Agano la Kale 2022
Juni 27–Julai 3. 1 Wafalme 17–19: “Bwana Akiwa Ndiye Mungu, Mfuateni”


“Juni 27–Julai 3. 1 Waamuzi 17–19: ‘Bwana Akiwa Ndiye Mungu, Mfuateni,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano la Kale 2022 (2021)

“Juni 27–Julai 3. 1 Wafalme 17–19,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2022

Picha
Eliya akiwa amesimama kando ya madhabahu inayowaka moto

Eliya Anabishana dhidi ya Makuhani wa Baali, na Jerry Harston

Juni 27–Julai 3

1 Wafalme 17–19

“Bwana Akiwa Ndiye Mungu, Mfuateni”

Makusudi ya maandiko—na darasa lako—ni kujenga imani katika Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo. Kusudi hili na liongoze maamuzi unayofanya juu ya nini cha kufundisha na maswali gani ya kuuliza.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kuelezea utambuzi wao kuhusu 1 Wafalme 17–19, unaweza kuwaalika wafikirie kichwa cha habari kwa kila sura hizi. Je, ni mistari gani iliyowafanya wafikirie juu ya vichwa hivi?

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

1 Wafalme 17:8–16; 19:19–21

Mwaliko wa kutoa dhabihu ni fursa ya kuifanyia mazoezi imani yetu.

  • Mfano wa mjane wa Sarepta unaweza kuwashawishi washiriki wa darasa lako wakati ambapo imani yao inajaribiwa. Unaweza kuanza kwa kuwaomba waorodheshe chaguzi ambazo zinahitaji imani katika Yesu Kristo. Kisha wangeweza kusoma kifungu katika 1 Wafalme 17:8–16 na kuongea kuhusu kile ambacho hadithi hii inawafundisha kuhusu kuwa na imani. Wahimize washiriki wa darasa kushiriki hisia zao kuhusu mjane huyu na jinsi mfano wake unavyowapa mwongozo wa kiungu wa kutumia imani yao. Je, imani yake inafanana vipi na imani ambayo Elisha alionyesha katika 1 Wafalme 19:19–21? Labda washiriki wa darasa wangekuwa tayari kushiriki dhabihu waliyofanya kwa Bwana na jinsi Bwana alivyowabariki.

  • Hadithi ya mjane wa Sarepta pia inaweza kutufundisha juu ya baraka zinazotokana na dhabihu. Unaweza kuwaomba washiriki wa darasa kutafakari ni jinsi gani wangejibu kauli kama hizi: “Sina uwezo wa kulipa zaka” au “Nina shughuli nyingi sana kukubali wito wa kutumikia.” Je, 1 Wafalme 17:8–16 inatufundisha nini ambacho kinaweza kutumika kwenye maelezo haya? Ni jinsi gani maarifa yetu juu ya Mwokozi hutusaidia wakati tunapoombwa kutoa dhabihu? Maneno ya Mzee Lynn G. Robbins katika “Nyenzo za Ziada” pia yangeweza kusaidia.

1 Wafalme 6:17–39

“Bwana Akiwa Ndiye Mungu, Mfuateni.”

  • Majadiliano ya 1 Wafalme 18:17–39 yangeweza kuwasaidia washiriki wa darasa kuwa na msimamo zaidi wa kumfuata Yesu Kristo na kumtumaini Yeye. Baada ya kupitia upya hadithi hii na darasa, unaweza kuandika ubaoni swali ambalo Eliya aliwauliza watu wa Israeli: “Mtasitasita katikati ya mawazo mawili hata lini?” (mstari wa 21). Washiriki wa darasa na waelezee kile wanachohisi swali hili lina maanisha nini. Je, ni sababu gani watu wanaweza kuwa walikuwa “wakisimama” (ambapo inaweza kumaanisha kusita, kuyumba, au kulegea) kati ya kumfuata Bwana na kumfuata Baali? Kwa nini wakati mwingine tunakuwa na shaka kuhusu kumfuata Yesu Kristo? Washiriki wa darasa wangeweza kushiriki uzoefu ambao umewasaidia wao kuchagua kumfuata Mwokozi.

Picha
Eliya amesimama juu ya mwamba

Mfano wa maelezo ya 1 Wafalme 19:11–12. Nabii, © Robert Booth Charles/Bridgeman Images

1 Wafalme 19:1–12

Bwana mara nyingi huongea kwa njia tulivu, rahisi.

  • Watu wengi wana changamoto ya kutambua wakati Bwana anapowasiliana na wao. Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kutambua zaidi sauti ya Bwana, ungeweza kuwaalika kusoma 1 Wafalme 19:1–12 na kuelezea kile Eliya alichojifunza. Labda washiriki wa darasa wangeweza kushiriki mambo ambayo umewafundisha kuhusu njia tofauti Bwana anazoongea nao. Ukitaka unaweza kuonyesha video ya “How Can I Feel the Holy Ghost More Often?” (kutoka “Face to Face with President Eyring and Elder Holland” [worldwide youth broadcast, Mar. 4, 2017], ChurchofJesusChrist.org).

  • Ili kusaidia majadiliano ya haraka juu ya kifungu “sauti ndogo tulivu,” unaweza kuonyesha vitu (au picha za vitu) ambavyo vinaweza kusaidia washiriki wa darasa kutafakari kifungu hicho. Washiriki wa darasa wangeweza kupendekeza mifano mingine. Kwa nini maneno “tulivu” na “ndogo” ni njia nzuri za kuelezea sauti ya Roho? Kwa maelezo mengine, washiriki wa darasa wangeweza kusoma maandiko kama Helamani 5:30; 3 Nefi 11:3–7; Mafundisho na Maagano 6:22–23; 8:2–3; 9:8–9; 11:12–14; 36:2. Wanaweza kushiriki maandiko mengine juu ya kumtambua Roho. Je, maandiko haya yanashauri nini juu ya kile tunachopaswa kufanya ili kusikia sauti ya Bwana? Video “Feeling the Holy Ghost” au “Voice of the Spirit” zinaweza kusaidia (ChurchofJesusChrist.org).

Picha
ikoni ya nyenzo za ziada

Nyenzo za Ziada

Mjane wa Sarepta.

Mzee Lynn G. Robbins alisema: Eliya alielewa fundisho kwamba baraka huja baada ya kujaribiwa kwa imani yetu [ona Etheri 12:6; Mafundisho na Maagano 132:5]. Hakuwa mbinafsi. Kama mtumishi wa Bwana, Eliya alikuwepo ili kutoa, sio kuchukua [ona 1 Wafalme 17:13–16]. … Sababu mojawapo Bwana anaelezea mafundisho kwa mifano ya mazingira halisi kabisa ni ili kuondoa visingizio. Kama Bwana anatarajia hata mjane masikini kulipa sarafu yake, hiyo inawaacha wapi wengine wote ambao wanaona kuwa haifai au sio rahisi kutoa dhabihu?” (“Zaka—ni Amri Hata kwa Fukara,” Liahona, Mei 2005, 35).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Kuwa chombo kinyenyekevu cha Roho. “Lengo lako kama mwalimu sio kuwasilisha somo lenye kuvutia bali ni kuwasaidia wengine kupokea ushawishi wa Roho Mtakatifu, ambaye ni mwalimu wa kweli” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 10).

Chapisha