Agano la Kale 2022
Agosti 8–14. Zaburi 1–2; 8; 19–33; 40; 46: “Bwana Ndiye Mchungaji Wangu”


“Agosti 8–14. Zaburi 1–2; 8; 19–33; 40; 46: ‘Bwana Ndiye Mchungaji Wangu’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Agano la Kale 2022 (2021)

“Agosti 8–14. Zaburi 1–2; 8; 19–33; 40,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2022

Picha
Yesu akitembea na kondoo

Bwana Ndiye Mchungaji Wangu, na Yongsung Kim, havenlight.com

Agosti 8–14

Zaburi 1–2; 8; 19–33; 4046

“Bwana Ndiye Mchungaji Wangu”

Muhtasari huu unapendekeza baadhi ya vifungu vizuri vya maandishi katika Zaburi ambavyo vitawabariki watoto, lakini usisikie kuzuiwa nazo. Fuata mwongozo wa Roho.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Siku chache mapema, waalike watoto wachache walete darasani michoro inayowakilisha vitu ambavyo wao na familia zao walivisoma kuhusu katika Zaburi wiki hii, kama vile mchungaji (ona Zaburi 23:1), kikombe (ona Zaburi 23:5), au moyo (ona Zaburi 24:4). Waalike watoto wazungumzie kuhusu michoro yao na mstari kutoka katika Zaburi ambayo inavitaja.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

Zaburi 19:1; 33:5

“Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu.”

Zaburi 19 na 33 inafundisha kwamba tunaweza kupata ushahidi wa utukufu na wema wa Mungu ukituzunguka kote kupitia uumbaji Wake mzuri. Wasaidie watoto kujifunza kuuona mkono wa Mungu katika dunia inayowazunguka wao.

Shughuli Yamkini

  • Waonyeshe watoto baadhi ya picha za vitu vizuri ambavyo Mungu ameviumba, au tazameni nje ya dirisha pamoja kuona vitu hivi. Waulize watoto kile wanachopenda kuhusu uumbaji wa Baba wa Mbinguni. Soma ama Zaburi 19:1 au 33:5, na waulize watoto jinsi wanavyohisi kuhusu Baba wa Mbinguni wanapoona uumbaji Wake.

  • Imbeni pamoja wimbo kuhusu uumbaji wa Mungu, kama vile “The World Is So Lovely” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 233). Waalike watoto wachague kitu fulani ambacho Mungu alikiumba (kama vile vilivyotajwa katika wimbo) na wachore picha yake ili kushiriki na familia zao.

Zaburi 23

“Bwana ndiye Mchungaji Wangu.”

Kama watoto wanaweza kujifunza katika umri mdogo kwamba Bwana ndiye mchungaji wao, watakuwa na uwezekano wa kumfuata Yeye “katika njia za haki.”

Shughuli Yamkini

  • Mpe kila mtoto nakala ya ukurasa wa shughuli ya wiki hii, au mpe kila mmoja wao picha kutoka kwa ukurasa wa shughuli. Waalike wasikilize unaposoma Zaburi 23. Waombe watoto waonyeshe au wanyanyue juu picha wanaposikia ikitajwa katika zaburi. Toa ushuhuda wako kwamba Yesu anatujali, kama vile mchungaji anavyowajali kondoo wake.

  • Waambie watoto baadhi ya njia ambazo unazijua kwamba Mwokozi anakupenda. Waalike watoto wasimame mmoja kwa wakati na kushiriki baadhi ya njia wanazozijua kwamba Yesu anawapenda. Imbeni pamoja wimbo ambao unaweza kuwapa mawazo, kama vile “I Feel My Savior’s Love” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 74–75).

Zaburi 30:5

Yesu Kristo anaweza kugeuza huzuni kuwa furaha.

Tafakari jinsi utakavyoweza kuwasaidia watoto kupata ushahidi wao wenyewe wa shangwe ambayo Yesu Kristo hutupatia tunapokuwa na huzuni.

Shughuli Yamkini

  • Waalike watoto wajifanye wanalia wakati unasoma kutoka katika Zaburi 30:5, “Kilio kinaweza kudumu kwa usiku.” Kisha waambie wawe na furaha unaposoma, “Lakini asubuhi huwa furaha.” Rudia kifungu hiki cha maneno mara chache, na ushuhudie kwa watoto kwamba kwa sababu ya Yesu Kristo, huzuni tunayohisi katika maisha haya inaweza kubadilishwa kwa furaha.

  • Onyesha picha ya Mwokozi, na waambie watoto kuhusu baadhi ya vitu ambavyo Yeye amevifanya kwa ajili yako ambavyo hukuletea furaha. Mpe kila mtoto nafasi ya kunyanyua picha na kushiriki kile Yesu amefanya ambacho huwaletea furaha.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

Zaburi 23; 27–28; 3246

Bwana ananipa amani, nguvu na mwongozo.

Nyingi za Zaburi hushuhudia baraka za Bwana katika maisha yetu. Unaweza kutumia Zaburi kuwasaidia watoto kujifunza kumtumaini na kumgeukia.

Shughuli Yamkini

  • Andika ubaoni Bwana ndiye . Waache watoto wachague moja ua zaidi ya maandiko yafuatayo na kusoma: Zaburi 23:1; 27:1; 28:1; 28:7; 32:7; 46:1. Waombe wakamilishe sentensi kwenye ubao wakitumia kile wanachojifunza kutoka kwenye maandiko yao. Wasaidie watoto kujadili kile hizi ishara zinatufundisha kuhusu Bwana.

  • Waonyeshe watoto picha ya mwanakondoo. Waombe wataje baadhi ya vitu ambavyo mwanakondoo huhitaji ili kuwa salama na mwenye afya, na wahimize kutafuta mawazo katika Zaburi 23:1–4. Kisha onyeshe picha ya mtoto. Tunahitajika nini tuwe salama kiroho na wenye afya? Someni pamoja Zaburi 23, na waulize watoto jinsi vitu mchungaji anavyofanya katika zaburi vinaweza kulinganishwa na kile Yesu Kristo anachotufanyia sisi.

Picha
Hekalu la Concepción Chile

Ni lazima tuwe wasafi kiroho na wasio na doa ili kuingia katika uwepo wa Bwana.

Zaburi 24:3–4

Ili kuingia hekaluni, tunahitaji “mikono safi na moyo mweupe.”

Wakati watoto wanapotazamia kuingia hekaluni siku moja, wasaidie kuelewa kwamba wanaweza kujiandaa kuwa safi kiroho kupitia Upatanisho wa Mwokozi.

Shughuli Yamkini

  • Waonyeshe watoto picha ya hekalu. Waalike wasome Zaburi 24:3 na watafute maneno yanayowakumbusha juu ya hekalu. Kisha someni pamoja mstari wa 4 ili kujifunza nani anaweza kuingia hekaluni (fafanua maneno wasiyoyajua). Ni kwa jinsi gani mikono yetu inapata uchafu kimwili? Ni kwa jinsi gani mikono na mioyo hupata uchafu kiroho? Ni kwa jinsi gani tunasafisha mikono yetu kimwili? Je, ni kwa jinsi gani, Mwokozi anatusaidia kusafisha mikono na mioyo yetu kiroho? (Kama inasaidia, eleza kwamba “mikono” katika mstari huu inaweza kuwakilisha matendo yetu na “mioyo” inaweza kuwakilisha tamaa zetu.)

  • Rejelea pamoja na watoto mahitaji ya kupata kibali cha hekalu (ona Russell M. Nelson, “Maneno ya Kutamatisha,” Liahona, Nov. 2019, 120–22; au mwalike mshiriki wa uaskofu kujadili mahitaji haya pamoja na darasa). Waalike watoto wachague kitu kimoja wanachohisi kinawapa mwongozo wa kujiandaa kuwa wastahiki kuingia katika hekalu.

Zaburi 46:10

“Acheni, mjue kuwa Mimi ni Mungu.”

Kuchukua muda wa kuwa mnyenyekevu na kutulia, licha ya shughuli nyingi tulizonazo, kunaweza kujenga ushuhuda wetu kwamba Mungu yu hai.

Shughuli Yamkini

  • Wasaidie watoto kukariri mstari wa kwanza kutoka katika Zaburi 46:10: “Acheni, mjue kuwa Mimi ni Mungu.” Zungumza nao kuhusu kile “acheni,” vyote kimwili na kiakili inachoweza kumaanisha. Shiriki na watoto uzoefu ambao kuwa “tuli” kuliimarisha ushuhuda wako wa Baba wa Mbinguni. Waombe watoto washiriki uzoefu wowote waliokuwa nao. Kwa nini kutulia ni njia muhimu ya kujua kwamba Mungu yu hai?

  • Waalike watoto warejelee pamoja nawe kile wanachofanya wakati wa siku ya kawaida. Wasaidie kufikiria muda wakati wa siku yao ambapo wangeweza kujaribu “kutulia” na kuhisi kuwa karibu na Baba wa Mbinguni. Wahimize waweke lengo la kutumia muda kama huo wakati wa wiki inayokuja ili kuimarisha ushuhuda wao wa Baba wa Mbinguni.

  • Waalike watoto waorodheshe baadhi ya vitu tunavyoweza kufanya ili kujua kwa ajili yetu wenyewe kwamba Baba wa Mbinguni ni halisi na kwamba Yeye anatupenda. Waalike wachague kitu fulani kutoka kwenye orodha ambacho wanataka kufanya.

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Waalike watoto wachague mstari wanaoupenda kutoka katika zaburi ambao wameuzungumzia leo. Wahimize washiriki mstari huo pamoja na mwanafamilia au rafiki.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Zingatia mahitaji ya watoto. Kama mwalimu, una nafasi ya kipekee ya kuelewa mahitaji ya wale unaowafundisha. Uzoefu wako, mazoea yako na watoto, na mwongozo wa Roho utakusaidia wewe kujua ni shughuli gani za kujifunza ambazo zina uwezekano wa kujenga imani yao katika Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo.

Chapisha