Scripture Stories
Musa juu ya Mlima Sinai


“Musa juu ya Mlima Sinai,” Hadithi la Agano la Kale (2022)

“Musa juu ya Mlima Sinai,” Hadithi za Agano la Kale

Kutoka 19–2024; 31–34; Kumbukumbu la Torati 4–7

Musa juu ya Mlima Sinai

Kuwasaidia watu kumkumbuka Bwana

Picha
Mlima Sinai

Musa na Waisraeli walisafiri kupitia nyikani. Wakafika kwenye mlima ulioitwa Mlima Sinai.

Kutoka 19:1

Picha
Musa akisali

Musa alipanda mlimani ili kuongea na Bwana. Bwana alimwambia Musa kwamba alitaka kuongea na Waisraeli uso kwa uso.

Kutoka 19:3, 9–11

Picha
Mawingu yakiuzunguka mlima

Waisraeli walifika hadi chini ya Mlima Sinai, na Bwana akasababisha wingu la moshi kuuzunguka ule mlima. Bwana alikuwa katika lile wingu. Alisema na Waisraeli na kuwapa amri. Mlima ulitikisika alipokuwa akiongea.

Kutoka 19:16–19; 20:1–17; Kumbukumbu la Torati 4:12–13, 33; 5:4–5

Picha
Waisraeli wakiogopa

Waisraeli waliogopa. Walimwomba Musa aongee na Bwana ili Musa aweze kuongea na wao kile ambacho Bwana alikitaka.

Kutoka 20:18–19

Picha
Wazee wa Waisraeli juu ya mlima

Musa alimchukua Haruni na wazee 70 wa Waisraeli kwenda juu ya mlima ili kupokea mafundisho zaidi ya Bwana. Bwana aliwatokea.

Kutoka 24:1, 9–11

Picha
Bwana akiandika juu ya mbao kwa ajili ya Musa

Kisha Bwana alimwambia Musa kuwaacha wale wazee hapo na kwenda juu zaidi ya mlima. Musa alitii. Bwana alitumia kidole Chake kuandika sheria Yake na amri juu ya zile mbao za mawe. Kwa siku 40, Bwana alimfundisha Musa mambo mengi.

Kutoka 24:12–18; 31:18

Picha
Waisraeli wakitengeneza ndama wa dhahabu

Wakati Musa akiwa juu ya Mlima Sinai, watu wa Israeli walichoka kumsubiri. Walimwambia Haruni awatengeneze sanamu waiabudu kama walivyokuwa nayo kule Misri. Haruni akakusanya dhahabu yao yote na akatengeneza sanamu ya ndama.

Kutoka 32:1–4

Picha
Waisraeli wakiabudu ndama wa dhahabu

Waisraeli walimwabudu yule ndama wa dhahabu na wakatoa dhabihu. Walisema ndama wa dhahabu, sio Bwana, aliwatoa utumwani kutoka Misri.

Kutoka 32:4–6, 21–24

Picha
Musa akishuka chini kutoka mlimani

Bwana alijua Waisraeli walikuwa wakiabudu sanamu na wanamsahau Yeye. Akamwamuru Musa kurudi na awaambie watu watubu.

Kutoka 32:7–10

Picha
Musa akiongea na Waisraeli, ndama wa dhahabu anaangamizwa

Musa aliposhuka chini kutoka Mlima Sinai na kuona Waisraeli wakiabudu ndama wa dhahabu. Alifadhaika sana. Watu hawakuwa tayari kutii sheria na amri ambazo Bwana aliziandika. Musa alizivunja zile mbao za mawe na akamwangamiza yule ndama wa dhahabu. Aliwasaidia Waisraeli kutubu na kumkumbuka Mungu wao wa kweli.

Kutoka 32:15–20, 25–29

Picha
Musa akisali

Musa alimwomba Bwana awasamehe Waisraeli na afanye ahadi nao tena. Musa aliahidi kuwaongoza na kuwafundisha.

Kutoka 32:30–34

Picha
Musa akiwa na mbao za Amri Kumi.

Bwana aliwaambia Musa atengeneze mbao za mawe mpya na aende tena kwenye Mlima Sinai. Bwana akafanya ahadi mpya na Waisraeli na akawapa Amri Zake Kumi.

Kutoka 20:2–17; 34:1–17, 28; Kumbukumbu la Torati 6:24–25; 7:12–13

Chapisha