Agano la Kale 2022
Juni 20–26. 2 Samweli 5–7; 11–12; 1 Wafalme 3; 8; 11: “Ufalme Wako Utathibitishwa Milele”


“Juni 20–26. 2 Samweli 5–7; 11–12; 1 Wafalme 3; 8; 11: ‘Ufalme Wako Utathibitishwa Milele,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano la Kale 2022 (2021)

“Juni 20–26. 2 Samweli 5–7; 11–12; 1 Wafalme 3; 8; 11,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2022

Picha
Mfalme Daudi ameketi kwenye kiti cha enzi

Mfalme Daudi Akitawazwa, na Jerry Miles Harston

Juni 20–26

2 Samweli 5–7; 11–12; 1 Wafalme 3; 8; 11

“Ufalme Wako Utathibitishwa Milele”

Unapojifunza maandiko, kwa maombi tafuta kujua ni kanuni zipi zitakuwa za maana zaidi kwa washiriki wa darasa lako ili uweze kuzingatia kwenye mahitaji yao.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Ili kujua ni nini washiriki wa darasa waliona cha maana katika kusoma kwao maandiko, unaweza kuwauliza waandike kumbukumbu ya kifungu ambacho kiliwahamasisha kwenye karatasi na kisha kuweka karatasi hiyo kwenye chombo. Kisha washiriki wa darasa wangeweza kuchagua karatasi kutoka kwenye chombo hicho, na darasa linaweza kusoma na kujadili mafungu hayo ya maneno.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

2 Samweli 6:1–8

Lazima tufanye kazi ya Mungu katika njia Yake.

  • Unaweza kuwaomba washiriki wa darasa kusoma 2 Samweli 6:1–8 na fikiria ni maonyo gani historia hii inayo kwetu sisi leo. Maelezo ya Brigham Young katika “Nyenzo za Ziada” yanaweza kusaidia. Je, ni njia zipi tunaweza kujaribu kufanya kazi ya Mungu kwa njia nyingine tofauti na vile alivyoelekeza? Kwa nini hii ni hatari? Labda washiriki wa darasa wangeweza kushiriki uzoefu ambao kwa huo walijifunza kuamini maelekezo ambayo Bwana hutoa kwa ajili ya kukamilisha kazi Yake.

2 Samweli 11

Tunapaswa kila mara kujilinda dhidi ya dhambi.

  • Kujifunza kutokana na janga la chaguzi mbaya za Daudi lililoandikwa katika 2 Samweli 11 inaweza kutusaidia kuepuka makosa kama hayo. Labda darasa lingeweza kusoma pamoja 2 Samweli 11:1–17 na kutambua uchaguzi ambao Daudi alifanya ambao ulimsababishia yeye kutenda dhambi. Je, Daudi angefanya nini tofauti? Unaweza pia kuwaomba washiriki wa darasa kuandika sentensi ambayo inaweza kusaidia kuhamasisha mtu kuepuka dhambi, kulingana na kile ambacho amejifunza kutoka 2 Samweli 11. Waalike washiriki wachache wa darasa kutoa mawazo yao.

  • Unaweza kutumia 2 Samweli 11 kujadili hatari za ponografia na dhambi nyingine za ngono. Kufanya hivi, darasa lingeweza kupitia kwa pamoja sehemu ya ujumbe wa Mzee L. Whitney Clayton “Blessed Are All the Pure in Hear” (Liahona, Mei 2007, 51–53). Je, ni ushauri gani Mzee Clayton anatoa juu ya hatari za ponografia? Pia mnaweza kutazama video “To Look Upon” (ChurchofJesusChrist.org). Mwokozi anawezaje kutusaidia kushinda majaribu au tabia hizi?

    Pengine washiriki wa darasa wangeweza kushiriki maoni ambayo wameona yanafaa katika juhudi zao za kulinda familia zao dhidi ya ponografia au kushinda athari za ponografia. Ujumbe wa Dada Linda S. Reeves “Protection from Pornography—a Christ-Focused Home” unaweza kusaidia (Liahona, Mei 2014, 15–17; ona pia “Nyenzo za Ziada”).

Picha
Hekalu la Barranquilla Columbia

Hekalu ni nyumba ya Bwana.

1 Wafalme 8:22–61

Mahekalu huleta baraka.

  • 1 Wafalme 8 inaelezea baraka ambazo Sulemani alitafuta kwa watu wake wakati hekalu lilipokamilishwa. Unaweza kugawanya mistari ya 22–61 miongoni mwa washiriki wa darasa na waombe waelezee kitu wanachokipata katika mistari yao ambacho kinawachochea katika ibada yao ya hekaluni. Washiriki wa darasa wangeweza kushiriki jinsi kuabudu katika nyumba ya Bwana kulivyobariki maisha yao.

1 Wafalme 8:61; 11:1–11

“Moyo wake haukuwa mkamilifu kwa Bwana.”

  • Inamaanisha nini “ mioyo [yetu] na … iwe kamili kwa Bwana”? (1 Wafalme 8:61). Je, hiyo ni tofauti na matendo yetu kuwa kamili? Kwa jinsi gani? Washiriki wa darasa wanapotafakari maswali haya, wangeweza kusoma 1 Wafalme 11:1–11 na kuona kitu ambacho Bwana anasema juu ya moyo wa Sulemani. Tunawezaje kuepuka makosa aliyoyafanya?

Picha
ikoni ya nyenzo za ziada

Nyenzo za Ziada

Kusimamisha safina.

Rais Brigham Young alifundisha: “Achilia mbali Ufalme, Bwana anasimamisha safina; na ikiwa inashindana, na inaonekana inahitaji kutulia, ikiwa njia ni kidogo wakati mwingine, na kwa muonekano wote unatishia kuangushwa kwake, kuwa mwangalifu jinsi unavyonyosha mkono wako kuituliza; wacha tusiwe wenye kuingilia kati yale ambayo hayatuhusu; achana nayo, ni kazi ya Bwana” (Discourses of Brigham Young, sel. John A. Widtsoe [1954], 66).

Kuzilinda familia dhidi ya Ponografia.

Dada Linda S. Reeves alifundisha: “Je, tunawezaje kuwalinda watoto na vijana wetu? Machujio ni zana muhimu, lakini chujio kubwa zaidi ulimwenguni, na la kipekee ambalo hatimaye litafanya kazi, ni chujio la ndani ya mtu binafsi ambalo linatokana na ushuhuda wa kina na wa kudumu wa upendo wa Baba yetu wa Mbinguni na dhabihu ya Mwokozi wetu ya kulipia dhambi kwa ajili ya kila mmoja wetu” (“Protection from Pornography—a Christ-Focused Home,” Liahona, Mei 2014, 16; ona pia Joy D. Jones, “Kushughulikia Pornografia: Linda, Jibu, na Ponya,” Ensign, Okt. 2019, 22–27).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Hakikisha kwamba unafundisha mafundisho ya kweli. “Kila mara jiulize, ‘Ni kwa jinsi gani kile ninachofundisha kitawasaidia washiriki wa darasa langu kujenga imani katika Kristo, kutubu, kufanya na kushika maagano na Mungu, na kupokea Roho Mtakatifu?’” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 20).

Chapisha