Scripture Stories
Danieli na Rafiki Zake


“Danieli na Rafiki Zake,” Hadithi za Agano la Kale (2022)

“Danieli na Rafiki Zake,” Hadithi za Agano la Kale

Danieli 1

Danieli na Rafiki Zake

Kukataa kula chakula cha mfalme

Picha
vijana wakichukuliwa na askari

Ufalme wa Babeli uliiteka Yerusalemu. Waliwachukua baadhi ya vijana werevu na wenye nguvu kutoka kwa familia zao huko Yerusalemu na kuwaleta Babeli ili wamtumikie mfalme.

Danieli 1:1–4

Picha
vijana ndani ya jumba la mfalme

Danieli na rafiki zake walikuwa kati ya vijana hawa. Walichaguliwa kutumikia ndani ya jumba la mfalme na kuwa watu wake wenye hekima.

Danieli 1:4–6

Picha
chakula na divai

Mfalme aliwapa Danieli na rafiki zake chakula na divai. Lakini wasingekula chakula cha mfalme au kunywa divai. Ilikuwa kinyume na amri za Mungu.

Danieli 1:5–8

Picha
vijana wakila chakula

Hii ilimfanya mtumishi wa mfalme ahofie maisha yake. Aliwahudumia Danieli na rafiki zake, na alidhani ikiwa wangekataa chakula cha mfalme, wangekuwa dhaifu kuliko vijana wengine. Ndipo mfalme angekuwa na hasira na kumuua mtumishi yule.

Danieli 1:9–10

Picha
Danieli akizungumza na mtumishi

Lakini Danieli alimtumaini Bwana na alitaka kutii amri zake. Danieli alimuomba mtumishi awapatie maji na nafaka kwa siku 10 na kisha kulinganisha afya yao na afya ya vijana wengine. Mtumishi alikubali.

Danieli 1:11–14

Picha
Danieli na marafiki wakisoma

Baada ya siku 10, Danieli na rafiki zake walikuwa wenye afya kuliko vijana wengine wote. Danieli na rafiki zake walifuata amri za Mungu na Mungu aliwafanya wawe watu wenye hekima kuliko wengine wote kwenye jumba la mfalme.

Danieli 1:15–20

Chapisha