Agano la Kale 2022
Oktoba 24–30. Ezekieli 1–3; 33–34; 36–37; 47: “Nami Nitawapa Ninyi Moyo Mpya”


“Oktoba 24–30. Ezekieli 1–3; 33–34; 36–37; 47: ‘Nami Nitawapa Ninyi Moyo Mpya”,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano la Kale 2022 (2021)

“Oktoba 24–30. Ezekieli 1–3; 33–34; 36–37; 47,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2022

Picha
Yesu akiwaongoza kondoo

Njoo, Unifuate, na Scott Sumner

Oktoba 24–30

Ezekieli 1–3; 33–34; 36–37; 47

“Nami Nitawapa Ninyi Moyo Mpya”

Maneno ya Ezekieli yanahifadhiwa na Bwana kwa kusudi la hekima na yanaweza kuwabariki washiriki wa darasa lako. Tafakari hili unapojifunza maandishi ya Ezekieli wiki hii.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Watu ambao walimsikia Ezekieli waliona maneno yake yalikuwa ya ‘kupendeza” na “kufurahisha,” “lakini hawakuyatenda” (ona Ezekieli 33:30–33). Washiriki wa darasa pia wanaweza kushiriki kifungu walichokipata katika maandishi ya Ezekieli kilichowapa mwongozo wafanye kitu fulani.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Ezekieli 34

Bwana anatualika tuwalishe Kondoo Wake.

Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kupata maana ya kibinafsi katika Ezekieli 34, unaweza kuandika ubaoni hali ambazo wanaweza kukabiliwa nazo, kama vile kujiandaa kuhudumu misheni, kulea watoto, au kupokea kazi ya kutumikia. Washiriki wa darasa wanaweza kuchagua moja na kutafakari wanaposoma kimya kimya Ezekieli 34: 1–10. Waalike washiriki ni ushauri gani kulingana na mistari hii wanaoweza kutoa kwa mtu aliye katika hali waliochagua. Inamaanisha nini kujilisha wenyewe badala ya kondoo wa Bwana? Ni kwa jinsi gani wachungaji ni kama Mwokozi? (mstari wa 11–16).

Unaweza kuhisi kupata mwongozo wa kuuliza maswali ambayo yanawasaidia washiriki wa darasa kutafakari sitiari katika Ezekieli 34:11–31. Kwa mfano, ni nini kinaweza kuwakilisha “malisho mema” na “zizi jema” katika mstari wa 14? Ni nini tofauti kati ya kondoo “waliopotea” na “waliofukuzwa”? (mstari wa 16). Ni jinsi gani Mwokozi anawaokoa aina zote za kondoo? Washiriki wa darasa wanaweza kushiriki ishara zingine wanazoweza kupata katika hii mistari na kuzungumza kuhusu kitu ambacho hizi ishara zinawafundisha kuhusu Yesu Kristo.

Ezekieli 37

Bwana anawakusanya watu Wake na kuwapa maisha mapya.

  • Kusoma Ezekieli 37 na kufikiria kuhusu ahadi za Bwana kuhusu kukusanyika kwa Israeli kunaweza kutupa umaizi kuhusu kukusanya kunamaanisha nini na jinsi sisi tunavyoweza kushiriki katika hilo. Ili kuwasaidia kupata umaizi huu ungeweza kuandika kwenye ubao maswali kama Bwana anajaribu kutimiza nini kupitia ukusanyaji wa Israeli? Je, Yeye anatimizaje hilo? Unaweza kisha kuomba nusu ya darasa kusoma Ezekieli 37:1–14 na ile nusu nyingine kusoma Ezekieli 37:15–28 wanapotafuta umaizi hivi vifungu viwili vinaweza kutoa kwa maswali ubaoni. Inaweza kusaidia kueleza kwamba vijiti vya Yusufu na Yuda vilivyotajwa katika mstari wa 16–19 vinawakilisha Kitabu cha Mormoni na Biblia. Washiriki wa darasa wanaposhiriki majibu yao, wahimize kuzungumza kuhusu kazi yao katika kukusanywa kwa Israeli katika siku za mwisho.

Picha
jangwa na Bahari ya Chumvi

Ezekieli aliona ono la mto ukitiririka kutoka kwenye hekalu na kuponya Bahari ya Chumvi.

Ezekieli 47:1–12.

Hekalu huleta uponyaji wa kiroho.

  • Picha zinaweza kuwasaidia washiriki wa darasa kuelewa ono lililoelezewa katika Ezekieli 47:1–12. Kwa mfano, unaweza kuonesha picha ya hekalu, mto, jangwa, na Bahari ya Chumvi (ona picha katika muhtasari wa wiki hii katika Njoo Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia na picha za Biblia, na. 3, “Jangwa la Yudea”). Inaweza kusaidia kuelezea kwamba Bahari ya Chumvi ina chumvi nyingi sana kiasi kwamba samaki na mimea haiwezi kuishi ndani yake. Washiriki wa darasa wanaweza kusoma mstari wa 1–12 na kushiriki ni nini kinachowavutia wao kuhusu maji yaliyoelezwa katika ono (ona pia Ufunuo 22:1 na kauli katika “Nyenzo za Ziada”). Wanaweza pia kuchora picha za ono la Ezekieli. Je, maji ni ishara ya nini? Je, miti iliyoelezewa katika mstari wa 12 inawakilisha nini? Labda washiriki wa darasa wangeweza kushiriki jinsi hekalu na baraka zake zimewaletea maisha ya kiroho na uponyaji.

Picha
ikoni ya nyenzo za ziada

Nyenzo za Ziada

Baraka za hekalu zinaweza kutuponya.

Kurejelea maji yakitirirka kutoka hekaluni katika ono la Ezekieli (ona Ezekieli 47:1–12), Mzee Dale G. Renlund alisema:

“Sifa mbili za maji zinazostahili kukumbukwa. Kwanza, ingawa mto mdogo haukuwa na kijito, ulikua na kuwa mto mkubwa, ukawa mpana na wenye kina kirefu kadiri ulivyotiririka. Kitu kama hicho hutokea kwa baraka ambazo hutiririka kutoka hekaluni wakati watu binafsi wanapounganishwa kama familia. Makuzi ya maana hutokea kwenda nyuma na mbele kupitia vizazi wakati ibada za kuunganisha zinapounganisha familia pamoja.

“Pili, mto ulihuisha kila kitu ambacho ulikigusa. Baraka za hekaluni vile vile zina nguvu za kushangaza za kuponya. Baraka za hekalu zinaweza kuponya mioyo na maisha na familia” (“Historia ya Familia na Kazi ya hekalu: Kuunganisha na Uponyaji,” Ensign au Liahona, Mei 2018, 47–48; ona pia video “And the River Will Grow,” ChurchofJesusChrist.org).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Wasaidie wengine kumpokea Roho. Mara nyingine walimu wanaweza kujaribiwa kufikiria ya kwamba ni elimu yao au mbinu zao au tabia zao zinazowashawishi wale wanaowafundisha. … Kusudi lako kama mwalimu sio kuwasilisha somo linalovutia bali ni kuwasaidia wengine kupokea ushawishi wa Roho Mtakatifu” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 10).

Chapisha