Agano la Kale 2022
Agosti 22–28. Zaburi 102–103; 110; 116–119; 127–128; 135–139; 146–150: “Kila Mwenye Pumzi na Amsifu Bwana”


“Agosti 22–28. Zaburi 102–103; 110; 116–119; 127–128; 135–139; 146–150: ‘Kila Mwenye Pumzi na Amsifu Bwana,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Agano la Kale 2022 (2021)

“Agosti 22–28. Zaburi 102–103; 110; 116–119; 127–128; 135–139; 146–150,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2022

Picha
Kristo kwenye joho jekundu akizungukwa na watu waliopiga magoti

Kila Goti Litapigwa, na J. Kirk Richards

Agosti 22–28

Zaburi 102–103; 110; 116–119; 127–128; 135–139; 146–150

“Kila Mwenye Pumzi na Amsifu Bwana.”

Kama utahitaji mawazo ya ziada unapojiandaa kufundisha, ona “Nyenzo za Ziada kwa ajili ya Kufundisha Watoto” na “Kukidhi Mahitaji ya Watoto Wadogo” mwanzoni mwa muhtasari huu.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Onyesha baadhi ya picha zilizopo kwenye muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia, na waalike watoto wazungumze kuhusu kile wanachoona katika picha. Wasaidie kuona miunganiko kati ya picha hizi na kile wanachojifunza katika kitabu cha Zaburi.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

Zaburi 119:105

Neno la Mungu ni kama nuru.

Watoto unaowafundisha wako katika njia ya kurudi kwa Baba wa Mbinguni. Neno la Mungu linaweza kuwasaidia kuwaweka katika njia hiyo sasa na katika maisha yao yote.

Shughuli Yamkini

  • Onyesha picha ya vitu vilivyotajwa katika Zaburi 119:105, na uwaalike watoto kuweka picha katika mpangilio wakati unaposoma mstari huu. Waombe watoto warudie vifungu vya maneno kutoka katika mstari huu pamoja nawe wakati ukionyesha picha.

  • Waombe watoto kuzungumza kuhusu vile wanavyohisi wakiwa gizani. Ni mambo gani ambayo ni magumu kufanya gizani? Unaweza kumwalika mtoto ajaribu kufanya kitu wakiwa wamefumba macho yao, kama vile kuchora picha. Kwa nini mambo haya ni rahisi sana kufanya wakati kuna nuru? Wasaidie watoto kuelewa jinsi neno la Mungu, kama linavyopatikana katika maandiko na maneno ya manabii wanaoishi, huangaza njia yetu kurudi kwa Baba wa Mbinguni.

Zaburi 139:1–3, 23

Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wananijua na wanipenda.

Kote katika maisha yetu, tunahitaji kukumbushwa kwamba Baba wa Mbinguni na Yesu wanatujua kibinafsi. Zaburi 139 inaweza kukusaidia kuwafundisha watoto kwamba Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wanawajua wao na kuwapenda.

Shughuli Yamkini

  • Tengeneza orodha fupi ya mambo unayoyajua kuhusu kila mtoto. Unapoisoma orodha ya kila mmoja kwa wakati, waombe watoto wabashiri ni nani unamuongelea. Soma Zaburi 139:1–3, na uwasaidie watoto kuelewa maneno ambayo wasioweza kuyajua. Shuhudia kwamba Baba wa Mbinguni na Yesu wanawajua wao vyema sana—Wanajua majina yao, kile kinachowafanya wawe na furaha na huzuni, na mambo wanayofanya vyema.

  • Soma Zaburi 139:23, na waalike watoto waweke mikono yao juu ya mioyo yao unaposema neno “moyo” na waguse vichwa vyao unaposema “fikra.” Shiriki hadithi ya wakati ulipohisi Mungu alijua moyo wako na fikra zako.

Zaburi 146:1, 5–9

Ninaweza kumsifu Bwana.

Kumsifu Bwana humaanisha kuonyesha shukrani zetu na upendo kwa ajili Yake. Wasaidie watoto kujifunza kwamba tunamsifu Yeye tunapofanya mambo kama vile kuimba, kuomba, na kutii mafundisho Yake.

Shughuli Yamkini

  • Waalike watoto washiriki uzoefu wa wakati mtu fulani alipowasifu au kuwaambia walifanya kazi nzuri. Shiriki baadhi ya mambo mazuri kutoka katika Zaburi 146:6–9 ambayo Bwana ametenda, na uwaalike watoto wasimulie mambo mengine ambayo Yeye anatutendea. Wasaidie kufikiria juu ya njia wanazoweza kumsifu Yeye kwa ajili ya mambo hayo.

  • Imbeni pamoja wimbo wa kusifu, kama vile “Beauty Everywhere” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 232). Elezea kwamba kwa Waisraeli hapo kale, Zaburi zilikuwa kama nyimbo tunazoimba leo ili kumwabudu na kumsifu Mungu.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

Zaburi 102:1–2103

Bwana hunipa faraja na tumaini.

Mungu anajua majaribu yetu na huzuni, na Yeye anataka kutufariji na kututia moyo. Wasaidie watoto kujenga imani yao Kwake ili waweze kumgeukia Yeye katika nyakati za mahitaji.

Picha
Yesu akiponya

Uponyaji, na J. Kirk Richards

Shughuli Yamkini

  • Muombe mmojawapo wa watoto asome Zaburi 102:1–2. Je, ni kwa jinsi gani Bwana anaweza kutusaidia katika nyakati zetu za shida? Je, ni kwa jinsi gani tunaomba msaada Wake? Shiriki uzoefu ambapo ulihisi kwamba Mungu alisikia maombi yako wakati ulikuwa na mahitaji, na uwaalike watoto kushiriki uzoefu wao na shuhuda zao.

  • Waalike watoto watafute maneno ya faraja na tumaini katika Zaburi 103. Je, ni kwa jinsi gani maneno haya yangewasaidia watu wanaokabiliwa na changamoto? Wahimize watoto waandike vifungu vya maneno walivyoviona vina maana kwao ili kuwakumbusha kwamba Bwana anaweza kuwasaidia wakati wanapitia majaribu.

Zaburi 119:105

Neno la Mungu hunisaidia kufuata njia Yake.

Ingawa ulimwengu unaweza kuonekana giza wakati mwingine, neno la Mungu linaweza kuangaza njia yetu na kutusaidia kurudi Kwake.

Shughuli Yamkini

  • Chora picha ya nuru ubaoni (kama vile taa) na picha ya maandiko. Waalike watoto wasome Zaburi 119:105. Nuru inatusaidiaje sisi? Neno la Mungu linatusaidiaje sisi? Waombe watoto waandike majibu yao ubaoni karibu na picha. Ni kwa jinsi gani neno la Mungu ni kama nuru? Ni kwa jinsi gani linatusaidia kukaa kwenye njia ambayo huongoza kurudi kwa Baba wa Mbinguni?

  • Wagawe watoto katika jozi, na ipe kila jozi mojawapo ya vifungu vya maandiko vifuatavyo: Zaburi 119:47–48; Zaburi 119:105; 1 Nefi 11:25; 2 Nefi 31:20. Waalike wasome vifungu na kutafuta kile Baba wa Mbinguni ametupatia ili kutusaidia kukaa katika njia ya kurudi Kwake. Waalike watoto kutafakari na kushiriki kile wanachohisi kuvutiwa kufanya kwa sababu ya kile walichojifunza.

  • Imbeni wimbo kwa pamoja kuhusu kufuata njia ya Mungu, kama vile “I Will Walk with Jesus” (ChurchofJesusChrist.org). Tunajifunza nini kutoka kwenye wimbo huu kuhusu jinsi ya kukaa katika njia sahihi?

Zaburi 139:23–24

Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wanaweza kunisaidia kujua jinsi ya kuwa bora.

Zaburi 139 hutufundisha kwamba Mungu anajua kila kitu kutuhusu sisi, ikiwa ni pamoja na uimara na udhaifu wetu. Kama tukimgeukia Yeye, anaweza kutufundisha kile tunachohitaji kufanya ili kuwa zaidi kama Yeye.

Shughuli Yamkini

  • Andika maneno ya Zaburi 139:23–24 ubaoni, na uwaalike watoto kupigia mstari maneno ambayo yanaelezea mambo ambayo Mungu anaweza kufanya kwa ajili yetu. Kwa nini tungependa Mungu afanye mambo haya? Ni kwa jinsi gani tunaweza kumwalika Yeye “atuongoze [sisi] katika njia ya milele”?

  • Wahimize watoto “wakague” maisha yao wenyewe ili kutafuta njia wanazoweza kuwa bora katika maeneo manne ya kuzingatia katika programu ya Watoto na Vijana—kiroho, kijamii, kimwili, na kiakili. Wakumbushe kwamba Bwana anajua jinsi wanavyoweza kuwa bora katika kila mojawapo ya maeneo haya, na wahimize kutafute mwongozo Wake.

  • Imbeni wimbo kuhusu jinsi Baba wa Mbinguni anaweza kutusaidia kuboreka, kama vile mstari wa pili wa “Help Me, Dear Father” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 99). Shiriki jinsi Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wamekusaidia wewe kuwa bora.

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Mara moja moja, unaweza kumwalika mmojawapo wa watoto na mmojawapo wa wanafamilia kushiriki pamoja na darasa kile wanachofanya ili kujifunza injili nyumbani. Wahimize watoto wengine kushiriki mawazo haya na familia zao.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Tumia muziki. Nyimbo za msingi na nyimbo za Kanisa zinaweza kuwasaidia watoto kuelewa na kutunza kweli za injili katika njia isiyosahaulika. Kuimba pia kunaweza kuwafanya watoto kuwa wachangamfu katika kujifunza. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 22.)

Chapisha