Scripture Stories
Pasaka


“Pasaka,” Hadithi za Agano la Kale (2022)

“Pasaka,” Hadithi za Agano la Kale

Kutoka 11–12; 14–15

Pasaka

Kulindwa na Bwana

Picha
Musa akisali

Farao hangewaacha Waisraeli kuwa huru, hivyo Bwana akamwambia Musa kwamba Yeye angeleta pigo moja la mwisho. Mtoto mzaliwa wa kwanza wa kila familia katika nchi ya Misri angekufa, hata mzaliwa wa kwanza wa wanyama wao.

Kutoka 11:1, 4–10

Picha
Musa akizungumza na watu

Bwana aliahidi kwamba kama Waisraeli wangefuata maelekezo Yake, pigo litapita juu yao na halitowadhuru.

Kutoka 12:3, 13, 23

Picha
Mwanaume akipaka rangi fremu ya mlango, watoto wakiangalia

Bwana aliwaambia kila familia ya Israeli kutoa dhabihu ya mwanakondoo dume aliye mkamilifu na kupaza damu yake juu ya fremu ya milango ya nyumba zao.

Kutoka 12:4–7

Picha
Familia wakila mlo wa usiku

Bwana aliwaambia Waisraeli kupika na kumla haraka yule mwanakondoo. Wakati wakila, yawapasa wawe wamevaa na tayari kuondoka na kuziacha nyumba zao. Kama Waisraeli wakifanya mambo haya, wazaliwa wao wa kwanza wangekuwa salama kutokana na pigo hilo.

Kutoka 12:8–11

Picha
Mwana wa Farao amekufa

Kama Bwana alivyoonya, pigo likaja. Wazaliwa wote wa kwanza katika Misri walikufa, ikijumuisha mwana mkubwa wa Farao. Lakini pigo likapita kando kwenye nyumba zenye damu kwenye fremu za mlango. Wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli wakaokolewa kwa sababu walimtii Bwana.

Kutoka 12:12–13, 29–30

Picha
Farao mwenye huzuni akimwambia Musa na Haruni waondoke

Farao alipoona mwanae mwenyewe alikuwa amekufa kwa sababu ya pigo hili, akawaambia Musa na Haruni wawachukue Waisraeli wote na waondoke Misri.

Kutoka 12:31–33

Picha
Farao mwenye hasira anatuma jeshi

Waisraeli wakaondoka, lakini Farao alikasirika. Alikusanya jeshi lake na magari ya kukokotwa na farasi na akawafukuzia Waisraeli.

Kutoka 12:37–41; 14:5–8

Picha
jeshi likiwafukuzia Waisraeli

Waisraeli wakapiga kambi kwenye Bahari ya Shamu. Punde Farao na jeshi lake likawafikia. Waisraeli walipowaona Wamisri wakiwajia, waliogopa. Lakini Musa aliwaambia Waisraeli kwamba Bwana angewalinda.

Kutoka 14:9–14

Picha
Musa akanyanyua fimbo, Bahari ya Shamu ikagawanyika.

Wamisri walivyokuwa wakikaribia, Bwana akamwambia Musa anyoshe juu fimbo yake. Musa akafanya, na Bwana akaigawanya bahari. Waisraeli wakavuka bahari kwenye nchi kavu. Wakawakimbia Farao na jeshi lake.

Kutoka 14:15–16, 21–22

Picha
Bahari ya Shamu inaliangukia jeshi la Wamisri

Jeshi la Wamisri liliwafukuzia Waisraeli. Baada ya Waisraeli wote kuvuka salama upande mwingine wa bahari, Bwana akaachilia maji yashuke chini. Jeshi la Wamisri likazama baharini.

Kutoka 14:23–30

Picha
Waisraeli wakicheza

Mwishowe Waisraeli wakawa huru. Wakaimba nyimbo, wakacheza, na wakamshukuru Bwana. Daima walikumbuka Pasaka kama wakati Bwana alipookoa maisha yao na kuwaongoza kutoka Misri.

Kutoka 14:31; 15:1–22

Chapisha