Scripture Stories
Adamu na Hawa


“Adamu na Hawa,” Hadithi za Agano la Kale (2022)

“Adamu na Hawa,” Hadithi za Agano la Kale

Mwanzo 2–3; Musa 3–5; Ibrahimu 5

Adamu na Hawa

Kupata uzoefu kwa kufanya chaguzi

Picha
Adamu na Hawa pamoja na wanyama

Adamu na Hawa walikuwa watoto wa kwanza wa Baba wa Mbinguni kuishi duniani. Waliishi ndani ya Bustani nzuri ya Edeni, wakiwa wamezungukwa na aina zote za mimea na miti. Mungu Baba yetu wa Mbinguni na Bwana Yesu Kristo waliwatembelea na kuzungumza nao.

Mwanzo 2:8–9; 3:8; Musa 3:8­–9; Ibrahimu 5:8, 14–19

Picha
mti wa ujuzi wa mema na mabaya

Mungu aliwaacha wale matunda ya kila mti isipokuwa mmoja. Ikiwa wangekula kutoka mti wa ujuzi wa mema na mabaya, wangepaswa kuondoka bustanini na hatimaye wangekufa. Shetani aliwadanganya Adamu na Hawa. Shetani alisema ikiwa wangekula tunda, wangejua mema na mabaya lakini hawangekufa.

Mwanzo 2:16–17; 3:1–5; Musa 3:9; 4:6–11; Ibrahimu 5:9, 12–13

Picha
Hawa akichuma tunda

Hawa alichagua kula tunda.

Mwanzo 3:5–6; Musa 4:12

Picha
mikono imeshikilia tunda

Hawa alimpa Adamu sehemu ya tunda. Adamu pia alichagua kula tunda.

Mwanzo 3:6–7; Musa 4:12

Picha
Adamu na Hawa wakijificha kutoka kwa Mungu na Yesu

Mungu na Bwana waliwatembelea, lakini Adamu na Hawa waliogopa na walijificha. Mungu aliuliza ikiwa walikuwa wamekula tunda la mti wa ujuzi wa mema na mabaya.

Mwanzo 3:8–13; Musa 4:13–14

Picha
Adamu na Hawa wakiondoka katika Bustani ya Edeni

Adamu na Hawa walimwambia Mungu kwamba walichagua kula tunda. Kwa sababu ya uchaguzi wao, walitakiwa kuondoka kwenye Bustani ya Edeni. Walitengwa na Mungu, lakini Yeye alikuwa na mpango kwa ajili yao. Sasa walijua mema na mabaya na wangeweza kupata watoto

Mwanzo 3:16–24; Musa 4:15–31

Picha
Familia ya Adamu na Hawa wakitazama moto

Adamu na Hawa waliahidi kutii amri zote za Mungu. Walifundishwa kutoa sadaka za wanyama. Wakati walipotii, walijifunza zaidi kuhusu Yesu Kristo Mwana wa Mungu. Wote walihisi shangwe kubwa kwa sababu Yeye angeisaidia familia yao kurudi kwa Mungu.

Mwanzo 3:23; Musa 5:1–12

Chapisha