Scripture Stories
Yona Nabii


“Yona Nabii,” Hadithi za Agano la Kale (2021)

“Yona Nabii,” Hadithi za Agano la Kale

Yona 1–4

Yona Nabii

Kujifunza kutumaini rehema za Bwana

Picha
Yona akionekana mwenye huzuni

Yona alikuwa nabii. Bwana alimwambia awaonye watu wa Ninawi kwamba mji wao ungeangamizwa ikiwa hawatatubu.

Yona 1:1–2

Picha
Yona akipanda merikebu

Lakini watu wa Ninawi walikuwa maadui kwa Waisraeli. Yona hakutaka kuwahubiria. Hivyo alipanda ndani ya merikebu ili kwenda mbali na Ninawi.

Yona 1:3

Picha
merikebu kwenye bahari yenye tufani

Wakati Yona akiwa ndani ya merikebu, tufani kubwa ilikuja. Watu kwenye merikebu walihofia maisha yao. Walimsihi Yona amuombe Bwana ili awaokoe.

Yona 1:4–6

Picha
Yona akizungumza na mabaharia

Yona alijua kwamba Bwana alituma tufani kwa sababu alikuwa akikimbia kile Bwana alichomuomba kufanya. Yona alitaka kuwaokoa watu waliokuwa ndani ya merikebu. Alisema ikiwa wangemtupa baharini, tufani ingetulia.

Yona 1:12

Picha
mabaharia wakimtupa Yona nje ya merikebu

Mabaharia hawakutaka kumtupa Yona baharini. Walijaribu kuipeleka merikebu ufukoni, lakini tufani ilikuwa kali. Hatimaye, walimtupa Yona baharini.

Yona 1:13–15

Picha
samaki mkubwa akimmeza Yona

Tufani ilikoma. Lakini hapo Yona alikuwa amemezwa na samaki mkubwa.

Yona 1:15, 17

Picha
Yona kwenye ufuko wa bahari

Yona alikuwa ndani ya tumbo la samaki kwa siku tatu mchana na usiku. Wakati huo, Yona aliomba na kutubu. Alitaka kufanya kile kilicho sahihi na kumsikiliza Bwana. Bwana alisikia maombi ya Yona na akamfanya samaki amtapike Yona kwenye nchi kavu.

Yona 1:17; 2:1–10

Picha
Yona akiwahubiria watu

Bwana akamwambia tena Yona kuwahubiria watu wa Ninawi. Safari hii Yona alitii. Alienda Ninawi na kuwaambia watu watubu la sivyo Bwana angeangamiza mji wao. Mfalme na watu wake walitubu. Bwana aliwasamehe na hakuiangamiza Ninawi.

Yona 3

Picha
Yona akionekana mtu aliyekasirika

Lakini Yona alivunjika moyo kwamba watu hawajaangamizwa. Hakudhani kwamba walistahili kusamehewa.

Yona 4:1–2

Picha
Yona akitazama mti ulio kufa

Ili kumfundisha Yona somo, Bwana aliotesha mti ili kumpa Yona kivuli kutokana na jua. Kisha mti ukafa, na Yona akahisi vibaya kwa ule mti.

Yona 4:5–9

Picha
Yona akifundisha kundi la watu

Bwana alikuwa akimfundisha Yona somo kuhusu watoto Wake. Yona alijifunza kwamba alipaswa kuwa na huzuni wakati watu hawataki kutubu na kwamba anapaswa kuwa na furaha pale wanapotubu.

Yona 4:10–11

Chapisha