Agano la Kale 2022
Agosti 8–14. Zaburi 1–2; 8; 19–33; 40; 46: “Bwana ndiye Mchungaji Wangu”


“Agosti 8–14. Zaburi 1–2; 8; 19–33; 40; 46: ‘Bwana ndiye Mchungaji Wangu,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano la Kale 2022 (2021)

“Agosti 8–14. Zaburi 1–2; 8; 19–33; 40; 46,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2022

Picha
Yesu akitembea pamoja na kondoo

Bwana Ndiye Mchungaji Wangu, na Yongsung Kim, havenlight.com

Agosti 8–14

Zaburi 1–2; 8; 19–33; 4046

“Bwana ndiye Mchungaji Wangu”

Usihisi umewekewa kikomo kwenye kuchagua Zaburi au kanuni zilizopendekezwa katika muhtasari huu. Mruhusu Roho akuongoze kwenye kweli ambazo zinakusaidia kuhisi uko karibu na Bwana.

Andika Misukumo Yako

Hatujui kwa uhakika nani aliandika Zaburi. Baadhi zimedhaniwa kuwa ni za Mfalme Daudi, lakini nyingi zake, waandishi wake hawajulikani. Bado hata baada ya kusoma Zaburi, tunaweza kuhisi kama vile tunajua mioyo ya Watunga zaburi, hata kama hatujui majina yao. Kile tusichofahamu ni kwamba Zaburi ilikuwa ni sehemu muhimu ya kuabudu kwa Waisraeli, na tunajua kwamba Mwokozi amezinukuu mara kwa mara. Katika Zaburi, tunapata dirisha kuingia kwenye moyo wa watu wa kale wa Mungu. Tunaona jinsi walivyohisi kuhusu Mungu, kitu gani wao walichohofia, na namna walivyopata amani. Kama waaminio leo, duniani kote, bado tunatumia maneno haya katika kumwabudu kwetu Mungu. Waandishi wa Zaburi inaonekana walikuwa na dirisha kuingia katika nafsi zetu na inaonekana walikuwa wamepata njia ya kuelezea jinsi tunavyohisi kuhusu Mungu, kile tunachohofia, na jinsi tunavyopata amani.

Kwa ajili ya muhtasari wa kitabu cha Zaburi, ona “Zaburi” katika Kamusi ya Biblia.

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

Zaburi 1; 23; 26–2846

Zaburi hutufundisha sisi kumtumaini Bwana.

Unaweza kuona unaposoma Zaburi ni mara ngapi waandishi wanaelezea hofu, huzuni, au wasiwasi. Hisia kama hizi ni za kawaida, hata kwa watu wa imani. Lakini kile kinachosababisha Zaburi kuleta msukumo ni suluhisho inayotoa, ikijumuisha kumtumaini Bwana kikamilifu. Zingatia jumbe hizi zenye kuleta msukumo unaposoma Zaburi 1; 23; 26–2846. Angalia yafuatayo, na andika kile unachogundua:

  • Mwaliko wa kumtumaini Bwana:

  • Maneno yanayomwelezea Bwana:

  • Maneno yanayoelezea amani, nguvu, na baraka zingine Yeye anazotoa:

  • Maneno ambayo huwaelezea wale wanaomtumaini Yeye:

Zaburi 222

Zaburi huelekeza fikra zetu kwenye maisha na huduma ya Yesu Kristo.

Zaburi nyingi huelekeza kwenye maisha ya duniani ya Yesu Kristo. Wakristo katika nyakati za Agano Jipya waliona muunganiko huu pia—kwa mfano, walitambua katika Zaburi 2 marejeleo kwenye majaribu ya Yesu mbele ya Mfalme Herode na Pontio Pilato (ona Matendo ya Mitume 4:24–30). Fikiria kusoma Zaburi 2 na 22 pamoja na Mathayo 27:35–46; Luka 23:34–35; na Yohana 19:23–24. Angalia muunganiko kati ya maneno katika zaburi na maisha ya Mwokozi, na endelea kuangalia muunganiko unaofanana unapojifunza kitabu cha Zaburi katika wiki chache zijazo.

Fikiria kama ungekuwa Myahudi nyakati za Yesu ambaye alikuwa anaifahamu Zaburi na kuona muunganiko kwenye maisha ya Mwokozi. Ni kwa jinsi gani elimu hii ingekuwa baraka kwako?

Ona pia Zaburi 31:5; 34:20; 41:9; Luka 24:44; Waebrania 2:9–12.

Zaburi 8; 1933

“Nchi imejaa fadhili za Bwana.”

Kusoma Zaburi 8; 19; na 33 kunaweza kukupa msukumo kufikiria matendo mengi ya ajabu ya uumbaji ya Bwana. Zingatia mawazo na hisia zako unapofanya hivyo. Ni kwa jinsi gani uumbaji wa Bwana “huubiri utukufu wa Mungu” kwako? (Zaburi 19:1).

Zaburi 19:7–1129

Neno la Bwana lina nguvu, “huiburudisha nafsi.”

Katika Zaburi, maneno kama ushuhuda, sheria, amri, na hukumu yanaweza kurejelea neno la Bwana. Kumbuka hilo unaposoma Zaburi 19:7–11. Mistari hii inapendekeza nini kwako kuhusu neno la Bwana? Zaburi 29 inakufundisha nini kuhusu sauti Yake? Katika uzoefu wako, ni kwa jinsi gani neno, au sauti ya Bwana iliendana na maelezo haya?

Picha
Hekalu la Concepción Chile

Tunapaswa kutakaswa kiroho na kuwa safi ili kuingia katika uwepo wa Bwana.

Zaburi 24; 26–27

Kuingia katika uwepo wa Bwana kunahitaji usafi.

Kwa sababu hekalu huko Yerusalemu lilijengwa kilimani, kirai “mlima wa Bwana” (Zaburi 24:3) kinaweza kumaanisha hekalu au kwenye uwepo wa Mungu. Hii inaongeza nini katika uelewa wako wa Zaburi 24? Inamaanisha nini kwako kuwa na “mikono safi na moyo mweupe”? (Zaburi 24:4).

Ni kitu gani Zaburi 26 na 27 inakufundisha kuhusu nyumba ya Bwana?

Ona pia Zaburi 15; David A. Bednar, “Mikono Safi na Moyo Mweupe,” Liahona, Nov. 2007, 80–83.

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

Zaburi 22.Wakati mmojawapo wa wanafamilia akisoma zaburi hii, wengine wanaweza kuangalia mifanano katika Mathayo 27:35–46. Baadae wangeweza kushiriki hisia zao kuhusu Yesu Kristo na dhabihu Yake kwetu.

Zaburi 23.Zaburi 23 ilikuwa ni mwongozo wa kiungu wa nyimbo kadhaa, kama vile “The Lord Is My Shepherd” na “The Lord My Pasture Will Prepare” (Nyimbo za Kanisa, na. 108, 109). Labda familia yako ingependa kuimba mojawapo ya nyimbo hizi na kutambua maneno katika zaburi ambayo yanaweza kuwa yalitia mwongozo kwenye maneno ya nyimbo hizi. Au wanaweza kufurahia kuchora picha za kitu walichokiona katika zaburi au wimbo wa kanisa na waache wanafamilia wabahatishe mistari au maneno ya nyimbo yanayoendana na picha. Ni kwa jinsi gani Bwana ni kama mchungaji kwetu?

Zaburi 24:3–5.Ili kusisitiza umuhimu wa kuwa na mikono safi na moyo mweupe, ungeweza kusoma Zaburi 24:3–5 wakati wanafamilia wakiosha mikono yao. Ni kitu gani mikono inawakilisha katika zaburi? Moyo unaashiria nini? Tunaweza kufanya nini ili kusafisha mikono yetu na kutakasa mioyo yetu kiroho?

Zaburi 30:5, 11.Zaburi 30:5 inajumuisha ahadi kwamba “kilio huja kukaa usiku, lakini asubuhi huwa furaha.” Ni kwa jinsi gani Bwana amegeuza huzuni yetu kuwa furaha? Baadhi ya wanafamilia wanaweza kufurahia kuigiza kile kilichoelezwa katika mstari wa 11.

Zaburi 33.Tazama ni mara ngapi neno wote limetumika katika zaburi hii. Tunajifunza nini kuhusu Bwana kutokana na matumizi ya kujirudia rudia ya neno hili, hasa katika mistari 13–15?

Zaburi 46:10.Mnaweza kufanya kitu fulani kwa pamoja kinachoitaka familia kuwa “tulivu.” Ni kwa jinsi gani kutulia kunatusaidia sisi kumjua Mungu? Ni nafasi gani tulizonazo za kuwa watulivu na kuja kumjua Mungu?

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “The Lord Is My Shepherd,” Nyimbo za Kanisa, na. 108.

Kuboresha Kujifunza Binafsi

Kuwa mbunifu. Maandiko kama Zaburi mara nyingi huwapa watu misukumo ya kumsifu Bwana katika njia za ubunifu. Ikiwa unahisi msukumo wa kuonyesha unyenyekevu wako kupitia muziki, mashairi, sanaa za maonyesho, au njia nyingine, tenda kufuata hisia hizo. Zingatia kushiriki kile ulichobuni ili kuwasaidia wengine kujenga imani katika Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo.

Picha
Yesu akiwa amembeba mwanakondoo mabegani

Mchungaji Mwema, na Ken Spencer

Chapisha