Agano la Kale 2022
Oktoba 31–Novemba 6. Danieli 1–6: “Hakuna Mungu Mwingine Awezaye Kuokoa”


“Oktoba 31–Novemba 6. Danieli 1–6: ‘Hakuna Mungu Mwingine Awezaye Kuokoa,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano la Kale 2022 (2021)

“Oktoba 31–Novemba 6. Danieli 1–16,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2022

Picha
Danieli akitafsiri ndoto ya mfalme

Danieli Anatafsiri Ndoto ya Nebukadreza, na Grant Romney Clawson

Oktoba 31–Novemba 6

Danieli 1–6

“Hakuna Mungu Mwingine Awezaye Kuokoa”

Washiriki wengi wa darasa watakuwa wanafahamu baadhi ya hadithi zilizoko katika kitabu cha Danieli. Unapojifunza na kujiandaa kufundisha, tafuta mwongozo kutoka kwa Roho kuhusu jinsi unavyoweza kuwasaidia washiriki wa darasa kupata maana binafsi kutoka katika sura hizi.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Inaweza kuwa msaada kwa washiriki wa darasa kuelezea jinsi kujifunza kwao injili kibinafsi na kifamilia kunavyoendelea. Wakati washiriki wa darasa wanaposhiriki umaizi kuhusu kitu ambacho Roho amewafundisha wiki hii, unaweza kuwauliza kile walichokuwa wakifanya wakati wakijifunza ambacho kiliwaongoza kwenye umaizi huo.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Danieli 1; 3; 6

Tunaweza kumtumaini Bwana wakati imani yetu inapojaribiwa.

  • Kuanza mjadala kuhusu jinsi Danieli, Shadraka, Meshaki, na Abednego walivyoonyesha imani katika Bwana, unaweza kuwaomba washiriki wa darasa wachache kufanya muhtasari wa changamoto ambazo wanaume hawa wanne walikabiliana nazo, zilizoelezewa katika Danieli 1, 3, na6. Kwa nini ingeweza kuwa vigumu kuwa waaminifu katika hizi hali? Ni hali gani mnazokabiliana nazo ambazo huijaribu imani yetu? Washiriki wa darasa wangeweza kupekua Danieli 1:10–13; 3:15–18; 6:10, kutafuta jinsi hawa wanaume wanne walivyojibu changamoto zao. Je, ni kwa jinsi gani mifano yao inaweza kutusaidia katika jitihada zetu za kuwa wanafunzi waaminifu wa Yesu Kristo?

  • Wengi wetu, kama vile Danieli na rafiki zake, tunahisi shinikizo la kushusha viwango vyetu. Nini baadhi ya vyanzo vya shinikizo hili maishani mwetu? Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kujifunza kutokana na mfano wa Danieli na rafiki zake, unaweza kugawa darasa katika makundi matatu na kupangia kila kundi kupitia mojawapo ya sura zifuatazo: Danieli 1, 3, au6. Ni kwa jinsi gani Bwana aliwabariki Danieli, Shadraka, Meshaki, na Abednego wakati walipochagua kuwa waaminifu licha ya shinikizo walilokabiliana nalo? Kila kundi lingeweza kushiriki pamoja na darasa kile walichogundua. Washiriki wa darasa wanaweza kisha kushauriana pamoja kuhusu jinsi ya kubaki waaminifu licha ya shinikizo la kijamii au aina nyingine ya shinikizo. Wanaweza pia kujadili umuhimu wa kutafuta marafiki wema ambao watatusaidia katika viwango vyetu.

Danieli 2

Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho ni ufalme wa Mungu duniani.

  • Kujadili Danieli 2 kunaweza kuwasaidia washiriki wa darasa lako kuelewa jinsi Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho linavyotimiza hatima yake kama jiwe lililotolewa unabii “lililochongwa mlimani” (mstari wa 45). Kuanza, mnaweza kupitia kama darasa maelezo ya Danieli na tafsiri ya ndoto ya Nebukadreza, inayopatikana katika Danieli 2:31–45. Kisha unaweza kuonyesha picha ya jiwe (au uchore moja ubaoni). Waalike washiriki wa darasa kushiriki kile walichojifunza kuhusu ufalme wa Mungu kwa kuyalinganisha na maelezo ya jiwe katika Danieli 2:34–35, 44–45. Pengine washiriki wa darasa wanajua baadhi ya historia ya Kanisa katika eneo lenu ambayo wanaweza kuelezea. Ni kwa jinsi gani tumeuona unabii wa Danieli ukitimia katika maisha yetu binafsi?

Danieli 2:1–30

Kupokea ufunuo kunahitaji maandalizi ya kiroho.

  • Labda washiriki wa darasa wangeweza kufaidika kutokana na kujifunza jinsi Danieli alivyojiandaa mwenyewe kupokea ufunuo uliohitajika kuelezea na kutafsiri ndoto ya Nebukadreza. Unaweza kuanza kwa kuwaomba washiriki wa darasa kurejelea Danieli 2:1–15 na kisha kueleza jinsi ambavyo wangejisikia kama wangejikuta wenyewe katika hali ya Danieli. Waalike wapekue Danieli 2:16–18 ili kujifunza kile ambacho Danieli alifanya. Je, tunajifunza nini kutoka katika Danieli 1:17 kuhusu jinsi Mungu alivyomwandaa Danieli? Je, tunaweza kujifunza nini kutoka kwa Danieli ambacho kinaweza kutusaidia tunapotafuta ufunuo wa binafsi? Je, tunaweza kujifunza nini kutokana na maneno na vitendo vya Danieli baada ya kupokea msaada wa Bwana? (ona Danieli 2:20–30).

Picha
wavulana wanne mezani wakikataa nyama inayotolewa na mwanaume

Kielelezo cha Danieli na rafiki zake wakikataa chakula cha mfalme, na Brian Call

Danieli 3

Wakati matokeo hayana uhakika, tunaweza bado kuchagua imani.

  • Tukio hili la Shadraka, Meshaki, na Abednego linalopitikana katika Danieli 3 linaweza kuwasaidia washiriki wa darasa kuelewa zaidi kile ilichomaanisha kuwa na imani katika Yesu Kristo. Unaweza kuwaalika washirki wa darasa kufanya muhtasari wa changamoto Shadraka, Meshaki, na Abednego waliyokabiliana nayo (ona Danieli 3:1–12) na kujadili jinsi wanavyoweza kujibu (ona Danieli 3:13–18). Je, tunajifunza nini kuhusu imani kutokana na majibu ya wanaume hawa? Unaweza kuandika ubaoni virai Mungu wetu aweza… na Bali kama si hivyo… kutoka mstari wa 17–18. Washiriki wa darasa wanaweza kupendekeza jinsi wanavyoweza kujaza nafasi zilizo wazi kwa hali ambazo wangeweza kukabiliana nazo. Kwa mfano, wanaweza kupendekeza “Mungu aweza kujibu maswali yetu yote” na “Lakini kama si hivyo, kwa subira nitamtumaini Yeye.” Washiriki wa darasa wanaposhiriki mifano, wahimize kuzungumza kuhusu jinsi gani Mwokozi hutusaidia na kutuimarisha hata wakati sisi hatujui jinsi matokeo ya mambo yatavyokuwa.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Tumia ishara za kuonekana kwa macho. “Sanaa, ikiwa ni pamoja na picha, video, na maigizo, vinaweza kusaidia ushirikishwaji wa wanafunzi—hasa wale wanaojifunza kwa kuona—na tengeneza matukio ya kimaandiko kuwa ya kukumbukwa (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 22).

Chapisha