Scripture Stories
Eliya na Makuhani wa Baali


“Eliya na Makuhani wa Baali,” Hadithi za Agano la Kale (2022)

“Eliya na Makuhani wa Baali,” Hadithi za Agano la Kale

1 Wafalme 18

Eliya na Makuhani wa Baali

Nabii wa Bwana dhidi ya makuhani wa uwongo

Picha
sanamu ndogo ya Baali

Ufalme wa Israeli uliendelea kuteseka kwa kukosa maji. Mfalme Ahabu aliwaambia watu kumfuata mungu wa uwongo aliyeitwa Baali.

1 Wafalme 18:1–2, 17–18

Picha
Eliya akizungumza na Ahabu

Mungu alimtuma Eliya nabii kukutana na Ahabu. Eliya aliwaalika watu wote kwenye kilele cha mlima. Aliwaalika mfalme na makuhani wake kwenye shindano ili kuona ikiwa Bwana au Baali ndiye alikuwa Mungu wa kweli.

1 Wafalme 18:19–21

Picha
Eliya akizungumza na Makuhani wa Baali

Eliya alielezea shindano. Yeye na makuhani wangeweka sadaka ya ng’ombe juu ya madhabahu, lakini hawakutakiwa kuwasha moto wao wenyewe. Badala yake, makuhani wangeomba kwa Baali ili ashushe moto. Kisha Eliya angeomba kwa Bwana ili ashushe moto. Eliya alijua kwamba ni Mungu wa kweli pekee angeweza kushusha moto.

1 Wafalme 18:22–25

Picha
Eliya akizungumza na kundi la watu

Makuhani wa Baali waliomba kwa mungu wao kuanzia asubuhi mpaka mchana, lakini hakuna kilichotokea. Eliya aliwadhihaki na kusema mungu wao Baali atakuwa amelala.

1 Wafalme 18:26–27

Picha
makuhani wa Baali wakiomba juu ya madhabahu

Makuhani walishikwa na hasira, wakaruka juu ya madhabahu na kupiga kelele mpaka jioni. Walitumaini mungu wao angejibu, lakini bado hakukuwa na moto.

1 Wafalme 18:28–29

Picha
Eliya akiwa amepiga magoti

Kisha ikafika zamu ya Eliya. Yeye alimjengea Bwana madhabahu, akachimba mfereji kuzunguka madhabahu na kuandaa sadaka.

1 Wafalme 18:30–32

Picha
Eliya na watu wakijenga madhabahu

Eliya aliwaomba watu wajaze maji mapipa manne na kuyamwaga juu ya kuni za madhabahu yake mara tatu. Maji yalilowesha kuni na madhabahu. Yalijaza mfereji wote.

1 Wafalme 18:33–37

Picha
Eliya akiomba karibu na madhabahu

Eliya alimuomba Bwana aonyeshe nguvu za kweli za Mungu. Moto wa Bwana ulishuka chini na kuteketeza sadaka, kuni, mawe na maji. Watu walifahamu kwamba Mungu wa Eliya alikuwa Mungu wa kweli. Eliya aliomba kwamba ukame uweze kukoma, na Bwana alituma mvua.

1 Wafalme 18:38–41

Chapisha