Agano la Kale 2022
Agosti 15–21. Zaburi 49–51; 61–66; 69–72; 77–78; 85–86: “Nitatangaza Yale Ambayo Amefanya Kwa ajili ya Nafsi Yangu”


“Agosti 15–21. Zaburi 49–51; 61–66; 69–72; 77–78; 85–86: ‘Nitatangaza Yale Ambayo Amefanya Kwa ajili ya Nafsi Yangu,’” Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Shule ya Jumapili: Agano la Kale 2022 (2021)

“Agosti 15–21. Zaburi 49–51; 61–66; 69–72; 77–78; 85–86,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2022

Picha
Yesu ameshikilia taa

Kuokoa Kile Kilichopotea, na Michael T. Malm

Agosti 15–21.

Zaburi 49–51; 61–66; 69–72; 77–78; 85–86

“Nitatangaza Yale Ambayo Amefanya Kwa ajili ya Nafsi Yangu”

Fikiria ushauri wa Mzee David A. Bednar ukiwa unajiandaa kufundisha: “Kuzungumzia na kusimulia peke yake siyo kufundisha. [Kufundisha] injili katika njia ya Bwana kunajumuisha kuchunguza na kusikiliza na kutambua kama vigezo vya awali kabla ya kuanza kuongea” (“Becoming a Preach My Gospel Missionary,” New Era, Okt. 2013, 6).

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Njia mojawapo ya kuwaalika washiriki wa darasa kuelezea kitu walichosoma wiki hii ni kuandika kwenye ubao “Midomo yangu itafurahi sana” au “Ulimi wangu nao utasimulia haki yako” (Zaburi 71:23-24). Washiriki wa darasa wangeweza kushiriki kile walichokiona kwamba huwasaidia “kushangilia sana” au “kuzungumza juu ya haki [ya Bwana].”

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Zaburi 51; 85–86

“Wewe, Bwana, U mwema, na umekuwa tayari kusamehe.”

  • Zaburi 51 inaelezea hisia ambazo wengi wetu tunakuwa nazo tunapotafuta kutubu na kusamehewa. Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kuelewa vizuri toba na kuhisi msukumo wa kutubu mara nyingi, unaweza kupendekeza kwamba wachunguze Zaburi 51 wakiwa na swali hili akilini: Kutubu kuna maana gani? Kisha waache washiriki majibu yanayopatikana. (Nyenzo za Ziada” ina utambuzi wenye kusaidia.) Kwa nini toba wakati mwingine inaonekana kutotamanika? Je, tunapata kitu gani katika zaburi hii ambacho kinaweza kufanya toba kuwa yenye shangwe?

  • Je, tunawezaje kuelezea jinsi kupokea msamaha wa dhambi kupitia nguvu ya Yesu Kristo ya kulipia dhambi kunavyokuwa? Waalike washiriki wa darasa kutoa mawazo yao, na wahimize kutafuta vifungu vya maneno katika Zaburi 51; 85–86 ambavyo vinaelezea matokeo ya msamaha Wake wenye utakaso katika maisha yetu (kwa mfano, ona Zaburi 51:1–2, 7–12; 85:2–9). Fikiria kuonyesha picha au vitu ili kusaidia washiriki wa darasa kutambua misemo hii. Washiriki wa darasa wangeweza kushiriki maoni yao kuhusu Mwokozi Yesu Kristo na utayari wake wa kulipa kwa ajili ya dhambi zetu ili sisi tuweze kusamehewa. Unaweza pia kuimba pamoja wimbo kuhusu dhabihu ya Mwokozi ya kulipia dhambi, kama vile “I Stand All Amazed” (Nyimbo za Kanisa, na. 193).

  • Ili kutubu, tunahitaji imani sio tu kwamba Yesu Kristo anaweza kutusafisha lakini pia kwamba Yeye atafanya hivyo. Washiriki wa darasa wanaweza kuwa wamepata vifungu vya maneno katika Zaburi 51; 85–86 wiki hii ambavyo vimeimarisha imani yao katika utayari wa Bwana wa kusamehe. Wahimize kushiriki kitu walichokipata. Unaweza pia kuwaelekeza kwenye Zaburi 86:5, 13, 15 na waulize mistari hii inafundisha nini kuhusu Bwana. Inaweza kumaanisha nini kwamba Yeye ni “mwingi wa rehema na kweli”? (mstari wa 15). Kwa nini ni muhimu kwetu kujua hili?

Zaburi 66:5–20.

Ushuhuda wetu juu ya Yesu Kristo unaweza kuwasaidia wengine kuja Kwake.

  • Moja ya baraka kubwa za kukusanyika pamoja katika Shule ya Jumapili ni fursa ya kupata nguvu kutokana na imani na ushuhuda wa wafuasi wengine wa Yesu Kristo. Ili kutoa nafasi hii kwa darasa lako, unaweza kuwaomba washiriki wa darasa kusoma Zaburi 66:16 na kutafakari swali hili: Kama ungetakiwa “utangaze kile ambacho [Bwana] amefanya kwa ajili ya nafsi [yako],” ungetangaza nini? Wakiwa wanatafakari, wanaweza kusoma mistari ya 5–20 kwa ajili ya kupata mawazo. Na waandike majibu yao. Kisha waalike “watamkiane” kwa kila mmoja—katika vikundi vidogo au kwa darasa zima—kile ambacho Yesu Kristo amekifanya kwa ajili ya nafsi zao.

    Picha
    vijana wawili wakiongea

    Tunaweza kushiriki na wengine shuhuda zetu kwa kile ambacho Bwana alitufanyia.

Picha
ikoni ya nyenzo za ziada

Nyenzo za Ziada

Toba inamaanisha badiliko.

Rais Russell M. Nelson alielezea toba kwa njia hii:

“Wakati Yesu anapotuomba mimi na wewe ‘tutubu,’ Anatualika kubadili akili zetu, ufahamu wetu, roho zetu—hata jinsi tunavyopumua. Anatuomba tubadili jinsi tunavyopenda, tunavyofikiri, tunavyohudumu, tunavyotumia muda wetu, tunavyowatendea wake zetu, tunavyowafundisha watoto wetu, na hata jinsi tunavyoitunza miili yetu.

“Hakuna kinachotoa uhuru zaidi, cha kiungwana zaidi, au cha muhimu zaidi kwa maendeleo yetu binafsi kuliko ilivyo fokasi ya mazoea ya kila siku kwenye toba. Toba siyo tukio; ni mchakato. Ni ufunguo kwa furaha na amani ya akili. Inapoambatana na imani, toba hufungua kufikia kwetu kwenye nguvu za Upatanisho wa Yesu Kristo. …

“Tunapochagua kutubu, tunachagua kubadilika! Tunamruhusu Mwokozi kutubadilisha kuwa toleo zuri zaidi la sisi wenyewe. Tunachagua kukua kiroho na kupokea shangwe—shangwe ya ukombozi katika Yeye. Tunapochagua kutubu, tunachagua kuwa zaidi kama Yesu Kristo!“ (“Tunaweza Kufanya Vizuri Zaidi na Kuwa Wazuri Zaidi,” Liahona, Mei 2019, 67).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Uliza Maswali Ambayo Yanagusa Moyo na Akili. “Waombe wanafunzi kuelezea jinsi wanavyojisikia kuhusu kifungu cha maandiko, je, watu katika maandiko yawezekana walikuwa wakijisikiaje, au je, ukweli katika kifungu hiki cha maneno kinahusianaje na maisha yetu” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 31).

Chapisha