Agano la Kale 2022
Agosti 29–Septemba4: Mithali 1–4; 15–16; 22; 31; Mhubiri 1–3; 11–12: “Kumcha Bwana Ni Chanzo cha Maarifa”


“Agosti 29–Septemba 4: Mithali 1–4; 15–16; 22; 31; Mhubiri 1–3; 11–12: ‘Kumcha Bwana Ni Chanzo cha Maarifa,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Agano la Kale 2022 (2021)

“Agosti 29–Septemba 4: Mithali 1–4; 15–16; 22; 31; Mhubiri 1–3; 11–12,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2022

Picha
mwanamume akisoma maandiko

Agosti 29–Septemba4

Mithali 1–4; 15–16; 22; 31; Mhubiri 1–3; 11–12

“Kumcha Bwana Ni Chanzo cha Maarifa”

Unaposoma Mithali na Mhubiri, wafikirie watoto unaowafundisha. Ni ujumbe gani kutoka kwenye maandiko haya unaweza kuwasaidia wao wajione wako karibu zaidi na Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo?

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Chora ubaoni picha za vitu ambavyo vimetajwa katika kitabu cha Mithali, kama vile moyo, nuru au njia. Wasaidie watoto kusoma Mithali 3:5; 4:18,26, na waalike kushiriki kile walichojifunza kuhusu vitu hivi kutoka kwenye maandiko.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

Mithali 3:5

Ninaweza kutumaini katika Bwana kwa moyo wangu wote.

Tunapomtumaini Bwana kwa mioyo yetu yote, tunakuwa na imani Kwake na kujua kwamba Yeye atatusaidia.

Shughuli Yamkini

  • Mruhusu mmoja wa watoto ashikilie picha ya Mwokozi wakati unaposoma Mithali 3:5. Waambie watoto kumtumaini Bwana kuna maana gani kwako. Waalike watoto watengeneze moyo kwa mikono yao au kuweka mikono yao kwenye mioyo yao wakati wakirudia kirai “mtumaini Bwana kwa moyo wako wote” mara kadhaa.

  • Chora moyo mkubwa ubaoni na wasaidie watoto wafikirie vitu wanavyoweza kufanya ili kuonesha kwamba wanamtumaini Bwana. Waalike wachore mawazo yao ndani ya moyo au juu ya kipande cha karatasi. Wahimize kushiriki mawazo yao pamoja na familia zao.

Picha
watoto wawili wakizungumza

Watoto wanaweza kutoa “jawabu la upole” kwa kutumia maneno ya ukarimu (Mithali 15:1).

Mithali 15:1,18

Ninaweza kutumia maneno ya ukarimu.

Katika hali ya wasiwasi au kukata tamaa, tunaweza kujaribiwa kujibu kwa hasira. Mithali 15:1,18 inatufundisha jinsi tunavyoweza kugeuza hasira.

Shughuli Yamkini

  • Soma Mithali 15:1 kwa watoto, na elezea maneno au virai vyoyote ambavyo havijulikani kwao. Shiriki mifano michache ya hali ambazo kwazo mtoto anaweza kuhisi hasira (kama vile mabishano na kaka au dada). Wasaidie kufikiria “jawabu la upole,” au maneno ya ukarimu, wanayoweza kutumia badala ya maneno ya hasira. Wasaidie wafanye mazoezi kusema vitu hivi kwa upole au kwa sauti ya utulivu.

  • Imbeni wimbo kuhusu ukarimu, kama vile “Kindness Begins with Me” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto,145). Wimbo huu unatufundisha nini kuhusu kuwa wakarimu?

  • Kuwasaidia watoto kuelewa kile inachomaanisha “kutokuwa mwepesi wa hasira” (Mithali 15:18), simulia hadithi binafsi kuhusu wakati wewe (au mtu fulani unayemjua) alipohisi hasira lakini akachagua kuwa mkarimu. Acha watoto washiriki uzoefu wao pia. Wasaidie watoto wafikirie juu ya mambo wanayoweza kufanya badala ya kuwa na hasira. Kwa mfano, wanaweza kumfikiria Yesu, kumwomba Baba wa Mbinguni msaada, kuimba wimbo wa Msingi, au, ikiwa inawezekana, kuondoka tu.

Mithali 22:9

Ninaweza kushiriki vitu nilivyo navyo pamoja na wengine.

Watoto wadogo wanaweza kujifunza kusaidia watu walio karibu nao ambao wana mahitaji. Ni kwa jinsi gani unaweza kuwashawishi ili washiriki kitu walichonacho pamoja na wengine?

Shughuli Yamkini

  • Waoneshe watoto picha kadhaa za wengine wakitumikia au wakiwasaidia watu wenye mahitaji, ikiwa ni pamoja na picha ya Mwokozi (kama vile Kitabu cha Sanaa ya Injili, na. 42, 44,46). Waombe watoto wakuambie nini kinatokea katika kila picha. Wasomee watoto Mithali 22:9. Eleza kwamba njia mojawapo tunayoweza kutumikia ni kwa kutoa “chakula kwa masikini,” lakini kuna njia nyingine nyingi za kuwasaidia wale walio na mahitaji. Waalike watoto wachore picha zao wenyewe wakimsaidia mtu fulani.

  • Leta vitu kadhaa darasani ambavyo unaweza kushiriki na watoto, kama vile picha au rangi za kuchorea. Unapogawa moja kwa kila mtoto, sema, “nitashiriki na [jina la mtoto].” Acha watoto wafanye zamu kushiriki vitu pamoja na wengine. Ni vitu gani vingine tunaweza kushiriki na wengine?

  • Imbeni pamoja wimbo kuhusu huduma, kama vile “‘Give,’ Said the Little Stream” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 236). Au onesha video “Gordon Hinckley: Masomo Niliyojifunza kama Mvulana” (ChurchofJesusChrist.org). Waulize watoto jinsi wanavyohisi wakati wanapowasaidia wengine.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

Mithali 1:7; 2:5; 15:33; 16:6; Mhubiri 12:13

“Kumcha Mungu” humaanisha kumpenda na kumtii Yeye.

Moja ya jumbe za muhimu katika Mithali na Mhubiri ni “kumcha Mungu, na kutii amri zake” (Mhubiri 12:13). Tafakari jinsi unavyoweza kuwasaidia watoto waelewe inamaanisha nini kumcha Mungu.

Shughuli Yamkini

  • Waalike watoto waorodheshe baadhi ya vitu ambavyo watu wanaweza kuogopa. Kisha waombe wasome Mithali 1:7 na Mhubiri 12:13. Inamaanisha nini kumcha Mungu? Ili kusaidia kujibu swali hili, muombe mtoto asome tena mistari, akibadilisha neno “kumcha” kwa neno “unyenyekevu.” Rudia shughulu hii kwa maneno kama “upendo,” “utiifu,” au “tii.” Ni kwa jinsi gani hii hubadili uelewa wetu wa kile inachomaanisha kumcha Mungu?

  • Mwalike kila mtoto achague moja ya mistari ifuatayo ili kusoma, akitafuta neno “kumcha”: Mithali 1:7; 2:5; 15:33; 16:6. Waombe watoto kushiriki kile mstari wao unachofundisha kuhusu baraka zinazokuja wakati tunapomcha Bwana, ambayo humaanisha kwamba tunaonesha unyenyekevu na heshima Kwake (ona pia Mithali 14:26–27). Je, tunamwonyeshaje Bwana kwamba tunampenda na kumheshimu Yeye?

Mithali 3:5–7

“Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote.”

  • Someni pamoja Mithali 3:5–7, na waalike watoto waorodheshe mambo ambayo mistari hii inasema tunapaswa kufanya na ambayo hatupaswi kufanya. Waulize wanachohisi kuhusu ni kitu gani kila moja ya mambo haya inamaanisha. Je, sifa zipi tunazipata kwa watu tunaowatumaini? Je, ni sifa zipi Bwana anazo ambazo zinatusaidia sisi kumtumaini Yeye?

  • Ili kuonesha kile inachomaanisha “kutozitegemea akili zako mwenyewe,” waruhusu watoto wajaribu kuegemeza fimbo au penseli dhidi ya vitu mbalimbali, kama vile kitabu au kipande cha karatasi. Ni vitu gani vimefanya vizuri? Kwa nini ni muhimu “kumtumaini Bwana” na kutozitegemea “akili zetu wenyewe“?

Methali 15:1,18; 16:32

“Jawabu la upole hugeuza hasira.”

Kuzungumza kwa hasira mara nyingi hufanya hata hali ya wasiwasi kuwa mbaya zaidi. Mistari hii inafundisha kwamba maneno yetu na mitazamo yetu vinaweza kugeuza ghadhabu au hasira.

Shughuli Yamkini

  • Andika maneno ghadhabu na ugomvi ubaoni, na shiriki mfano wa mabishano ambayo watoto wanaweza kuwa nayo. Kisha waombe watoto wasome Mithali 15:1,18; 16:32 na kutafuta ushauri wanaoweza kuwapa watoto ambao wanabishana. Kila mara watoto wanaposhiriki wazo, waalike wafute sehemu ya maneno ubaoni. Waalike kubadilisha maneno hayo kwa mengine yanayoelezea sifa kama za Kristo ambazo huleta amani.

  • Wasaidie watoto kufikiria matukio katika maandiko ambapo Mwokozi alionesha mfano wa kile alichofundisha katika Mithali 15:1,18; 16:32. Kwa mawazo, wanaweza kutazama katika Yohana 8:1–11; 18:1–11. Imbeni pamoja wimbo kuhusu Mwokozi, kama vile “I’m Trying to Be like Jesus” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 78–79). Ni jinsi gani tunaweza kufuata mfano wa Yesu Kristo wakati tunapochangamana na wanafamilia, marafiki na wengine?

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Wasaidie watoto wachague mstari waliosoma darasani ambao waliupenda. Wahimize kushiriki mstari huo pamoja na familia zao na wawaambie kile walichojifunza kutoka kwenye mstari huo.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Jiboreshe na uwe mwalimu kama Kristo. Tafakari jinsi unavyoweza kuongeza uwezo wako wa kuwasaidia watoto kujenga imani yao kwa Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo. Maswali ya kujitathmini mwenyewe kwenye ukurasa wa 37 wa Kufundisha katika Njia ya Mwokozi yanaweza kusaidia.

Chapisha