Scripture Stories
Kuhusu Agano la Kale


“Kuhusu Agano la Kale,” Hadithi za Agano la Kale (2022)

“Kuhusu Agano la Kale,” Hadithi za Agano la Kale

Kuhusu Agano la Kale

Ahadi za zamani za Baba wa Mbinguni kwa watoto Wake

Picha
Kielelezo cha maisha kabla ya kuja duniani

Sehemu ya kwanza ya Biblia Takatifu ni Agano la Kale. Maandiko haya yaliandikwa muda mrefu uliopita, hata kabla Yesu Kristo hajazaliwa. Yana hadithi ambazo zinatusaidia kuwa na imani kwake Yeye. Yanatufundisha kwamba kila mtu hapa duniani ni sehemu ya familia ya Baba wa Mbinguni na kwamba Yeye anawapenda watoto Wake.

Kumbukumbu la Torati 7:7–9; Isaya 45:10–12

Picha
Adamu na Hawa katika Bustani

Katika Agano la Kale, Yesu Kristo anaitwa Yehova na Bwana. Yeye anafuata maelekezo ya Baba wa Mbinguni. Tangu wakati wa Adamu na Hawa, Baba wa Mbinguni amekuwa akimtuma Bwana Yesu Kristo kuongea na manabii Wake. Baba wa Mbinguni humtuma Roho Mtakatifu ili kutusaidia sisi tujue kuwa maneno ya nabii ni ya kweli.

Kutoka 6:2–3; 2 Mambo ya Nyakati 20:20; Amosi 3:7; 2 Petro 1:21; Musa 2:1

Picha
Uzao wa Adamu

Bwana aliwaahidi nabii Ibrahimu na mke wake Sara kwamba familia yao ingekua na kuubariki ulimwengu wote. Mjukuu wao Yakobo alikuwa na familia kubwa ambayo ilikuja kuwa taifa. Waliitwa nyumba ya Israeli, au Waisraeli. Manabii waliwafundisha kutazamia wakati ambapo Yesu Kristo angekuja.

Mwanzo 15:5–6; 17:1–8; Kumbukumbu la Torati 18:15; Isaya 7:14

Picha
watu wakiangalia upinde wa mvua

Hadithi nyingi katika Agano la Kale zinaonyesha jinsi Bwana alivyotimiza ahadi Zake kwa Waisraeli.

Mwanzo 9:13–17; Yeremia 11:4–5; Waebrania 11:1–35

Picha
Musa akionyesha fimbo kwa watu

Wakati Waisraeli walipowasikiliza manabii na kushika amri, Bwana aliwasaidia. Walipokuwa siyo watiifu, Yeye hakuweza kuwasaidia.

Kumbukumbu la Torati 11:26–28; Ayubu 36:11–12

Picha
watoto wakisoma maandiko

Wewe ni sehemu ya familia ya Baba wa Mbinguni. Baba wa Mbinguni ni mkarimu, na Anakupenda. Yeye anao mpango kwa ajili yako. Kwa sababu ya Bwana Yesu Kristo, wewe unaweza kurudi kuishi na Baba wa Mbinguni tena. Kama tu Waisraeli walivyofundishwa, wewe nawe unaweza kuchagua kuwa na imani katika Bwana na kushika amri Zake.

Kutoka 15:2; Kumbukumbu la Torati 4:31; 5:10; Musa 1:39

Chapisha