Scripture Stories
Malkia Esta


“Malkia Esta,” Hadithi za Agano la Kale (2022)

“Malkia Esta,” Hadithi za Agano la Kale

Esta 2–5; 7–9

Malkia Esta

Shujaa wakati wa hatari

Picha
Esta ndani ya jumba la mfalme

Baadhi ya Waisraeli waliitwa Wayahudi. Esta alikuwa Myahudi aliyeishi Persia. Wazazi wake walikufa, hivyo binamu yake Mordekai alimtunza. Alialikwa kwenye jumba la mfalme pamoja na wasichana wengine katika ufalme. Mfalme alitaka malkia mpya, na alimchagua Esta.

Esta 2:2–7;16–17

Picha
watu wakimsujudia Hamani

Mfalme alikuwa na mtumishi aliyeitwa Hamani ambaye alipandishwa cheo kuwa na nguvu kubwa. Hamani alimsaidia mfalme kuongoza nchi. Mfalme alimfanya kila mmoja kumsujudia Hamani.

Esta 3:1–2

Picha
Mordekai na Hamani

Lakini Mordekai hakumsujudia Hamani. Mordekai angemsujudia Bwana pekee. Hii ilimfanya Hamani awe na hasira. Alitaka kumwadhibu Mordekai na Wayahudi wote.

Kutoka 20:5; Esta 3:5–6, 8

Picha
askari akitoa tangazo kwa kundi la watu

Hamani alimwambia mfalme kwamba Wayahudi hawakufuata sheria za mfalme. Hivyo mfalme alimruhusu Hamani kutengeneza sheria mpya: siku moja iliyopangwa, Wayahudi wote wangeuawa.

Esta 3:8–11, 13

Picha
Mordekai akizungumza na Esta

Mordekai alimwomba Esta azungumze na mfalme. Mfalme angeweza kubadilisha sheria ya Hamani na kuwaokoa Wayahudi. Lakini Esta alikuwa na hofu. Wakati mwingine mfalme aliwaua watu waliokwenda kuzungumza naye bila ya mwaliko.

Esta 4:5–11

Picha
Esta akiwatazama watu

Mordekai alimwomba Esta awafikirie Wayahudi ambao wangeuawa. Mordekai alisema Bwana yawezakuwa alimweka Esta kwenye jumba la mfalme ili awaokoe Wayahudi.

Esta 4:13–14

Picha
Esta akiomba

Esta alifahamu kwamba alilazimika kuzungumza na mfalme, hata ikiwa ingemaanisha kwamba angeuawa. Esta aliwaomba Wayahudi wote na watumishi wake wafunge pamoja naye.

Esta 4:15–16

Picha
Esta akitazama milango

Baada ya kufunga kwa siku tatu, Esta alijitayarisha na kwenda kuonana na mfalme.

Esta 5:1

Picha
Esta akimsujudia mfalme

Wakati alipomkaribia mfalme, mfalme alimnyooshea fimbo yake. Hii ilimaanisha mfalme alifurahi kumwona na asingemuua. Alimuuliza ni nini alichotaka. Esta alimwambia mfalme kwamba watu wake walikuwa hatarini. Kwa sababu ya sheria ya Hamani, yeye pamoja na Wayahudi wote katika ufalme wangeuawa.

Esta 5:2–3; 7:4–6

Picha
askari akitoa tangazo kwa watu

Mfalme alimkasirikia Hamani na kuamuru auawe. Mfalme alitengeneza sheria mpya ambayo iliwalinda Wayahudi. Sasa waliruhusiwa kujilinda ikiwa yeyote angejaribu kuwaumiza.

Esta 7:9–10;8:10–11

Picha
Esta

Imani ya Esta katika Bwana na ujasiri wake wa kuzungumza na mfalme viliwaokoa watu wake. Badala ya kifo na huzuni, kulikuwa na sherehe. Wayahudi walisherehekea.

Esta 8:16–17; 9:18–32

Chapisha