Agano la Kale 2022
Julai 4–10. 2 Wafalme 2–7: “Yuko Nabii katika Israeli”


“Julai 4–10. 2 Wafalme 2–7: ‘Yupo Nabii katika Israeli,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano la Kale 2022 (2021)

“Julai 4–10, 2 Nefi 2–7 Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2022

Picha
Elisha akimwonyesha mtumishi magari ya moto

Kielelezo cha Elisha akimwonyesha mtumishi wake magari ya moto , © Review & Herald Publishing/licensed from goodsalt.com

Julai 4–10

2 Wafalme 2–7

“Yuko Nabii katika Israeli”

Unapojiandaa kufundisha, soma 2 Wafalme 2–7 ukitafuta mwongozo wa kiungu kwa ajili ya maisha yako mwenyewe. Kisha sikiliza ushawishi kuhusu ujumbe ambao utabariki washiriki wa darasa lako.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Wakati mwingine washiriki wa darasa wanahitaji muda wa kupitia upya kwa ufupi sura walizosoma kabla ya kuweza kuelezea utambuzi walioupata kutoka kwenye usomaji wao binafsi wa maandiko. Jaribu kutoa dakika chache kwa ajili ya hili mwanzoni mwa darasa; kisha waalike washiriki wa darasa kuelezea kitu walichojifunza.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

2 Wafalme 26

Mungu anaweza kufanya miujiza katika maisha yetu.

  • Unapojadili miujiza katika 2 Wafalme 2–6, inaweza kusaidia kuwauliza washiriki wa darasa kufafanua neno muujiza. Unaweza kuelezea utambuzi huu kutoka kwa Rais Howard W. Hunter: “[Miujiza] ni dhihirisho la nguvu za [Mungu] ambazo hatuna uwezo wa kuzielezea au kuzielewa kikamilifu. … Ishara hizi na maajabu yalikuwa dhahiri zaidi katika maisha na huduma ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu mwenyewe. Lakini ya kushangaza na kujazwa maajabu kama vile ilivyokuwa, miujiza mingi ya Kristo ilikuwa ni akisi tu ya maajabu makubwa zaidi ambayo Baba yake alikuwa ameyafanya mbele yake na anaendelea kufanya kote kutuzunguka sisi. … Kutakuwa na miujiza mingi kila wakati ikiwa tuna macho ya kuona na masikio ya kusikia” (“The God That Doest Wonders,” Ensign, Mei 1989, 15–16). Je, utambuzi huu unatusaidiaje sisi kuona mkono wa Mungu katika maisha yetu?

  • Fikiria kuwauliza washiriki wa darasa kuorodhesha miujiza iliyoelezewa katika 2 Wafalme 2–6. Je, tunajifunza nini kuhusu Bwana kutoka kwenye miujiza hii? Washiriki wa darasa pia wanaweza kuwa tayari kuzungumza juu ya miujiza—mikubwa au midogo—ambayo wao au familia zao wamepata. Je, tunawezaje kutambua vyema miujiza ya Mungu maishani mwetu—pamoja na ile ambayo ni tofauti na ile tuliyotarajia?

  • Washiriki wa darasa wanaweza kupata msukumo kulinganisha baadhi ya miujiza ambayo Elisha alifanya na mingine ambayo Yesu Kristo alifanya (ona 2 Wafalme 4:8–37 na Luka 7:11–16; 2 Wafalme 4:42–44 na Yohana 6:1–13; 2 Wafalme 5:1–15 na Luka 17:11–19). Miujiza hii inatufundisha nini sisi kuhusu Mwokozi na manabii Wake?

2 Wafalme 5:1–19

Ikiwa sisi ni wanyenyekevu na watiifu, Yesu Kristo anaweza kutuponya.

  • Somo moja tunaloweza kujifunza kutokana na kupona kwa ukoma wa Naamani ni umuhimu wa unyenyekevu. Ili kuanza majadiliano, unaweza kuandika kwenye ubao kiburi cha Naamani na unyenyekevu wa Naamani. Washiriki wa darasa wanaweza kutafuta 2 Wafalme 5:1–19 na kuandika ubaoni vifungu vya maneno vinavyoonyesha kiburi au unyenyekevu wa Naamani. Je, ni kwa jinsi gani sisi wakati mwingine tuko kama Naamani? Je, wakati mwingine tunakuwaje kama watumishi wake? Ni kwa jinsi gani tumekuja kujua kile alichokuja kukijua Naamani?

  • Somo jingine tunaloweza kujifunza kutoka kwenye hadithi hii ni thamani ya kumtii Mungu katika mambo madogo. Unaweza kuanza kwa kusoma 2 Wafalme 5:9–12 na kuomba mawazo ya washiriki wa darasa kuhusu ni kwa nini Naamani “akaondoka kwa hasira” (mstari 12). Kwa nini wakati mwingine tunapendelea kufanya “jambo kubwa” ambalo Mungu hutuomba sisi, kuliko mambo rahisi? (mstari 13). Nini thamani ya kufanya mambo haya rahisi?

2 Wafalme 6:8–23

“Wale walio pamoja nasi ni wengi kuliko wale walio pamoja nao.”

  • Sisi sote tunazo nyakati ambapo tunahisi tuko pekee yetu au tunaogopa. Fikiria jinsi kujadili hadithi hiyo katika 2 Wafalme 6:8–23 inavyoweza kusaidia washiriki wa darasa ambao wanajisikia hivi. Unaweza kuanza kwa kuwauliza tu washiriki wa darasa ni nini kinachowavutia kuhusu mistari hii. Wanaweza pia kushiriki matukio wakati “Bwana alipofungua macho [yao]” (mstari 17) na kuwasaidia kuona kwamba hawako peke yao (ona pia “Nyenzo za Ziada”). Je, tunawezaje kusaidiana ili “tusiogope”? (mstari 16).

Picha
ikoni ya nyenzo za ziada

Nyenzo za Ziada

“Tufungue macho yetu ya kiroho.”

Inarejelea hadithi katika 2 Wafalme 6:8–23, Mzee Ronald A. Rasband alisema:

“Yawezekana au haiwezekani kutumiwa magari ya moto ili kuondoa hofu zetu na kuwashinda mashetani wetu , lakini somo ni bayana. Bwana yu pamoja nasi, anatujali na anatubariki katika njia ambazo ni Yeye pekee ndiye anayeweza kufanya hivyo. Sala inaweza kushusha chini nguvu na ufunuo ambao tunauhitaji ili kulenga mawazo yetu juu ya Yesu Kristo na dhabihu Yake ya kulipia dhambi. Bwana alijua ya kwamba wakati mwingine tungejisikia woga. Nimelipitia hilo vivyo hivyo na wewe pia. … Katika Kanisa hili tunaweza tukawa wachache kwa idadi kulingana na jinsi dunia inavyofafanua ushawishi, lakini tunapofungua macho yetu ya kiroho, ‘walio pamoja nasi ni wengi kuliko wale walio pamoja nao’ [2 Wafalme 6:16]” (“Usifadhaike,” Liahona, Nov. 2018, 18–19).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Warejeze wanafunzi kwenye maandiko. Wakati wowote unapoweza, wahimize washiriki wa darasa kurejelea kwenye maandiko na maneno ya manabii walio hai kwa ajili ya kupata mwongozo, majibu ya maswali, na msaada. Neno la Mungu ni chanzo kikuu cha ukweli. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 21.)

Chapisha