Scripture Stories
Yakobo na Esau


“Yakobo na Esau,” Hadithi za Agano la Kale (2022)

“Yakobo na Esau,” Hadithi za Agano la Kale

Mwanzo 25–27

Yakobo na Esau

Kaka wawili na haki moja ya mzaliwa wa kwanza

Picha
Esau na Yakobo wakifanya kazi

Isaka na Rebeka walikuwa na wavulana mapacha, Yakobo na Esau. Esau alikuwa mwindaji hodari. Yakobo aliishi maisha ya kawaida na alimfuata Bwana.

Mwanzo 25:20–28

Picha
Esau na Isaka

Esau alizaliwa kwanza. Mzaliwa wa kwanza kwa kawaida alipokea baraka ya haki ya mzaliwa wa kwanza kutoka kwa baba yake. Haki ya mzaliwa wa kwanza ilimaanisha angeongoza familia na kuwa na ardhi kubwa na wanyama wengi ili kusaidia kuitunza familia. Lakini Esau alijijali zaidi yeye mwenyewe kuliko familia yake, na hakuwatii wazazi wake na Bwana.

Mwanzo 25:25, 32; 26:34–35

Picha
Yakobo akimpa Esau chakula

Siku moja Esau alirudi kutoka mawindoni. Alikuwa na njaa kali na akamwomba Yakobo ampe chakula. Bwana alitaka Yakobo apate baraka ya haki ya mzaliwa wa kwanza kwa sababu Esau hakuistahili. Yakobo alimwomba Esau wabadilishane haki ya mzaliwa wa kwanza kwa chakula. Esau alikubali na akampa Yakobo haki yake ya mzaliwa wa kwanza.

Mwanzo 25:23, 29–34; Waebrania 11:20

Picha
Rebeka na Isaka

Rebeka na Isaka walitaka kile kilicho bora kwa ajili ya watoto wao. Walikuwa na huzuni kwamba Esau aliendelea kufanya mambo aliyotaka yeye na si ambayo Bwana alitaka.

Mwanzo 26:34–35

Picha
Isaka akizungumza na Esau

Isaka alikuwa mzee na kipofu. Kabla hajafa, alimuomba Esau kuwinda na kumpikia mnyama ili ale na afurahi.

Mwanzo 27:1–4

Picha
Rebeka akimwangalia Esau

Rebeka alijua kwamba ilikuwa ni muda kwa Isaka kutoa baraka ya haki ya mzaliwa wa kwanza.

Mwanzo 27:5

Picha
Rebeka akizungumza na Yakobo

Rebeka alimwomba Yakobo atafute wanyama wawili ili aweze kupika chakula kabla ya Esau kurejea. Kisha Yakobo angepokea baraka.

Mwanzo 27:6–17

Picha
Isaka akimpa Yakobo baraka

Yakobo alivalia kama Esau na kuleta chakula kwa baba yake. Isaka alimpa Yakobo baraka ya haki ya mzaliwa wa kwanza. Wakati Esau aliporejea, alimkasirikia sana Yakobo. Lakini haki ya mzaliwa wa kwanza ilimwendea Yakobo kwa sababu alitii amri za Bwana na Esau hakutii.

Mwanzo 27:18–29

Chapisha