Agano la Kale 2022
Januari 3-9. Mwanzo 1–2; Musa 2–3; Ibrahimu 4–5: “Hapo Mwanzo Mungu Aliumba Mbingu na Nchi”


“Januari 3-9. Mwanzo 1- 2; Musa 2- 3; Ibrahimu 4- 5 ‘Hapo Mwanzo Mungu Aliumba Mbingu na Nchi,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano la Kale 2022 (2021)

“Januari 3-9. Mwanzo 1–2; Musa 2–3; Ibrahimu 4–5,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2022

Picha
picha ya dunia na mwezi

Januari 3-9

Mwanzo 1–2; Musa 2–3; Ibrahimu 4–5

“Hapo Mwanzo Mungu Aliumba Mbingu na Nchi”

Hata kama umesoma kuhusu Uumbaji kabla, daima kuna mengi ya kujifunza kutoka katika maandiko. Omba kwa ajili ya mwongozo kutoka kwa Roho Mtakatifu ili akusaidie kupata uelewa mpya.

Andika Misukumo Yako

Kwa sababu ulimwengu uliotuzunguka ni mzuri sana na wa kifahari, ni vigumu kufikiria kuwa dunia ilikuwa “wazi, na haina mtu,” “utupu na yenye ukiwa” (Mwanzo 1:2; Ibrahimu 4:2). Kitu kimoja hadithi ya Uumbaji inatufundisha ni kuwa Mungu anaweza kufanya kitu kikubwa kutokana na kitu kisicho na umbile. Hilo ni la msaada kukumbukwa wakati maisha yanapoonekana kuwa ya vurugu. Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo ndio Waumbaji, na kazi Zao za ubunifu kwetu sisi hazijaisha. Wao wanaweza kufanya nuru ikaangaza katika nyakati za kiza katika maisha yetu. Wanaweza kutengeneza sakafu kavu katikati ya bahari zenye dhoruba za maisha yetu. Wanaweza kuviamuru vitu vya asili, na kama tutatii neno Lao kama vitu hivyo vilivyofanya, Wao wanaweza kutubadilisha sisi kuwa viumbe vizuri kama tulivyokusudiwa kuwa. Hiyo ni sehemu ya kile kinachomaanishwa kuumbwa katika sura ya Mungu, kwa mfano Wake (ona Mwanzo 1:26). Tunao uwezekano wa kuwa kama Yeye: kuinuliwa, kutukuzwa, viumbe wa selestia.

Kwa ajili ya muhtasari wa kitabu cha Mwanzo, ona “Mwanzo” katika Kamusi ya Biblia.

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

Mwanzo 1:1–25; Musa 2:1–25; Ibrahimu 4:1–25

Chini ya maelekezo ya Baba wa Mbinguni, Yesu Kristo aliumba nchi.

Mzee D. Todd Christofferson alisema, “Maelezo ya kina yawayo yoyote juu ya mchakato wa uumbaji, tunajua kwamba haikuwa kama ajali bali ni kwamba ulielekezwa na Mungu Baba na kutekelezwa na Yesu Kristo” (“Kwa Nini Ndoa, Kwa nini Familia,” Liahona, Mei 2015, 51). Wakati kukiwa na mengi tusiyoyajua kuhusu namna kamili jinsi ulimwengu ulivyoumbwa, tafakari kile unachojifunza kuhusu Uumbaji kutokana na kile Mungu alichokifunua katika Mwanzo 1:1–25; Musa 2:1–25; na Ibrahimu 4:1–25. Je, umetambua nini katika hadithi hizi ambacho ni cha kufanana? Je, umetambua nini ambacho ni cha tofauti? Je, ni mawazo gani unayo kuhusu Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wakati unaposoma kuhusu Uumbaji?

Ona pia Mafundisho na Maagano 101:32–34.

Picha
mfarishi ukionyesha hatua tofauti za uumbaji

Uumbaji, na Joan Hibbert Durtschi

Mwanzo 1:27–28; 2:18–25; Musa 3:18, 21–25; Ibrahimu 5:14–19

Ndoa kati ya mwanamume na mwanamke imetawazwa na Mungu.

“Adamu na Hawa waliunganishwa pamoja katika ndoa kwa muda na kwa milele zote kwa uwezo wa ukuhani usio na mwisho” (Russell M. Nelson, “Lessons from Eve,” Ensign, Nov. 1987, 87). Kwa nini huu ni ukweli muhimu kujua? Tafakari hili unaposoma Mwanzo 1:27–28; 2:18–25; Musa 3:18, 21–25; na Ibrahimu 5:14–19. Kama ungependa kujifunza zaidi kuhusu ndoa ndani ya mpango wa Mungu, soma na utafakari nyenzo zilizoorodheshwa hapa chini. Je, nyenzo hizi zinakushawishi kufanya nini ili kuboresha ndoa yako au kujiandaa kwa ajili ya ndoa katika wakati ujao?

Ona pia Mathayo 19:4–6; 1 Korintho 11:11; Linda K. Burton, “Tutapaa Pamoja,” Liahona, Mei 2015, 29–32; “Familia: Tangazo kwa Ulimwengu,” ChurchofJesusChrist.org.

Mwanzo 2:2–3; Musa 3:2–3; Ibrahimu 5:2–3

Mungu aliibariki na kuitakasa siku ya Sabato.

Mungu aliifanya siku ya Sabato kuwa takatifu, na Yeye anatutaka sisi tuishike kitakatifu. Mzee David A. Bednar alifundisha, “Sabato ni muda wa Mungu, muda mtakatifu uliowekwa mahususi kwa ajili ya kumwabudu Yeye na kwa ajili ya kupokea na kukumbuka ahadi zake kuu na za thamani” (“Ahadi za Thamani Kuu Kupita Kiasi,” Liahona, Nov. 2017, 92). Je, ni kwa jinsi gani ungetumia maelezo haya na Mwanzo 2:2–3; Musa 3:2–3; au Ibrahimu 5:2–3 kumwelezea mtu kwa nini wewe unachagua kuiheshimu siku ya Sabato? Je, ni kwa jinsi gani Bwana amekubariki kwa kuifanya siku Yake kuwa takatifu?

Ona pia Isaya 58:13–14; Mafundisho na Maagano 59:9–13; “The Sabbath Is a Delight” (video), ChurchofJesusChrist.org.

Picha
family study icon

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

Mwanzo 1:1–25; Musa 2:1–25; Ibrahimu 4:1–25.Ni kwa jinsi gani unaweza kufanya kujifunza kuhusu Uumbaji kuwa ya kufurahisha kwa ajili ya familia yako? Ungeweza kuipeleka nje familia yako kuchunguza aina ya vitu ambavyo vilifanyika wakati wa kila historia ya kipindi cha Uumbaji, kama vile nyota, miti, au wanyama. Ungeweza pia kuonyesha picha za vitu vilivyoumbwa katika kila kipindi na mwalike mshiriki wa familia kuziweka picha hizo katika mpangilio baada ya kusoma moja ya hadithi za Uumbaji kwa pamoja. Je, vitu hivi vilivyoumbwa vinatufundisha nini kuhusu Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo?

Mwanzo 1; Musa 2; Ibrahimu 4.Njia mojawapo ya kusoma hadithi ya Uumbaji ni kuialika familia yako kutafuta ni mara ngapi katika Mwanzo 1 au Musa 2 Mungu aliviita vitu ambavyo amevifanya kuwa ni “vyema.” Je, hii inapendekeza nini kuhusu jinsi tunavyopaswa kuvitendea vitu vilivyoumbwa na Mungu—ikijumuisha na sisi wenyewe? Je, tunajifunza nini kutokana na njia ambayo matukio haya yametamkwa katika Ibrahimu 4?

Mwanzo 1:26–27; Musa 2:26–27; Ibrahimu 4:26–27.Kwa nini ni muhimu kujua kwamba tuliumbwa katika sura ya Mungu? Je, ni kwa jinsi gani hii inagusa jinsi tunavyojisikia kuhusu sisi wenyewe, wengine, na Mungu?

Kama una watoto wadogo, mnaweza kusoma pamoja Musa 2:27 na kucheza mchezo rahisi: Onesha picha ambayo ina mchoro wa Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo, kama vile picha namba 90 katika Kitabu cha Sanaa za Injili (2009), na waombe wana familia kupokezana kuonyesha sehemu yenye mwili wa Baba wa Mbinguni au Yesu Kristo. Kisha wanafamilia wengine wangeweza kuonyesha sehemu kama hiyo katika miili yao.

Mwanzo 1:28; Musa 2:28; Ibrahimu 4:28.“Amri ya Mungu kwa watoto Wake kuongezeka na kuijaza dunia inabaki kuwa na nguvu” (“Familia: Tangazo kwa Ulimwengu,” ChurchofJesusChrist.org). Wanafamilia wanaweza kuigiza jinsi ya kuelezea imani yetu kuhusu amri hii kwa wale ambao hawajui juu ya ukweli huu au ambao wanaamini tofauti.

Mwanzo 1:28; Musa 2:28; Ibrahimu 4:28.Je, ina maanisha nini “kutawala … juu ya kila kilicho hai kitambaacho juu ya dunia”? (Ona pia Mafundisho na Maagano 59:16–21). Je, ni kwa jinsi gani familia yetu inaweza kutimiza jukumu letu la kuitunza dunia?

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “My Heavenly Father Loves Me,” Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 228–29.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Kutumia maandiko katika maisha yetu. Baada ya kusoma kifungu cha maandiko, waalike wanafamilia kukitumia katika maisha yao. Kwa mfano, ni kwa namna gani Musa 3:1–3 inatumika kwetu sisi katika kuitunza Sabato kila wiki? (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 21.)

Picha
Yesu Kristo amesimama kwenye mawingu.

Uumbaji, na Annie Henrie Nader

Chapisha