Scripture Stories
Mfalme Yosia


“Mfalme Yosia,” Hadithi za Agano la Kale (2022)

“Mfalme Yosia,” Hadithi za Agano la Kale

2 Wafalme 22; 2 Mambo ya Nyakati 34–35

Mfalme Yosia

Kutafuta kutii amri za Bwana

Picha
mfalme kijana Yosia

Yosia alikuwa na umri wa miaka minane wakati alipofanywa kuwa mfalme wa Yuda. Alikuwa mfalme mwema aliyempenda Bwana. Alitaka kuwasaidia watu wake, Waisraeli, kumtii Bwana na kuacha kuabudu sanamu. Alipokuwa mkubwa, yeye na watu wake walianza kukarabati hekalu na kulirembesha tena.

2 Wafalme 22:1–2; 2 Mambo ya Nyakati 34:3–7

Picha
Hilkia anaokota hati ndefu za zamani katika magofu ya hekalu

Wakati watu wakifanya kazi katika hekalu, Hilkia kuhani mkuu akapata kitabu cha sheria, hati ndefu kama ya zamani ambayo ilikuwa na maandiko matakatifu.

2 Wafalme 22:3–9

Picha
akiwa mwenye huzuni mfalme Yosia anasikiliza kutoka kwenye kitabu cha sheria

Mtumishi anamsomea Yosia. Yosia alisikia yale maneno na alihuzunika kwa sababu watu wake hawakumtii Bwana. Akararua mavazi yake ili kuonyesha kuwa alihuzunika.

2 Wafalme 22:10–13, 19

Picha
Watumishi wa Yosia wakizungumza na Hulda

Alimwambia Hilkia amuulize Bwana alipaswa kufanya nini. Hilkia na watumishi wa mfalme walimtembelea Hulda. Alikuwa nabii mke, kiongozi mwaminifu aliyeongozwa na Mungu. Alisema Bwana alifurahishwa na Yosia kwa sababu alikuwa akiwasaidia watu kutii. Bwana aliahidi kwamba Mfalme Yosia angeishi katika amani.

2 Wafalme 22:12–20

Picha
Mfalme Yosia kwenye karamu ya Pasaka

Mfalme Yosia alitaka watu wake kushika ahadi zao kwa Bwana. Aliwaomba washerehekee Pasaka ili iwasaidie kukumbuka jinsi Bwana alivyoaachilia huru Waisraeli miaka mingi iliyopita huko Misri.

2 Mambo ya Nyakati 35:1–19

Chapisha