Agano la Kale 2022
Machi 21–27. Kutoka 1–6: “Nimekumbuka Agano Langu”


“Machi 21–27. Kutoka 1–6: ‘Nimekumbuka Agano Langu,’” Njoo,Unifuate—Kwa ajili ya shule ya Jumapili: Agano la Kale 2022 (2021)

“Machi 21–27. Kutoka 16,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2022

Picha
Musa na kichaka kinachoungua

Musa na Kichaka Kinachoungua, na Harry Anderson

Machi 21–27

Kutoka 1–6

“Nimekumbuka Agano Langu”

Uliposoma Kutoka 1–6, fikiria kuhusu watu unaowafundisha. Kweli zipi katika sura hizi ni za kufaa kuwa za maana kwao? Ni kwa jinsi gani utaweza kuwasaidia kugundua kweli hizi?

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Wazo moja la kuwatia moyo washiriki wa darasa kushiriki kile wanachojifunza ni kuandika swali kama hili ubaoni: Unaposoma Kutoka 1–6, ulitambua nini ambacho hukutambua kabla? Waombe washiriki wa darasa kushiriki majibu yao.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Kutoka 1–2

Yesu Kristo ni Mkombozi wetu.

  • Hata kama Mwokozi hakutajwa kwa jina katika Kutoka 1–2, maelezo haya yanaweza kuwasaidia washiriki wa darasa kujenga imani katika misheni Yake kutukomboa kutoka utumwa. Washiriki wa darasa wangeweza kupata maneno au virai katika Kutoka 1–2 ambavyo vinaelezea taabu walizokumbana nazo wana wa Israeli. Jinsi gani maelezo haya yanafanana na utumwa wa kiroho au taabu zingine tunazokumbana nazo? Jinsi gani wana wa Israeli walitafuta kukombolewa, na jinsi gani Mungu aliwajibu? (Ona pia Kutoka 2:23–25; 3:7–8). Jinsi gani tunatumia nguvu za Mungu tunapohitaji kukombolewa? Jinsi gani Mungu anajibu maombi yetu kwa ajili ya msaada? Washiriki wa darasa wangeweza kutafuta utambuzi wa ziada katika ujumbe wa Rais Russell M. Nelson “Drawing the Power of Jesus into Our Lives” (Liahona, Mei 2017, 39–42).

    Picha
    Mtoto Musa ndani ya kikapu

    Musa katika Nyasi, © Providence Collection/licensed from goodsalt.com

Kutoka 3–4

Tunapofanya kazi ya Bwana, tunaweza kuwa na nguvu za Bwana.

  • Mhuhtasari wa wiki hii katika Njoo,Unifuate—Kwa Ajili ya watu binafsi na Familia unapendekeza kuchunguza Kutoka 3–4 kutafuta jinsi Bwana alivyojibu wasiwasi wa Musa kuhusu kazi ya kuwakomboa Wana wa Israeli kutoka utumwani. Kama washiriki wa darasa lako walifanya shughuli hii nyumbani, waombe kushiriki kile walichojifunza. Au mngeweza kufanya shughuli hii kama darasa. Hususani, washiriki wa darasa wangeweza kuchunguza Kutoka 3:11–18; 4:1–17, kutafuta wasiwasi wa Musa na majibu ya Bwana kwa kila moja wapo. Jinsi gani majibu ya bwana yangetusaidia wakati tuna wasiwasi kuhusu uwezo wetu wa kufanya kazi Yake?

Kutoka 3:5

Tunapaswa kuonesha heshima kuu kwa vitu na sehemu takatifu.

  • Jinsi gani unaweza kutumia mfano wa Musa kutia moyo majadiliano kuhusu jinsi tunavyopaswa kuvichukulia vitu vitakatifu? Kwa mfano, baada ya kusoma Kutoka 3:5 pamoja, ungeweza kuonesha vitu vitakatifu au picha za vitu vitakatifu (kama vile maandiko au mahekalu) na vitu vya kawaida au picha za vitu vya kawaida (kama vile vitabu vya kidunia au majengo ya kawaida). Washiriki wa darasa wangeweza kuzungumza kuhusu vitu vingine wanavyofikiri ni vitakatifu na kushiriki jinsi wanavyoonesha heshima kuu kwa vitu hivyo (ona pia Mambo ya Walawi 19:30; Mafundisho na Maagano 6:10–12). Kwa nini Mwokozi anatutaka kuvichukulia vitu vitakatifu kwa heshima kuu?

Kutoka 5:4–9, 20–23; 6:1–13

Azma za Bwana zitatimizwa katika muda wake mwenyewe.

  • Inaweza kukatisha tamaa wakati juhudi zetu za dhati kufanya mema hazionekani kufanya kazi—pengine rafiki hashawishiki kwenye juhudi zetu za kuhudumia au sala zetu za kwa ajili ya mtoto mtukutu zinaonekana hazijibiwi. Kujifunza kuhusu uzoefu kama huo aliokuwa nao Musa, washiriki wa darasa wangeweza kusoma Kutoka 5:4–9, 20–23. Bwana alimsaidia vipi Musa kushinda hisia zake za kukata tamaa? (Ona Kutoka 6:1–13). Washiriki wa darasa wangeweza kushiriki uzoefu wakati hawakuona matokeo ya mara moja kutokana na jitihada zao za kumtumikia Bwana. Uzoefu alioupata Musa katika sura hizi unatufundisha nini kuhusu jinsi tunavyoweza kuitikia katika hali kama hizo? (Ona pia “Nyenzo za Ziada.”)

Picha
ikoni ya nyenzo za ziada

Nyenzo za Ziada

Tunawatumikia wengine kwa ajili ya Bwana.

Rais Joy D. Jones alieleza jinsi yeye na mume wake walivyotumikia kwa uaminifu katika kazi waliyopangiwa ya kuhudumu lakini hawakuona mafanikio kutokana na juhudi zao. Wawili hao walitafakari na kusali kwa ajili ya mwongozo. Akisimulia jibu kwa sala zao, Rais Jones alisema:

“Tuligundua kwamba tulikuwa tukijaribu kwa uaminifu kuhudumia familia hii na kumtumikia askofu wetu, lakini tulipaswa kujiuliza kama kweli tulihudumu kwa sababu ya upendo kwa Bwana. Mfalme Benyamini aliweka wazi tofauti hii wakati aliposema, ‘Tazama, nawaambia kwamba kwa sababu niliwaambia kuwa nimewatumikia maishani mwangu, sitamani kujivuna, kwani nimekuwa tu katika utumishi wa Mungu’ [Mosia 2:16; msisitizo umeongezwa].

“Hivyo nani hasa Mfalme Benyamini alikuwa akimtumikia? Baba wa Mbinguni na Mwokozi. Kujua ni nani na kwa nini katika kutumikia wengine kunatusaidia kuelewa kwamba onyesho kuu la upendo ni kujitolea kwa Mungu” (“Kwa ajili Yake,” Liahona, Nov. 2018, 50).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Shiriki uzoefu wa kiroho. Njia moja ya kualika ushawishi wa Roho Mtakatifu katika darasa lako ni kuwatia moyo washiriki wa darasa kushiriki kile Roho Mtakatifu alichowafundisha walipokuwa wakijifunza maandiko wiki hii.

Chapisha