Agano la Kale 2022
Februari 21–27. Mwanzo 24–27: Agano Limefanywa Upya


“Februari 21–27. Mwanzo 24–27: Agano Limefanywa Upya,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano la Kale 2022 (2021)

“Februari 21–27. Mwanzo 24–27,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2022

Picha
Rebeka

Kielelezo cha Rebeka, na Dilleen Marsh

Februari 21–27

Mwanzo 24–27

Agano Limefanywa Upya

Unaposoma Mwanzo 24–27, sali kujua jinsi unavyoweza kuwatia moyo washiriki wa darasa kuwa na uzoefu wao wenyewe wa kujifunza kutoka kwenye maandiko.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Kuwatia moyo washiriki wa darasa kushiriki utambuzi wao kutoka Mwanzo 24–27, ungeweza kuwaomba wachague kifungu mahususi ambacho kinawatia moyo na wakiandike kwenye kipande cha karatasi. Kusanya karatasi, na chagua baadhi za kusoma na jadilini kama darasa.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Mwanzo 24

Ndoa ya Agano ni muhimu kwa mpango wa milele wa Mungu.

  • Umuhimu ambao Ibrahimu aliuweka kwenye kumtafuta mke kwa ajili ya Isaka unatoa fursa kujadili umuhimu wa ndoa ya agano katika mpango wa Mungu kwa ajili yetu. Kuanza majadiliano, washiriki wa darasa wangeweza kupitia kwa haraka mwanzo 24 na kushiriki vitu Bwana alivyofanya kusaidia kuwaleta Isaka na Rebeka pamoja katika ndoa. Kwa nini ndoa ni muhimu kwa Bwana? Kuwasaidia washiriki wa darasa kujadili swali hili, ungeweza kushiriki pamoja nao kauli ya Mzee D. Todd Christofferson katika “Nyenzo za Ziada.” Jinsi gani tunaweza kusaidia kuhakikisha kwamba malengo ya Mungu kwa ajili ya ndoa yametimizwa?

  • Waulize washiriki wa darasa ni sifa gani wameziona kwa mwenza, wazazi, au wenza wengine waliooana ambayo imechangia kwenye ndoa yenye uaminifu, ya furaha. Maelezo katika Mwanzo 24 yanaonesha sifa ambazo zinaweza kumsaidia mtu kutengeneza furaha katika ndoa—na katika vipengele vingine vya maisha. Kwa mfano, katika mstari wa 12 tunajifunza kuhusu kuongozwa na sala, na katika mstari wa 19 tunajifunza kuhusu kutoa juhudi za ziada katika huduma. Kanuni gani zingine zinaweza kupatikana katika sura hizi? Washiriki wa darasa wanaweza pia kuangalia kwenye “Familia: Tangazo kwa Ulimwengu.” (ChurchofJesusChrist.org).

Mwanzo 25:29–34

Tunaweza kuchagua kati ya kukidhi haja haraka na vitu vya thamani kubwa.

  • Jinsi gani unaweza kuwasaidia washiriki wa darasa kupata mafunzo binafsi kutokana na uzoefu wa Yakobo na Esau? Wazo moja ni kuwaomba kutengeneza orodha mbili ubaoni—moja ya baraka za milele Mungu anazotaka kutupatia na vitu vingine vya kiulimwengu ambavyo vinatuvuta kutoka kwenye baraka hizo. Kisha washiriki wa Darasa wangeweza kusoma Mwanzo 25:29–34, wakibadilisha “urithi” kwa kitu fulani kutoka kwenye orodha ya kwanza na “chakula cha dengu” na kitu fulani kutoka kwenye orodha ya pili. Jinsi gani adui anajaribu kutushawishi kubadilisha baraka za Mungu kwa vitu ambavyo havina thamani? Fikiria kuwaomba washiriki wa darasa kupeana ushauri juu ya jinsi ya kulenga kwa Mwokozi na baraka za milele Anazotupatia.

Mwanzo 26:18–25, 32–33

Yesu Kristo ni chemchemi ya maji ya uzima.

  • Mwanzo 26 inataja mara kadhaa kwamba Isaka na watu wa nyumba yake walitakiwa kuchimba visima kupata maji, na hii mara nyingi ilihitaji juhudi kubwa. Ukweli huu ungeweza kukusaidia kuwafundisha washiriki wa darasa kuhusu juhudi zilizohitajika kuleta “maji ya uhai” ya Mwokozi ndani ya maisha yetu (ona Yohana 4:10). Pengine ungeweza kueleza hili kwa mchoro ubaoni wa chanzo cha maji kilichofunikwa kwa uchafu mwingi. Washiriki wa darasa wangeweza kufanya zamu kupangusa kiasi cha uchafu wakati wanapoelezea jinsi wanavyoweza kupata maji ya uzima ya Mwokozi. Watie moyo kutumia Guide to the Scriptures kupata mistari ambayo ina uhusiano na vitu wanavyoshiriki.

    Picha
    kisima cha kale

    Kisima katika Beer‑sheba ya kale, ambapo Ibrahimu na Isaka walichimba visima.

Picha
ikoni ya nyenzo za ziada

Nyenzo za Ziada

Ndoa na familia ni uumbaji wa Mungu.

Mzee D.Todd Christofferson alitoa baadhi ya sababu kwa nini ndoa na familia ni muhimu sana kwa mpango wa Mungu:

“Familia iliyojengwa juu ya ndoa ya mwanamume na mwanamke hutoa mazingira bora kwa mpango wa Mungu kushamiri—mazingira kwa ajili ya kuzaliwa kwa watoto, ambao huja katika usafi na wasio na hatia kutoka kwa Mungu, na mazingira kwa ajili ya kujifunza na kujitayarisha watakayohitaji kwa ajili ya ufanisi wa maisha ya duniani na uzima wa milele katika ulimwengu ujao. Kiasi fulani cha familia zilizojengwa katika ndoa kama hizo ni muhimu sana kwa jamii kustahimili na kustawi. …

“… Lakini madai yetu ya jukumu la ndoa na familia msingi wake si sayansi ya kijamii bali ni juu ya ukweli kuwa ni uumbaji wa Mungu. Ni Yeye hapo mwanzoni alimuumba Adamu na Hawa katika mfano wake, mwanamume na mwanamke, na akawaunganisha wao kama mume na mke kuwa ‘mwili mmoja’ na kuongezeka na kuijaza nchi. Kila mtu anabeba mfano wa kiungu, lakini ni katika muungano wa ndoa ya mwanamume na mwanamke kama kitu kimoja kwamba pengine tunaweza kupata maana kamili kabisa ya sisi kuumbwa katika mfano wa Mungu—mwanamume na mwanamke. … Ndoa kama hiyo … ni sawa na sehemu ya mpango wa furaha kama Anguko na Upatanisho” (“why Marriage, why Family,” Liahona, Mei 2015, 52).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Lenga ufundishaji wako kwenye mafundisho. Unapowaalika washiriki wa darasa kushiriki, hakikisha unaendelea kurejesha majadiliano kwenye mafundisho katika maandiko. Unaweza kufanya hivi kwa kuwaomba wanafunzi wasome vifungu vya maandiko darasani, kuuliza maswali kuhusu nini maandiko yanasema, na kuwaomba washiriki wa darasa kushiriki ushuhuda wao juu ya mafundisho yanayofundishwa.

Chapisha