Scripture Stories
Malaki Nabii


“Malaki Nabii,” Hadithi za Agano la Kale (2022)

“Malaki Nabii,” Hadithi za Agano la Kale

Malaki 13

Malaki Nabii

Kuishi sheria ya zaka

Picha
watu wakitoa zaka mbaya

Wayahudi walilipa zaka kwa kutoa sehemu moja ya kumi ya mazao na wanyama wao kwa Bwana. Bwana aliwabariki walipolipa zaka. Lakini baadhi ya Wayahudi walianza kutoa mkate mbovu au mnyama asiyeona au mgonjwa kama zaka. Wakabakisha kilicho bora kwa ajili yao wenyewe.

Mwanzo 14:20; 28:22; Kumbukumbu la Torati 12:6, 11, 17; Malaki 1:7–8, 12–13

Picha
Malaki akifundisha watu

Bwana hakupendezwa. Malaki nabii, aliwaambia Wayahudi walikuwa wakimwibia Bwana walipokuwa siyo waaminifu katika kulipa zaka. Malaki aliwaambia watubu.

Malaki 3:8–9

Picha
Malaki akiwaangalia watu wakitoa zaka ya uaminifu.

Bwana aliwapa Wayahudi ahidi. Kama watatoa zaka ya uaminifu, Bwana angewamwagia baraka kubwa kutoka mbinguni.

Malaki 3:10–12

Chapisha