Agano la Kale 2022
Januari 10-16. Mwanzo 3–4; Musa 4–5: Anguko la Adamu na Hawa


“Januari 10-16. Mwanzo 3–4; Musa 4–5: Anguko la Adamu na Hawa,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano la Kale 2022 (2021)

“Januari 10-16. “Mwanzo 3–4; Musa 4-5,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2022

Picha
Adamu na Hawa wakitembea pamoja

Adamu na Hawa, na Douglas M. Fryer

Januari 10–16

Mwanzo 3–4; Musa 4–5

Anguko la Adamu na Hawa

Unapojifunza Mwanzo 3–4 na Musa 4–5, zingatia kile ambacho Bwana anajaribu kukufundisha. Andika ukweli huu na mawazo yako ya kiroho, kisha uyatafakari wiki hii yote.

Andika Misukumo Yako

Mwanzoni, hadithi ya Anguko la Adamu na Hawa yaweza kuonekana kama jambo liletalo huzuni. Adamu na hawa wakafukuzwa nje ya Bustani ya Edeni Wakatupwa ulimwenguni mahali ambapo maumivu, huzuni, na kifo daima vipo (ona Mwanzo 3:16–19). Na walitengwa na Baba yao wa Mbinguni. Lakini kwa sababu ya ukweli uliorejeshwa kupitia Nabii Joseph Smith katika kitabu cha Musa, tunajua kwamba hadithi ya Adamu na Hawa hakika ni hadithi moja ya matumaini—na ni sehemu muhimu ya mpango wa Mungu kwa watoto Wake.

Bustani ya Edeni ilikuwa nzuri. Lakini Adamu na Hawa walihitaji kitu kilichokuwa zaidi ya mazingira mazuri. Walihitaji—na sote tunahitaji—fursa ya kukua. Kuondoka Bustani ya Edeni ilikuwa jambo muhimu la kwanza kuelekea kurudi kwa Mungu na hatimaye kuwa kama Yeye. Hii ilimaanisha kukabiliana na upinzani, kufanya makosa, kujifunza kutubu na kumwamini Mwokozi, ambaye Upatanisho Wake unafanya uwezekano wa kukua na “shangwe ya ukombozi wetu” (Musa 5:11). Kwa sababu hiyo unaposoma kuhusu Anguko la Adamu na Hawa, usilenge kwenye kinachoonekana kama jambo la huzuni bali juu ya uwezekano—siyo juu ya paradiso Adamu na Hawa waliyoipoteza bali juu ya utukufu ambao uchaguzi wao ambao umeruhusu sisi kuupokea.

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

Mwanzo 3:1–7; Musa 4; 5:4–12

Anguko lilikuwa sehemu muhimu ya mpango wa Mungu ili kuwakomboa watoto Wake

Anguko la Adamu na Hawa lilileta kifo cha kimwili na cha kiroho ulimwenguni. Pia lilileta shida, huzuni na dhambi. Hivi vyote vinaonekana kama ni sababu za kujutia Anguko. Lakini Anguko lilikuwa sehemu ya mpango wa baba wa Mbinguni kwa ajili ya kuwakomboa na kuwainua watoto Wake kupitia “dhabihu ya Mwana Pekee wa Baba” (Musa 5:7). Unaposoma Mwanzo 3:1–7; Musa 4; 5:4–12, ni kweli gani unazipata ambazo zinakusaidia kuelewa Anguko na jinsi Upatanisho wa Yesu Kristo unavyolishinda? Maswali kama haya yanaweza kusaidia:

  • Je, ni kwa jinsi gani Anguko liliwaathiri Adamu na Hawa? Je, ni kwa jinsi gani linaniathiri mimi?

  • Je, ni kwani nini Adamu na Hawa walitoa dhabihu? Je, dhabihu hizo zilikuwa ni ishara ya nini? Je, ninaweza kujifunza nini kutokana na maneno ya malaika katika mistari hii?

  • Je, ni kwa nini Adamu na Hawa walikuwa na “furaha” baada ya Anguko lao? Je ninajifunza nini kutoka katika hadithi hii kuhusu mpango wa Mungu kunikomboa mimi kupitia Yesu Kristo?

Kwa sababu ya Kitabu cha Mormoni na mafunuo mengine ya siku za mwisho, tunao mtazamo wa kipekee juu ya Anguko. Kwa mfano, zingatia kile nabii Lehi alichowafundisha familia yake kuhusu Adamu na Hawa katika 2 Nefi 2:15–27. Je ni kwa jinsi gani mafundisho ya Lehi yanafafanua kile kilichotokea katika Bustani ya Edeni na kinavyotusaidia sisi kuelewa kwa nini ilikuwa muhimu?

Ona pia 1 Wakorintho 15:20–22; Mosia 3:19; Alma 12:21–37; Mafundisho na Maagano 29:39–43; Makala ya Imani 1:3; Dallin H. Oaks, “Mpango Mkuu,” Liahona, Mei 2020, 93–96; Dallin H. Oaks, “Upinzani katika Mambo Yote,” Liahona, Mei 2016, 114–17; Jeffrey R. Holland, “Mahali Haki, Upendo, na Huruma Hukutana,” Liahona, Mei 2015, 104–6.

Picha
Hawa ameshika tunda

Kuondoka Edeni, na Annie Henrie Nader

Mwanzo 3:16; Musa 4:22

Inamaanisha nini Adamu kuwa “mtawala” wa Hawa?

Kifungu hiki cha maandiko wakati mwingine kimeeleweka vibaya kwa kumaanisha kwamba mwanamume anahalalishwa katika kumtendea mkewe vibaya. Katika siku yetu, manabii wa Bwana wamefundisha kwamba wakati mume anapaswa kuongoza katika nyumba kwa haki, anapaswa kumuona mke wake kama wenza walio sawa (ona “Familia: Tangazo kwa Ulimwengu” [ChurchofJesusChrist.org]). Mzee Dale G. Renlund na Dada Ruth Lybbert Renlund wanaeleza kwamba mume mwenye haki “atatafuta kutumikia; atatambua kosa na atatafuta msamaha; atakuwa mwepesi kutoa sifa; atajali mapendeleo ya washiriki wa familia; atauona uzito mkuu wa wajibu wa kutoa ‘mahitaji muhimu ya maisha na ulinzi’ kwa ajili ya familia yake; atamtendea mke wake kwa heshima ya hali ya juu na kwa staha. … Ataibariki familia yake” (The Melchizedek Priesthood: Understanding the Doctrine, Living the Principles [2018], 23).

Musa 5:4–9, 16–26

Mungu ataikubali dhabihu yangu kama nitatoa kwa moyo ulio radhi na wa utiifu.

Adamu na Hawa walijifunza kwamba dhabihu za wanyama zilikuwa ni ishara ya dhabihu ya Kristo ya kulipia dhambi, na walifanya hilo “lijulikane kwa wana na mabinti zao” (Musa 5:12). Unapojifunza Musa 5:4–9, 16–26, zingatia mitizamo tofauti ya wana wao wawili, Kaini na Habili, juu ya dhabihu hizi. Je, ni kwa nini Bwana aliikubali dhabihu ya Habili lakini sio ya Kaini?

Je, ni aina gani ya dhabihu Bwana anaitaka kutoka kwako? Je, kuna kitu cho chote katika Musa 5:4–9, 16–26 ambacho kinabadilisha njia ambayo wewe unafikiria kuhusu dhabihu hizo?

Ona pia Zaburi 4:5; 2 Wakorintho 9:7; Omni 1:26; 3 Nefi 9:19–20; Moroni 7:6–11; Mafundisho na Maagano 97:8; Jeffrey R. Holland, “Tazameni Mwana Kondoo wa Mungu,” Liahona, Mei 2019, 44–46.

Picha
ikoni ya kujifunza kaama familia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko kama Ffamilia na Jioni ya Nyumbani

Mwanzo 3; Musa 4.Je, unaweza kufanya nini ili kusaidia familia yako kuelewa vyema Anguko la Adamu na Hawa? Ungeweza kunakili picha kutoka “Adamu na Hawa” (katika Hadithi za Agano la Kale) na kuzikata. Kisha mnaweza kufanya kazi pamoja kuziweka picha katika mpangilio wakati mkijadili tukio hili la Adamu na Hawa. Je, ni kwa nini Anguko lilikuwa muhimu katika mpango wa wokovu wa Baba wa Mbinguni? Kuangalia video ya “The Fall” (ChurchofJesusChrist.org) inaweza kusaidia kujibu swali hili.

Musa 4:1–4.Je, tunajifunza nini kuhusu Mungu, Yesu Kristo na Shetani kutoka mistari hii? Je, ni kwa nini haki ya kujiamulia ni muhimu sana kwa mpango wa Mungu ambapo Shetani alitaka kuiharibu?

Musa 5:5–9.Je, Mungu aliwaamuru Adamu na Hawa kufanya nini ili kuwasaidia wao kufikiria kuhusu Mwokozi? Je, Mungu ametupatia nini sisi ili kutusaidia kufikiria kuhusu Mwokozi?

Musa 5:16–34.Je, ina maanisha nini kuwa “mlinzi wa kaka yangu”? Je, ni kwa jinsi gani tunaweza kutunzana vyema kama familia?

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “Choose the Right Way,” Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 160–61.

Kuboresha Kujifunza Binafsi

Tumia vielelezo vya kujifunza maandiko. Unapojifunza maandiko, tumia tanbihi, Mwongozo wa Mada, Kamusi ya Biblia, Mwongozo wa Maandiko, na vielelezo vingine vya kujifunza maandiko ili kupata utambuzi wa nyongeza.

Picha
Malaika amewatembelea Adamu na Hawa

Mfanano, na Walter Rane

Chapisha