Scripture Stories
Musa na Nyoka wa Shaba


“Musa na Nyoka wa Shaba,” Hadithi za Agano la Kale (2022)

“Musa na Nyoka wa Shaba,” Hadithi za Agano la Kale

Hesabu 21

Musa na Nyoka wa Shaba

Kujifunza kuwa na imani katika Bwana.

Picha
nyoka wakiwashambulia watu

Wakati Waisraeli walipokuwa wakisafiri nyikani mara nyingi walimsahau Bwana na kulalamika. Bwana aliwatuma nyoka ili kuwasaidia kumkumbuka Yeye. Nyoka waliwauma watu, wengi wa watu hao walikufa.

Hesabu 21:1–6

Picha
watu wakimwomba Musa

Kisha watu walitubu. Walimsihi Musa aombe kwa Bwana ili afanye nyoka wale watoweke. Bwana akuwaondoa wale nyoka. Lakini alitengeneza njia kwa ajili ya watu kuokolewa kama wangeumwa.

Hesabu 21:7.

Picha
Musa akiwa amemshika nyoka wa shaba

Bwana alimwambia Musa kutengeneza nyoka kutokana na shaba na kumning’iniza kwenye fimbo. Watu walipoumwa na nyoka na wakamwangalia yule nyoka wa shaba, Bwana aliwaokoa. Bwana aliwasaidia Waisraeli kuwa wanyenyekevu na kumtumaini Yeye.

Hesabu 21:8–9; 1 Nefi 17:41; Helamani 8:14–15

Chapisha