Scripture Stories
Shadraka, Meshaki, na Abednego


“Shadraka, Meshaki, na Abednego,” Hadithi za Agano la Kale (2022)

“Shadraka, Meshaki, na Abednego,” Hadithi za Agano la Kale

Danieli 1; 3

Shadraka, Meshaki, na Abednego

Jaribu hatari la imani

Picha
Mfalme Nebukadreza na sanamu ya dhahabu

Mfalme Nebukadreza alitengeneza sanamu kubwa, ya dhahabu na kuwalazimisha watu wake waiabudu. Ikiwa wangekataa, wangetupwa kwenye tanuru la moto.

Danieli 1:6–7; 3:1–6

Picha
Shadraka, Meshaki, na Abednego

Marafiki wa Danieli Shadraka, Meshaki, na Abednego walimpenda Mungu na hawangemwabudu mungu wa uongo wa mfalme. Mfalme alikuwa na hasira juu yao.

Danieli 3:6–15

Picha
Shadraka, Meshaki, na Abednego wakizungumza na mfalme

Marafiki watatu walimwambia mfalme kwamba wangemwabudu Mungu pekee. Waliamini Mungu angeweza kuwalinda. Lakini hata ikiwa Asingewalinda, wangesimamia kile walichokiamini.

Danieli 3:15–18

Picha
wanaume watatu pamoja na malaika ndani ya moto

Mfalme alikuwa na ghadhabu juu ya Shadraka, Meshaki, na Abednego. Alisababisha watupwe ndani ya tanuru la moto. Lakini mfalme alipotazama ndani ya tanuru, alishangazwa kuona kiumbe wa mbinguni ndani ya moto akiwa na wanaume watatu. Hawakuunguzwa na moto.

Danieli 3:19–25

Picha
wanaume watatu wakitoka nje ya moto

Mfalme aliwaita Shadraka, Meshaki, na Abednego, na walitoka nje ya tanuru. Moto haukuwadhuru au hata kuchoma nguo zao.

Danieli 3:26–27

Picha
Shadraka, Meshaki, na Abednego wakizungumza na mfalme

Shadraka, Meshaki, na Abednego walitii amri za Mungu, hata wakati maisha yao yalipokuwa hatarini. Mfano wao ulimsaidia mfalme kumwamini Mungu.

Danieli 3:28–29

Chapisha