Scripture Stories
Mtoto Musa


“Mtoto Musa,” Hadithi za Agano la Kale (2022)

“Mtoto Musa,” Hadithi za Agano la Kale

Kutoka 1–2

Mtoto Musa

Kumlinda kiongozi wa baadaye wa Waisraeli

Picha
Farao akiangalia ufalme

Familia ya Yakobo ilikuwa ya watu mashuhuri huko Misri. Waliitwa Waisraeli. Farao, mfalme wa Misri, aliogopa kwamba siku moja kungekuwa na Waisraeli wengi sana na kwamba wangetawala Misri, hivyo aliwafanya Waisraeli kuwa watumwa wake.

Kutoka 1:7–14

Picha
askari wakitazama ng’ambo ya mto

Farao kisha aliamuru kwamba watoto wachanga wote wa kiume wa Waisraeli walipaswa kuuawa. Familia za Waisraeli zilikuwa na hofu sana.

Kutoka 1:15–22

Picha
Yokebedi, Miriam na mtoto Musa ndani ya mto

Mama Muisraeli aliyeitwa Yokebedi alifikiria njia ya kumwokoa mwana wake mchanga. Alimuweka mtoto wake ndani ya kikapu na kukificha kikapu hicho ndani ya majani marefu pembezoni mwa Mto Nile. Dada wa mtoto, Miriam, alisimama mbali ili kuhakikisha usalama wa mtoto.

Kutoka 2:1–4

Picha
Binti wa Farao akiwa amembeba mtoto Musa

Wakati akioga mtoni, binti wa Farao aligundua kikapu. Alimwona mtoto Muisraeli asiye na usaidizi akilia na alitaka kumtunza kama mtoto wake mwenyewe. Miriam alikuja kwa binti wa Farao na aliomba ikiwa angeweza kumleta mwanamke Muisraeli ili amtunze mtoto.

Kutoka 2:5–6

Picha
Binti wa Farao, Yokebedi, Miriam na mtoto Musa

Miriam alimleta mama yake, Yokebedi, kwa binti wa Farao. Binti wa Farao alikubali kumlipa Yokebedi ili amtunze mtoto.

Kutoka 2:8–9

Picha
Binti wa Farao, Yokebedi na Musa

Mtoto Muisraeli alikua. Binti wa Farao alimkuza kama mwana wake mwenyewe. Alimwita jina lake Musa.

Kutoka 2:10

Chapisha