Agano la Kale 2022
Julai 18–24. Ezra 1; 3–7; Nehemia 2; 4–6; 8: “Hii Ni Kazi Kubwa Ninayoifanya Mimi”


“Julai 18–24. Ezra 1; 3–7; Nehemia 2; 4–6; 8: ‘Hii Ni Kazi Kubwa Ninayoifanya Mimi’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano la Kale 2022 (2021)

“Julai 18–24. Ezra 1; 3–7; Nehemia 2; 4–6; 8,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2022

Picha
hekalu la Zerubbabeli

Kielelezo cha hekalu la Zerubbabeli, na Sam Lawlor

July 18–24.

Ezra 1; 3–7; Nehemia 2; 4–6; 8

“Hii Ni Kazi Kubwa Ninayoifanya Mimi”

Unapowaalika washiriki wa darasa lako kuelezea kitu kile kilichoonekana cha kipekee kwao katika vitabu vya Ezra na Nehemia, pia shiriki mawazo yoyote uliyopokea ulipokuwa ukijisomea.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Wakati mwingine kuandika maneno muhimu au vifungu vya maneno ubaoni kunaweza kuwakumbusha washiriki wa darasa mambo waliyojifunza kutoka katika maandiko na kufanya iwe rahisi kwao kuelezea. Kwa mfano, unaweza kuandika Jenga Upya, Karabati, na Anzisha Upya ubaoni na waalike washiriki wa darasa kushiriki mistari kutokana na usomaji wao ambayo inahusiana na mojawapo au zaidi ya maneno haya.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Ezra 3:8–13; 6:16–22

Mahekalu yanaweza kuleta shangwe.

  • Kusoma kuhusu shangwe ambayo Wayahudi walijisikia wakati hekalu lao likijengwa upya inaweza kusaidia washiriki wa darasa kujisikia kuwa na shukrani kwa mahekalu katika siku zetu. Labda unaweza kuwaalika washiriki wa darasa kurejelea Ezra 3:8–13 na 6:16–22 na kisha kujadili njia kadhaa ambazo Wayahudi walisherehekea ujenzi huo na kuwekwa wakfu kwa hekalu. Kwa nini ujenzi wa hekalu ni sababu ya kusherehekea? Unaweza kuwaalika washiriki wa darasa kushiriki jinsi mahekalu, na kazi tunayofanya humo, zinavyowaletea furaha. Maelezo katika “Nyenzo za Ziada” yanaweza kuwatia moyo washiriki wa darasa kuona shangwe ya kazi ya hekaluni.

    Picha
    familia ikitembea juu ya viwanja vya hekalu.

    Hekalu linaweza kuwa chanzo cha shangwe katika maisha yetu.

Ezra 4–5; Nehemia 2; 4; 6

Tunaweza kusaidia kazi ya Mungu kusonga mbele licha ya upinzani.

  • Vitabu vya Ezra na Nehemia vinaelezea watu wanaotimiza kazi muhimu licha ya upinzani kutoka kwa maadui zao. Ili kuanza majadiliano, unaweza kuuliza washiriki wa darasa ile “kazi kubwa” ya Nehemia (Nehemia 6:3) inaweza kulinganishwa na nini katika maisha yetu. Ni kazi gani muhimu ambayo Mungu ametupa kufanya? Kisha unaweza kusoma Ezra 4:4 na kujadili jinsi Shetani anavyojaribu kudhoofisha mikono yetu na kutusumbua katika kufanya kazi ya Mungu. Je, tunajifunza nini kutoka kwa Nehemia na wafanyakazi wenzake katika Nehemia 2:18–20; 4:6–9na 6:1–3? Je, inamaanisha nini kuwa na “moyo wa kufanya kazi” katika huduma ya Mwokozi? (Nehemia 4:6). Fikiria kushiriki sehemu ya ujumbe wa Rais Dieter F. Uchtdorf “We Are Doing a Great Work and Cannot Come Down” (Liahona, Mei 2009, 59–62), hususani sehemu mbili za mwisho.

  • Unaweza kuhisi kuhamasika kuongoza mjadala ukilinganisha juhudi za Zerubabeli za kujenga tena hekalu na juhudi zetu za kuhudhuria hekaluni na kufanya kazi ya uokoaji huko. Kwa mfano, ungeweza kuandika ubaoni vichwa vya habari viwili: Zerubabeli na Sisi. Chini ya Zerubabeli, washiriki wa darasa wangeweza kuandika kile “maadui wa Yuda na Benyamini” (Ezra 4:1) walichofanya ili kujaribu kuwazuia Zerubabeli na Wayahudi kujenga upya hekalu (ona Ezra 4). Chini ya Sisi, washiriki wa darasa wanaweza kuorodhesha njia ambazo adui hujaribu kutuzuia kuhudhuria hekaluni. Wangeweza kisha kupeana ushauri wao kwa wao kuhusu jinsi tunavyoweza kutafuta msaada wa Bwana katika kushinda huo upinzani.

Nehemia 8:1–2

Tunabarikiwa tunapojifunza maandiko.

  • Labda washiriki wa darasa wangeweza kusoma Nehemia 8:1–12 pamoja na kujadili jinsi Ezra na watu wake walivyojisikia kuhusu Mungu na neno Lake. Wahamasishe washiriki wa darasa kurejelea kwenye mistari maalum ambayo inaonyesha jinsi walivyojisikia. Waalike washirki wa darasa kuelezea jinsi wanavyojisikia kuhusu neno la Mungu. Ni kwa jinsi gani tunaweza kuboresha juhudi zetu za kusoma neno la Mungu?

Picha
ikoni ya nyenzo za ziada

Nyenzo za Ziada

Pata shangwe ya hekalu.

Rais Russell M. Nelson alifundisha:

“Tunaweza tukapewa mwongozo wa kiungu siku nzima kuhusu mambo ya hekaluni na historia ya familia ambayo wengine wamepata. Lakini ni lazima tufanye kitu fulani ili tuweze kuipata shangwe hiyo sisi wenyewe. Ningependa kutoa changamoto kwa kila mmoja wetu ili hisia nzuri ya kazi hii iweze kuendelea na hata kuongezeka. “Ninakualikeni ninyi kwa sala mfikirie ni dhabihu gani—hususani dhabihu ya muda—ambayo mnaweza kuitoa ili kufanya kazi zaidi ya hekaluni na historia ya familia kwa mwaka huu.

Sisi tumejiingiza katika kazi ya Mwenyezi Mungu. Yu hai. Yesu ndiye Kristo. Hili ni Kanisa Lake. Sisi ni watoto Wake wa agano. Anaweza kututegemea” (Russell M. Nelson na Wendy W. Nelson, “Fungua Mbingu kupitia Kazi za Hekaluni na Historia ya Familia,” Liahona, Okt. 2017, 39).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Wajumuishe wazazi wa vijana. Kama unawafundisha vijana, waelezee wazazi wao kile unachowafundisha. Wanaweza kukusaidia kuelewa mahitaji ya vijana wao na jinsi ya kuwasaidia. Hii pia inaweza kuwa njia nzuri ya kuhimiza majadiliano ya kifamilia juu ya kile ambacho vijana wanajifunza darasani. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 27.)

Chapisha