimarisha ushuhuda wa watoto kwenye Uumbaji?

Shughuli Yamkini

  • Wasaidie watoto kufikiria nyakati ambapo walitengeneza kitu kwa kufuata maelekezo ya mtu mwingine. Kwa mfano, labda waliandaa mapishi wakati mzazi au ndugu akiwaongoza. Andika Nani aliumba dunia? ubaoni, na waalike watoto kutafuta jibu katika Musa 2:1. Shuhudia kwamba Yesu Kristo aliumba dunia chini ya uongozi wa Baba wa Mbinguni.

  • Mpe kila mtoto kifungu kwenye Musa 2 kinachohusiana na moja ya siku za uumbaji, na muombe achore picha ya vitu ambavyo Baba wa Mbingu na Yesu waliumba siku hiyo. Waombe watoto kushikilia picha zao na kusimama katika mpangilio wa siku za Uumbaji, na kisha mualike kila mtoto kufundisha watoto wengine yale yaliyotokea katika siku waliyopangiwa. Je, tunajifunza nini juu ya Baba wa Mbingu na Yesu Kristo kutoka kwenye hadithi ya Uumbaji?

Musa 2:26–27

Adamu na Eva waliumbwa kwa mfano wa Mungu.

Dunia itawapa watoto ujumbe mwingi wa uongo kuhusu miili yao. Mafundisho katika Musa 2:26–27 ni motisha yenye nguvu ya kuheshimu na kutunza miili yetu.

Shughuli Yamkini

  • Someni pamoja Musa 2:26–27. Ni nini mistari hii hutufundisha kuhusu miili yetu? Onyesha video “God’s Greatest Creation” (ChurchofJesusChrist.org), au cheza mchezo “Your Body Is a Temple” (Friend, Aug. 2019, 24–25). Unaweza pia kusoma nukuu zinazohusiana kutoka kwa ujumbe wa Rais Russell M. Nelson “Your Body: A Magnificent Gift to Cherish” (New Era, Aug. 2019, 2–7) hiyo itasaidia watoto kuhisi shukrani kwa Baba wa Mbinguni kwa ajili ya miili yao.

  • Chora kielelezo cha mwili kwenye ubao, na uwaalike watoto kuchagua sehemu ya mwili na uandike pembezoni mwa sehemu hiyo kwa nini wanashukuru kwa kuwa na hiyo sehemu. Elezea shukrani yako kwa ajili ya mwili wako, na ushuhudie ya kwamba tuliumbwa kwa sura ya Mungu.

Mwanzo 2:2–3

Siku ya Sabato ni takatifu.

Watoto wanaweza kulazimika kuelezea marafiki zao kwa nini wao wanaifanya Jumapili tofauti na siku zingine. Mwanzo 2:2–3 inafundisha kwa nini siku ya Sabato ni siku takatifu. Unaweza kufanya nini kuwasaidia watoto kuelewa vizuri na kuelezea fundisho hili?

Shughuli Yamkini

  • Kuitakasa siku ya Sabato kunaonyeshaje upendo wetu na heshima yetu kwa Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo? Wasaidie watoto kuigiza matukio ambapo wanamuelezea rafiki kwa nini wanachagua kufanya mambo Jumapili ambavyo huonyesha heshima kwa Baba wa Mbinguni na Yesu. Pendekeza kwamba watumie Mwanzo 2:2–3 na 5:2 katika maelezo yao.

  • Wape watoto dakika chache waandike orodha ya vitu vingi ambavyo wanaweza kufikiria ambavyo wanaweza kufanya ili Sabato iwe siku takatifu. Waalike watoto kushiriki orodha zao, na wahimize waongeze kwenye orodha zao kwani wengine wanashiriki maoni ambayo hawakufikiria. Pendekeza kwamba watoto waende na orodha hizo nyumbani kwao na wazirejelee wakati wanahitaji maoni ya vitu vizuri vya kufanya siku ya Sabato.

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Wasaidie watoto wafikirie juu ya jinsi wanavyoweza kufanya shughuli na familia zao sawa na ile uliyoifanya darasani. Unaweza kutaka kuwasaidia kuandika muhtasari ili kujikumbusha.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Wasaidie watoto kuelezea ubunifu wao. Watoto wanapojenga, kuchora, au kupaka rangi kitu kinachohusiana na hadithi au kanuni wanayojifunza, mara nyingi wanaikumbuka vizuri zaidi. Wahimize kutumia uumbaji wao kuzifundisha familia zao. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 25.)

Chapisha