Scripture Stories
Ayubu


“Ayubu,” Hadithi za Agano la Kale (2021)

“Ayubu,” Hadithi za Agano la Kale

Ayubu 1–3; 19; 38–42

Ayubu

Kutumaini katika upendo wa Bwana

Picha
Ayubu pamoja na familia wakila mlo wa usiku

Ayubu alikuwa mtu mwema aliyempenda Bwana na kushika amri Zake. Yeye na mke wake walikuwa na watoto 10, na alikuwa na makundi mengi ya mifugo na utajiri mkubwa.

Ayubu 1:1–5

Picha
Ayubu akitazama upepo mkali

Bwana aliruhusu imani ya Ayubu ijaribiwe. Ayubu alipitia mambo magumu.

Ayubu 1:6–12

Picha
Nyumba ya Ayubu ikiungua moto.

Siku moja wanyama wengi wa Ayubu waliibiwa. Baadaye moto ulichoma mali yote ya Ayubu na kuua watumishi wake wote na wanyama wengine. Kisha upepo mkali ukaangusha nyumba ya mwana wa Ayubu. Watoto wa Ayubu walikuwa ndani, na wote wakafa. Ayubu na mke wake hawakuwa na chochote kilichowabakia isipokuwa afya zao.

Ayubu 1:13–19

Picha
Ayubu na mke wake wakisali

Ayubu na mke wake walikuwa na huzuni. Walipoteza kila kitu, hata watoto wao. Lakini bado Ayubu alikuwa na imani katika Bwana. Hakumlaumu Bwana kwa kile kilichotokea.

Ayubu 1:20–22

Picha
Mke wa Ayubu akimlisha Ayubu mgonjwa

Ayubu kisha akaugua sana. Madonda makali yalijaa kwenye mwili wake. Ayubu na mke wake walijiuliza kwa nini mambo haya yote mabaya yalikuwa yanatokea.

Ayubu 2:7–9; 3:1–11

Picha
Yesu akimwonyesha Ayubu ulimwengu

Bwana alizungumza na Ayubu na kumwonyesha dunia, nyota na viumbe hai vyote. Bwana alimfundisha Ayubu somo muhimu. Vitu vyote viliumbwa ili kuwasaidia watoto wa Baba wa Mbinguni kujifunza kuhusu Mwanawe Yesu Kristo na kumfuata Yeye.

Ayubu 38–41

Picha
Ayubu na familia

Ayubu alitubu na kumuomba Bwana amsamehe kwa kuwa na shaka. Aliahidi kumtumaini Bwana. Bwana alijua kuwa Ayubu alimpenda. Alimponya Ayubu na kumbariki kwa watoto wengi zaidi na mara mbili ya utajiri aliokuwa nao mwanzoni.

Ayubu 19:25–2642

Chapisha