Scripture Stories
Nehemia


“Nehemia,” Hadithi za Agano la Kale (2022)

“Nehemia,” Hadithi za Agano la Kale

Nehemia 1–246

Nehemia

Kujenga upya ukuta huko Yerusalemu

Picha
Nehemia, mfalme anaangalia

Nehemia alikuwa Myahudi aliyeishi huko Uajemi. Alikuwa mtumishi aliyeaminiwa na mfalme. Siku moja Nehemia alisikia kwamba Wayahudi huko Yerusalemu walikuwa wakiteseka. Kuta zilizolinda Yerusalemu zilikuwa zimebomolewa na katu hazijajengwa tena. Yerusalemu ilikuwa hatarini. Nehemia alifunga na kuomba msaada kwa Bwana.

Nehemia 1

Picha
Mfalme akiongea na Nehemia kuhusu ukuta

Mfalme alimwuliza Nehemia kwa nini alikuwa na huzuni sana. Alimwambia mfalme kuhusu hatari katika Yerusalemu. Mfalme alisema kwamba angeweza kusaidia. Nehemia aliomba kwenda Yerusalemu na kuujenga upya ule ukuta. Mfalme akamfanya Nehemia kuwa kiongozi na akampatia vifaa alivyohitaji.

Nehemia 2:2–8

Picha
Nehemia akijenga ukuta, maadui wanaangalia

Nehemia na Wayahudi walianza kujenga upya kuta. Lakini maadui waliwafanyia dhihaka na kujaribu kuwazuia.

Nehemia 2:17–20

Picha
watu wakimfanyia mzaha Nehemia

Maadui walijaribu kumtega Nehemia ili aondoke mjini. Lakini Nehemia hakuondoka. Alimtumaini Bwana. Yeye alikuwa anafanya Kazi Kuu.

Nehemia 6:2-4

Picha
Nehemia akisimama juu ya ukuta uliomalizika

Nehemia aliwaambia watu wake wasiogope. Wakawaweka walinzi ili kuulinda. Wayahudi waliendelea kuujenga ukuta. Bwana aliwapa nguvu Wayahudi, nao wakaumaliza ukuta katika siku 52. Yerusalemu ilikuwa salama tena.

Nehemia 4:6–15; 6:5–9, 15–16

Chapisha