Agano la Kale 2022
Agosti 8–14. Zaburi 1–2; 8; 19–33; 40; 46: “Bwana Ndiye Mchungaji Wangu”


“Agosti 8–14. Zaburi 1–2; 8; 19–33; 40; 46: ‘Bwana Ndiye Mchungaji Wangu,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano la Kale 2022 (2021)

“Agosti 8–14. Zaburi 1–2; 8; 19–33; 40; 46,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2022

Picha
Yesu akitembea na kondoo

Bwana Ndiye Mchungaji Wangu, na Yongsung Kim, havenlight.com

Agosti 8–14

Zaburi 1–2; 8; 19–33; 4046

“Bwana Ndiye Mchungaji Wangu”

Panga njia za washiriki wa darasa kuelezea uzoefu wa kiroho ambao wanapata wanaposoma Zaburi.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Kuwaalika washiriki wa darasa kuelezea kile walichogundua katika Zaburi inaweza kuwa rahisi kama kuuliza maswali kama haya: Je, Roho alikufundisha nini uliposoma Zaburi wiki hii? Ni zaburi zipi zilizo kusaidia kujisikia karibu sana na Bwana?

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Zaburi 1; 23; 26–2846

Zaburi inatufundisha kumtumaini Bwana.

  • Muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia unapendekeza kusoma Zaburi 1; 23; 26–2846 na kuangalia yafuatayo:

    • Mwaliko wa kumtumaini Bwana

    • Maneno ambayo yanamwelezea Bwana

    • Maneno ambayo yanaelezea amani, nguvu, na baraka zingine Anazotoa

    • Maneno ambayo yanawaelezea wale wanaomtumaini Yeye

    Unaweza kuandika vifungu hivi vya maneno ubaoni na uwaalike washiriki wa darasa waandike, karibu na kila kifungu, kitu walichopata katika Zaburi 1; 23; 26–28; au 46. Kama wanahitaji msaada, unaweza kuwaonyesha mistari hii: Zaburi 1:1–4; 23:1–6; 26:1, 6–8, 12; 27:1, 3, 8, 14; 28:1, 7; 46:1–3, 10. Washiriki wa darasa wangeweza kushiriki hisia walizokuwa nazo juu ya Mwokozi wanaposoma zaburi hizi.

  • Kwa sababu Zaburi zilikuwa kama nyimbo kwa Waisraeli, unaweza kuwaalika washiriki wa darasa kupendekeza nyimbo ambazo zinawakumbusha zaburi walizosoma wiki hii. Wanaweza kurejelea faharasa ya “Maandiko” mwishoni mwa kitabu cha nyimbo kwa maoni (ona pia orodha katika “Nyenzo za Ziada”). Washiriki wa darasa wangeweza kuimba chache ya hizi nyimbo na kutambua mada za kawaida katika nyimbo na zaburi. Je, tunapata ujumbe gani wa amani na imani katika Yesu Kristo?

Zaburi 2; 22; 31:5

Zaburi zinaelekeza akili zetu kwenye maisha na huduma ya Yesu Kristo.

  • Kusoma Zaburi—hususani zile zinazoelekeza kwenye maisha ya Mwokozi—inaweza kuwa njia nzuri ya kuimarisha imani katika Yesu Kristo. Unaweza kugawanya darasa katika vikundi vya watu wawili wawili au zaidi na kipe kila kikundi moja ya jozi zifuatazo za marejeleo: Zaburi 2:1–3 na Matendo ya Mitume 4:24–28; Zaburi 2:7 na Matendo ya Mitume 13:30–33; Zaburi 22:1 na Mathayo 27:45–46; Zaburi 22:7–8 na Mathayo 27:39–43; Zaburi 22:16 na Luka 23:32–33; Zaburi 22:18 na Mathayo 27:35; Zaburi 31:5 na Luka 23:46. Omba kila kikundi kutafuta jinsi unabii katika Zaburi ulivyotimizwa katika maisha ya Mwokozi na ujadili jinsi maandiko haya yanavyoimarisha ushuhuda wao juu ya Mwokozi.

    Au unaweza kuandika marejeo ya maandiko ubaoni na uwaalike washiriki wa darasa waoanishe kifungu kutoka Zaburi na tukio linalofanana katika Agano Jipya.

    Unaweza pia kualika washiriki wa darasa kushiriki marejeo mengine kwa Mwokozi ambayo walipata katika masomo yao juu ya Zaburi (kama vile Zaburi 34:20; 41:9; ona pia Luka 24:44).

    Baada ya washiriki wa darasa kujadili maandiko haya, wangeweza kuzungumza juu ya kwa nini zaburi hizi zingekuwa na maana kwa Wayahudi ambao walimjua Mwokozi. Kwa nini zinamaana kwetu sisi?

Zaburi 23.

“Bwana ndiye mchungaji wangu”

  • Kuwasaidia washiriki wa darasa kujadili picha na ishara katika Zaburi 23, fikiria kuonyesha picha zinazohusiana na maoni katika zaburi, kama vile zile zilizo katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia. Unaweza kisha kuwaomba washiriki wa darasa watambue maneno au vifungu vya maneno vyenye maana katika zaburi na kujadili kile yanachoweza kuwakilisha. Kwa mfano, ni vipi misemo kama “katika malisho ya majani mabichi hunilaza” au “maji ya utulivu” huleta akilini? Je, “gongo” na “fimbo” vyanifariji inaweza kumaanisha nini? Inaweza kumaanisha nini kwa “kikombe” chetu kinafurika? Je, alama hizi zinatufundisha nini kuhusu Yesu Kristo? Unaweza kupendekeza kwamba washiriki wa darasa warudie zaburi hiyo, wakibadilisha baadhi ya alama na maana zinazopatikana zilizojadiliwa na darasa.

Picha
ikoni ya nyenzo za ziada

Nyenzo za Ziada

Nyimbo zinazohusiana na Zaburi.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Tumia muziki. Nyimbo zinamwalika Roho wa Bwana, kuleta hisia za uchaji, hutuunganisha sisi kama washiriki, na kutoa njia kwetu ya kutoa sifa kwa Bwana. Nyimbo hutupeleka kwenye toba na matendo mema, hujenga ushuhuda na imani, huwafariji wachovu, kuwafariji wenye kuomboleza, na kutupa mwongozo wa kiungu wa kuvumilia hadi mwisho” (Nyimbo za Kanisa, ix).

Chapisha