Agano la Kale 2022
Desemba 27–Januari 2. Musa 1; Ibrahimu 3: “Hii Ndiyo Kazi Yangu na Utukufu Wangu”


“Desemba 27–Januari 2. Musa 1; Ibrahimu 3: ‘Hii Ndiyo Kazi Yangu na Utukufu Wangu,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Bainafsi na Familia: Agano la Kale 2022 (2021)

“Desemba 27–Januari 2. Musa 1; Ibrahimu 3,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2022

Picha
picha ya nyota zikiwa angani

Desemba 27–Januari 2

Musa 1; Ibrahimu 3

“Hii Ndiyo Kazi Yangu na Utukufu Wangu”

Unaposoma kile Mungu alichosema kwa Musa na Ibrahimu, tafakari kile ambacho Yeye anaweza kuwa anasema kwako pia.

Andika Misukumo Yako

Biblia inaanza kwa maneno “hapo mwanzo Mungu aliumba mbingu na nchi” (Mwanzo 1:1). Lakini kulikuwa na nini kabla ya “mwanzo” huu? Na kwa nini Mungu aliumba vyote hivi? Kupitia Nabii Joseph Smith, Bwana ametoa mwanga juu ya maswali haya.

Kwa mfano, Yeye ametupatia kumbukumbu ya ono ambamo Ibrahimu aliona maisha yetu kama roho “kabla ya ulimwengu kuwako” (ona Ibrahimu 3:22–28). Bwana pia ametupatia tafsiri yenye mwongozo wa kiungu au masahihisho ya milango sita ya kwanza ya kitabu cha Mwanzo, kinachoitwa kitabu cha Musa—ambacho hakianzi na “hapo mwanzo.” Badala yake, kinaanza na uzoefu ambao Musa aliupata wenye kutoa mazingira ya hadithi maarufu ya Uumbaji. Kwa pamoja, haya maandiko ya siku za mwisho ni mahali pazuri pa kuanzia ili kujifunza juu ya Agano la Kale kwa sababu yanajibu baadhi ya maswali ya msingi ambayo yanaweza kujenga usomaji wetu: Mungu ni Nani? Sisi ni nani? Je, Kazi ya mungu ni ipi, na nafasi yetu ni ipi katika kazi hiyo? Milango ya ufunguzi ya kitabu cha Mwanzo inaweza kuonekana kama majibu ya Bwana kwa ombi la Musa: “Umrehemu mtumishi wako, Ee Mungu, na uniambie juu ya dunia hii, na wakazi wake, na pia mbingu” (Musa 1:36).

Picha
Learn More image
Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

Musa 1

Kama mtoto wa Mungu, ninayo hatima ya kiungu.

Rais Dieter F. Uchtdorf alifundisha, “Sehemu kubwa ya mkanganyiko tunaouona katika maisha haya huja kutokana tu na kutoelewa sisi ni nani” (“The Reflection in the Water” [Church Educational System fireside for young adults, Nov. 1, 2009], ChurchofJesusChrist.org). Baba wa Mbinguni anajua hili, na Shetani vivyo hivyo. Ujumbe wa kwanza wa Mungu kwa Musa unajumuisha ukweli kwamba “wewe u mwanangu” na “nawe u mfano wa Mwanangu wa Pekee” (Musa 1:4, 6). Kinyume chake, Shetani alimwita Musa kama tu “mwana wa mtu” (Musa 1:12). Je, maisha na maamuzi yako yangekuwaje ya tofauti kama ungefikiria juu yako mwenyewe kama Shetani anavyotaka ujifikirie, kama “mwana [au binti] wa mtu”? Je, ni kwa jinsi gani kujua na kukumbuka kwamba wewe ni mtoto wa Mungu kunabariki maisha yako?

Je, ni mistari au vifungu gani vya maneno katika Musa 1 vinakupa ufahamu kuwa unastahiki wa kiungu?

Picha
Yesu Kristo miongoni mwa nyota

Kristo na Uumbaji, na Robert T. Barrett

Musa 1:12–26

Ninaweza kupinga ushawishi wa Shetani.

Kama Musa 1 inavyoonyesha kwa uwazi kabisa, matukio ya kiroho yenye nguvu hayatupi sisi kinga dhidi ya majaribu. Ukweli ni kwamba, moja ya mbinu za Shetani ni kutujaribu sisi tutilie mashaka uzoefu au kile tunachojifunza kutokana na uzoefu huo. Unaposoma kuhusu majibu ya Musa kwa Shetani katika mistari ya 12–26, unajifunza nini ambacho kinaweza kukusaidia kubaki mkweli kwa ushuhuda ambao umeupokea? Je, ni kitu gani kinakusaidia kupinga majaribu mengine ya Shetani? (ona, kwa mfano, mistari ya 15 na 18).

Kulingana na kile unachojifunza, unaweza kutengeneza mpango kwa ajili ya kushinda majaribu. Kwa mfano, mngeweza kumalizia maelezo haya “Wakati ninapojaribiwa , nita .”

Ona pia Mathayo 4:1–11; Helamani 5:12; Gary E. Stevenson, “Usinidanganye,” Liahona, Nov. 2019, 93–96; “I Am a Son of God” (video), ChurchofJesusChrist.org.

Musa 1:27–39; Ibrahimu 3

Kazi ya Mungu na utukufu Wake ni kunisaidia mimi nipate uzima wa milele.

Baada ya kuona ono la uumbaji wa Mungu, Musa alifanya ombi kwa Bwana: “Niambie … kwa nini mambo haya yako hivi” (Musa 1:30). Je, ni kitu gani kinakuvutia kuhusu majibu ya Bwana katika Musa 1: 31-39?

Ibrahimu pia alipata uzoefu wa kupokea ono, lililoandikwa katika Abraham 3. Je unapata nini katika mistari ya 22–26 ambacho kingeweza kusaidia kujibu ombi la Musa?

Zingatia kuorodhesha kweli zingine ambazo Musa na Ibrahimu walijifunza katika maono yao: kweli kuhusu Mungu, kuhusu wao wenyewe, na kuhusu madhumuni ya uumbaji wa Mungu. Ni kwa jinsi gani kweli hizi zinaathiri jinsi wewe mwenyewe unavyojiona na ulimwengu unaokuzunguka?

Ona pia Dieter F. Uchtdorf, “You Matter to Him,” Liahona, Nov. 2011, 19–22; Gospel Topics, “Premortality,” topics.ChurchofJesusChrist.org.

Ibrahimu 3:22–23

Je, kuna wengine tofauti na Ibrahimu “waliochaguliwa kabla [wao] hawajazaliwa”?

Katika ulimwengu wa roho wa maisha kabla ya kuja duniani, Mungu aliteuwa roho fulani kutimiza misheni maalumu wakati wakiwa katika maisha ya mwili. Hii inaitwa kutawazwa kabla. … Mafundisho ya kutawazwa kabla yanatumika kwa waumini wote wa Kanisa, siyo tu kwa Mwokozi na manabii Wake” (Gospel Topics, “Foreordination,” topics.ChurchofJesusChrist.org).

Je, ni kwa jinsi gani tulipata vitabu vya Musa na Ibrahimu?

Kitabu cha Musa ni sehemu ya kwanza ya tafsiri ya Joseph Smith ya Biblia kwa mwongozo wa kiungu. Kitabu cha Ibrahimu kilifunuliwa kwa Joseph Smith wakati wa kazi yake na papiri za Kimisri. Vitabu hivi, vinapatikana leo katika Lulu ya Thamani Kuu, vinatoa taarifa nyingi kuhusu Musa, Ibrahimu, na manabii wengine ambayo haipatikani katika Agano la Kale. Ili kujifunza zaidi kuhusu jinsi gani tulipata vitabu hivi, ona “Joseph Smith Translation of the Bible” (Church History Topics, ChurchofJesusChrist.org/study/history/topics) na “Translation and Historicity of the Book of Abraham” (Gospel Topics, topics.ChurchofJesusChrist.org).

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko Kama familia na Jioni ya Nyumbani

Musa 1:2-6; Ibrahimu 3:11- 12.Ungeweza kuwaalika wana familia kutafuta vifungu vya maneno katika wimbo “I Am a Child of God” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 2–3) ambavyo vinahusiana na ukweli unaofundishwa katika maandiko haya.

Musa 1:4, 30–39.Je, familia yako ingefurahia kuangalia baadhi ya “kazi za mikono ya [Mungu]”? (mstari wa 4). Pengine mngeweza kusoma mistari hii kwenye bustani au chini ya nyota usiku. Kisha mngeweza kuongelea kuhusu kwa nini Mungu aliumba ulimwengu na kuhusu jinsi sisi tulivyoshiriki katika hiyo “kazi Yake na utukufu [Wake]” (mstari wa 39).

Musa 1:18.Je, ni ushauri gani tunaweza kuushiriki ili kusaidiana “kuhukumu kati ya” Mungu na Shetani? (Ona pia Moroni 7:12–18; Mafundisho na Maagano 50:23–24.)

Ibrahimu 3:24–26.Ungeweza kuwapa washiriki wa familia kazi ya kufurahisha lakini pia yenye changamoto ambayo inawaruhusu wao kuthibitisha kuwa wanaweza kufuata maelekezo, kama vile kukunja karatasi mfano wa ndege au kufuata maelezo ya upishi Je, ni kwa jinsi gani shughuli hii ni sawa na dhumuni la maisha yetu duniani kama inavyoelezewa katika mistari hii?

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “I Am a Child of God,” Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 2–3.

Kuboresha Kujifunza Binafsi

Tafuta ukweli wa Injili. Katika maandiko, wakati mwingine kweli za injili zinaelezwa moja kwa moja; wakati mwingine zinatolewa kupitia mfano au hadithi. Jiulize, “Ni ukweli gani wa milele unafundishwa katika mistari hii?”

Picha
Musa anamwamuru Shetani kuondoka

Musa Anamshinda Shetani na Joseph Brickey

Chapisha