Scripture Stories
Eliya Nabii


“Eliya Nabii,” Hadithi za Agano la Kale (2022)

“Eliya Nabii,” Hadithi za Agano la Kale

1 Wafalme 16–18

Eliya Nabii

Imani ya mama na miujiza ya Bwana

Picha
Eliya akizungumza na Mfalme Ahabu na Malkia Yezebeli

Ufalme wa Israeli haukuwa na mvua na maji yalikuwa yakikaribia kuisha. Mfalme Ahabu na Malkia Yezebeli hawakuwapenda manabii wa Bwana. Walisababisha hata baadhi ya manabii kuuawa. Mfalme na malkia waliomba kwa miungu kwa ajili ya mvua. Lakini nabii Eliya aliwaambia kwamba Bwana asingeleta mvua kwa miaka mingi.

1 Wafalme 16:29–33; 17:1; 18:13

Picha
Eliya akijificha kutoka kwa askari

Mfalme na malkia walimkasirikia Eliya. Bwana alimuonya Eliya ajifiche kwa sababu maisha yake yalikuwa hatarini.

1 Wafalme 17:2–3

Picha
Eliya akiwa amepiga magoti ndani ya kijito

Bwana alimuongoza Eliya kwenye kijito na kutuma ndege kumletea chakula. Lakini kwa sababu hakukuwa na mvua, kijito kilikauka na Eliya hakuwa na maji.

1 Wafalme 17:4–7

Picha
Eliya akizungumza na mwanamke

Bwana alimuongoza Eliya kwa mwanamke kwenye mji wa mbali. Eliya alimuomba maji na mkate. Lakini alikuwa na kiasi cha kuwatosha tu yeye na mtoto wake kwa siku moja zaidi.

1 Wafalme 17:8–12

Picha
Eliya akizungumza na mwanamke

Eliya alifahamu kuwa kilikuwa chakula chake cha mwisho. Alimuahidi mwanamke kwamba ikiwa atampa chakula, Bwana angetoa chakula kwa ajili ya familia yake mpaka mvua zitakaporejea.

1 Wafalme 17:13–14

Picha
Eliya, mwanamke na mtoto wakila chakula

Mwanamke alimtengenezea Eliya mkate. Kisha unga na mafuta yake viliongezeka! Kulikuwa na chakula cha kutosha kwa ajili ya Eliya na familia ya mwanamke kwa siku nyingi.

1 Wafalme 17:15–16

Picha
mwanamke akiomboleza kifo cha mtoto

Siku moja mtoto wa yule mwanamke aliugua na kufa. Mwanamke alimwuliza Eliya kwa nini Bwana angeruhusu hili litokee kwake.

1 Wafalme 17:17–20

Picha
mwanamke akimkumbatia mtoto

Eliya alikuwa na ukuhani. Alimbariki mtoto wa mwanamke na kumuomba Bwana kumruhusu mtoto arejee tena kwenye uhai. Mtoto alipumua tena na mwanamke alijua kwamba Eliya alikuwa nabii wa Bwana.

1 Wafalme 17:21–24

Chapisha