Agano la Kale 2022
Oktoba 24–30. Ezekieli 1–3; 33–34; 36–37; 47: “Nitatia Roho Mpya ndani Yako”


“Oktoba 24–30. Ezekieli 1–3; 33–34; 36; 47 ‘Nitatia Roho Mpya ndani Yako,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano la Kale 2022 (2021)

“Oktoba 24–30. Ezekieli 1–3; 33–34; 36–37; 47,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2022

Picha
Yesu akiwaongoza kondoo

Njoo, Unifuate, na Scott Sumner

Oktoba 24–30

Ezekieli 1–3; 33–34; 36–37; 47

“Nitatia Roho Mpya ndani Yako”

Ezekieli alialikwa kwa mfano “kula” neno la Mungu—kujijaza nalo (ona Ezekieli 2:9–3:3, 10). Unawezaje kujazwa na neno la Mungu wiki hii?

Andika Misukumo Yako

Ezekieli alikuwa nabii uhamishoni. Pamoja na Waisraeli wengine, alikuwa amekamatwa na kupelekwa Babeli miaka kadhaa kabla ya Yerusalemu kuharibiwa kabisa. Huko Yerusalemu, Ezekieli angekuwa kuhani akihudumu hekaluni. Huko Babeli, alikuwa miongoni mwa “wale wafungwa,” na “alikaa pale walipoketi” (Ezekieli 3:15). mamia ya maili kutoka hekaluni na akiwa na tumaini dogo la kurudi kwenye nyumba pendwa ya Mungu. Ndipo siku moja Ezekieli akapata ono. Aliona “utukufu wa Bwana” (Ezekieli 1:28)—sio nyuma katika hekalu la Yerusalemu lakini huko Babeli miongoni mwa wahamishwa. Uovu huko Yerusalemu, alijifunza, ulikuwa mkubwa sana kwamba uwepo wa Mungu haukuwepo tena pale (ona Ezekieli 8–11; 33:21).

Jukumu moja la Ezekieli lilikuwa kuwaonya Waisraeli juu ya matokeo ya uasi wao—onyo ambalo kwa kiasi kikubwa halikusikilizwa. Lakini kulikuwa na zaidi kwenye ujumbe wa Ezekieli: alitabiri kwamba, licha ya mambo kuwa mabaya, kulikuwa na njia ya kurudi. Ikiwa watu wa Mungu wangekubali mwaliko wa “kusikia neno la Bwana” (Ezekieli 37:4), kile kilichokuwa kimekufa kingeweza kufufuliwa. “Moyo wa jiwe” unaweza kubadilishwa na “moyo mpya” (Ezekieli 36:26). “Nami] nitatia roho yangu ndani yenu,” Bwana aliwaambia, “nanyi mtaishi” (Ezekieli 37:14). Na katika siku za mwisho, Bwana angeanzisha hekalu jipya na Yerusalemu mpya, “na jina la mji huo tangu siku hiyo litakuwa hili, Bwana yupo hapa” (Ezekieli 48:35).

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

Ezekieli 1–3.

“Nawe utawaambia maneno yangu,”

Kusoma kuhusu wito wa huduma ya Ezekieli katika Ezekieli 1–3 inaweza kukuchochea ufikirie juu ya fursa ambazo Mungu amekupa “kuongea kwa maneno Yake” kwa wengine (Ezekieli 3:4). Katika Ezekieli 2–3, angalia maneno Yake ya kutia moyo na maelekezo kwa Ezekieli. Ingawa watu unaowahudumia labda sio waasi kama watu wa Ezekieli, fikiria jinsi maneno ya Mungu kwa Ezekieli yanavyoathiri jinsi unavyoona huduma yako Kanisani, nyumbani, na mahali pengine.

Ona pia Ezekieli 33:1–9; D.Todd Christofferson, “Sauti ya Onyo,” Ensign au Liahona, Mei 2017, 108–11.

Ezekieli 33:10–19.

Bwana anataka kusamehe.

“Ikiwa dhambi zetu … ziko juu yetu,” Waisraeli waliofungwa walishangaa, “jinsi gani tunapaswa kuishi wakati ule?” (Ezekieli 33:10). Kwa kujibu, Bwana aliwafundisha ukweli muhimu kuhusu toba na msamaha. Maswali haya yanaweza kukusaidia kutafakari kweli hizo:

Ezekieli 34

Bwana ananialika kuwalisha kondoo Wake.

Katika Ezekieli 34, Bwana anawaita viongozi wa watu Wake kama “wachungaji.” Unaposoma, fikiria nini cheo hiki kinapendekeza kwako juu ya maana ya kuwa kiongozi. Je! Ni “kondoo” gani ambao Bwana anataka uwalishe? Je! Unawezaje kufuata mfano aliouweka Mwokozi kama mchungaji wetu? (ona mstari wa 11–31).

Ona pia Yohana 21:15–17.

Picha
jangwa na Bahari ya Chumvi

Ezekieli aliona katika maono mto ukitiririka kutoka hekaluni na kuiponya Bahari ya Chumvi.

Ezekieli 37

Bwana anawakusanya watu Wake na kuwapa maisha mapya.

Kukusanyika kwa Israeli kumeonyeshwa katika Ezekieli 37 kupitia ishara mbili. Unaposoma juu ya ile ya kwanza—mifupa iliyokufa ikifufuliwa ((ona mstari wa 1–14)—tafakari kile unachojifunza kuhusu kukusanya Israeli pande zote mbili za pazia (ona pia Ezekieli 36:24–30).

Ishara ya pili (ona mstari wa 15–28) inajumuisha vijiti viwili, ambavyo wasomi wengi wanatafsiri kama bodi za mbao zilizounganishwa na bawaba. Fimbo ya Yuda inaweza kuwakilisha Biblia (kwa kuwa sehemu kubwa ya Biblia iliandikwa na uzao wa Yuda), na fimbo ya Joseph inaweza kuwakilisha Kitabu cha Mormoni ( maadamu familia ya Lehi ilikuwa uzao wa Yusufu wa Misri). Kwa kuzingatia hilo, mistari hii inakufundisha nini kuhusu jukumu la maandiko katika kukusanyika kwa Israeli? Ni nini 2 Nefi 3:11–13 (unabii kuhusu Joseph Smith na Kitabu cha Mormoni) huongeza katika uelewa wako?

Ona pia 2 Nefi 29:14; “The Book of Mormon Gathers Scattered Israel” (video, ChurchofJesusChrist.org).

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa Ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

Ezekieli 33:1–5.Ili kuelezea mistari hii, mwanafamilia mmoja anaweza kujifanya “mlinzi” kwa kutazama dirishani na kuwaambia wanafamilia wengine kinachotokea nje. Ni kwa jinsi gani nabii wetu aliyehai ni kama mlinzi kwetu?

Ezekieli 33:15–16.Mistari hii inatufundisha nini kuhusu msamaha tunaoweza kupata kupitia Yesu Kristo?

Ezekieli 36:26–27.Ionyeshe familia yako baadhi ya mawe unapojadili ina maana gani kuwa na “moyo mgumu.” Wacha wapendekeze maneno ambayo yanaelezea “moyo mpya” na “roho mpya” ambayo Mwokozi anatupa (ona Mosia 3:19; 5:2).

Ezekieli 37:15–28.Wanafamilia wanaweza kutafuta vijiti viwili na kuandika kwenye kimoja Kwa Yuda (Biblia) na kingine Kwa Joseph (Kitabu cha Mormoni) (ona mstari wa 16–19). Kisha wanaweza kushiriki hadithi au maandiko kutoka kwenye Biblia na Kitabu cha Mormoni ambayo yanawasaidia kujisikia karibu na Mwokozi na kuwa “watu [Wake]” (mstari wa 23).

Ezekieli 47:1–12.Mistari hii inaelezea maono ya Ezekieli ya maji yanayotiririka kutoka hekaluni na kuponya Bahari ya Chumvi—bahari yenye chumvi sana hata kwamba samaki na mimea hawawezi kuishi ndani yake. Watoto wanaweza kufurahia kuchora picha ya ono hili. Je! Maji yanayotiririka kutoka hekaluni yanaweza maanisha nini? (Ona video “And the River Will Grow,” ChurchofJesusChrist.org). Ni kwa jinsi gani hekalu linatusaidia kutuponya? (ona Ezekieli 47:8–9,11).

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “Dear to the Heart of the Shepherd,” Nyimbo za Kanisa, na. 221.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Usijaribu kumaliza kila kitu. Unaweza usiweze kuchunguza kila ukweli katika Ezekieli na familia yako. Tafuta mwongozo wa kiroho kuamua nini cha kuzingatia. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 7.)

Picha
kielelezo cha mto unaotiririka kutoka hekaluni

“Tazama, maji yalitoka chini ya kizingiti cha nyumba.… Na kila kitu kitaishi popote utakapofikilia mto huo” (Ezekieli 47:1,9). Picha iliyotumiwa chini ya leseni kutoka shutterstock.com.

Chapisha