Agano la Kale 2022
Oktoba 17–23. Yeremia 30–33; 36; Maombolezo 1; 3: “Nitageuza Masikitiko Yao Kuwa Furaha”


“Oktoba 17–23. Yeremia 30–33; 36; Maombolezo 1; 3: ‘Nitageuza Masikitiko Yao Kuwa Furaha,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano la Kale 2022 (2021)

“Oktoba 17–23. Yeremia 30-33; 36 Maombolezo 1:3,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2022

Picha
Sanamu ya Yeremia nabii

Kilio cha Yeremia Nabii, kutoka kwenye sanamu na Shule ya Nazarene

Oktoba 17–23

Yeremia 30–33; 36; Maombolezo 1; 3

“Nitageuza Masikitiko Yao Kuwa Furaha”

Unapoandika misukumo yako, fikiria jinsi kanuni katika Yeremia na Maombolezo zinazoshabihiana na vitu vingine ulivyojifunza katika Agano la Kale.

Andika Misukumo Yako

Wakati Bwana alipomwita Yeremia kwanza kuwa nabii, Alimwambia kwamba kazi yake itakuwa “kung’oa, na kubomoa” (Yeremia 1:10)—na katika Yerusalemu, kulikuwa na uovu mwingi wa kung’oa na kubomoa. Lakini hii ilikuwa ni sehemu tu ya utume wa Yeremia—aliitwa pia “kujenga, na kupanda” (Yeremia 1:10). Ni nini kinachoweza kujengwa au kupandwa katika magofu ya ukiwa yaliyoachwa na uasi wa Israeli? Vivyo hivyo, wakati dhambi au shida zimeacha maisha yetu kuwa magofu, tunawezaje kujenga na kupanda tena? Jibu liko katika “Tawi la haki” (Yeremia 33:15), Masiya aliyeahidiwa. Masiya huleta “agano jipya” (Yeremia 31:31)—hilo ambalo linahitaji zaidi ya kujitolea kijuujuu au sura ya nje ya kujitolea. Sheria yake lazima iwe “ndani yetu,” ikiandikwa “mioyoni mwetu.” Hivyo ndivyo inamaanisha kweli kwa Bwana “kuwa Mungu [wetu]” na sisi “kuwa watu [Wake]” (Yeremia 31:33). Ni mchakato wa maisha yote, na bado tutafanya makosa na yanasababisha kuomboleza mara kwa mara. Lakini tunapofanya hivyo, tuna ahadi hii kutoka kwa Bwana: “Nitageuza masikitiko yao kuwa furaha” (Yeremia 31:13).

Kwa ajili ya muhtasari wa Maombolezo, ona “Maombolezo, Kitabu cha” katika Mwongozo kwenye Maandiko (scriptures.ChurchofJesusChrist.org).

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa Ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

Yeremia 30–31; 33

Bwana atawatoa Israeli kutoka utumwani na kuwakusanya.

Katika Yeremia 30–31; 33 Bwana alikubali “maombolezo, na kulia kwa uchungu” (Yeremia 31:15) kwamba Waisraeli wangepata uzoefu wakati wanaenda utumwani. Hata hivyo, Naye alitoa maneno ya faraja na tumaini. Je! Unafikiri ni virai gani katika sura hizi ambavyo vingewapa Waisraeli faraja na tumaini? Je, Unapata ahadi gani kutoka kwa Bwana kwa watu Wake? Je, ni kwa jinsi gani ahadi hizi zinatumika kwako leo?

Yeremia 31:31–34; 32:37–42.

“Watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao.”

Ingawa Waisraeli walikuwa wamevunja agano lao na Bwana, Yeremia alitabiri kwamba Bwana ataanzisha tena “agano jipya” na “agano la milele” na watu Wake (Yeremia 31:33; 32:40). Agano jipya na la milele ni “utimilifu wa injili ya Yesu Kristo [ona Mafundisho na Maagano 66:2.]. Ni jipya kila wakati linafunuliwa upya kufuatia kipindi cha ukengeufu. Ni la milele kwa maana kwamba ni agano la Mungu na limekuwa likifurahiwa katika kila kipindi cha injili ambapo watu wamekuwa tayari kuipokea” (Mwongozo wa Maandiko, “Agano Jipya na la Milele,” scriptures.ChurchofJesusChrist.org; italiki imeongezwa).

Unaposoma Yeremia 31:31–34; 32:37–42, tafakari ina maana gani kwako kuwa sehemu ya watu wa agano wa Mungu. Ni kwa jinsi gani mistari hii inaathiri jinsi unavyoona mahusiano yako ya agano na Mungu? Inamaanisha nini kuwa na sheria Yake kuandikwa moyoni mwako? (ona Yeremia 31:33).

Ona pia Yeremia 24:7; Waebrania 8:6–12.

Picha
msichana akijifunza maandiko

Maandiko yanaweza kutuhamasisha kutubu na kumrudia Bwana.

Yeremia 36

Maandiko yana nguvu ya kunigeuza kutoka kwenye uovu.

Bwana alimwamuru Yeremia kurekodi unabii wake katika “kitabu” au hati ya kukunja, akielezea kwamba ikiwa watu wangesikia unabii huu, “Huenda … wapate kurudi, kila mtu akaiache njia yake mbaya; nami nikawasamehe uovu wao na dhambi yao” (Yeremia 36:2–3). Unaposoma Yeremia 36, fikiria akibainisha jinsi watu wafuatao walivyohisi juu ya unabii huu:

Bwana:

Yeremia:

Baruku:

Yehudi na Mfalme Yehoyakimu:

Elnathani, Delaya, na Gemaria:

Tafakari jinsi unavyohisi kuhusu maandiko na jukumu lake katika maisha yako. Jinsi gani yamekusaidia kuachana na uovu?

Ona pia Julie B. Beck, “Nafsi Yangu Hufurahia katika Maandiko,” Ensign au Liahona, Mei 2004, 107–9.

Maombolezo 1; 3

Bwana anaweza kutuondolea huzuni tunayoipata kwa sababu ya dhambi.

Kitabu cha Maombolezo ni mkusanyiko wa mashairi yaliyoandikwa baada ya kuharibiwa kwa Yerusalemu na hekalu lake. Kwa nini unafikiri ni muhimu kwamba maombolezo haya yalihifadhiwa na kujumuishwa katika Agano la Kale? Fikiria ni mafumbo gani katika Maombolezo 1 na 3 yanakusaidia kuelewa huzuni kubwa ambayo Israeli walihisi. Ni jumbe gani za matumaini katika Kristo ambazo unazipata? (ona hususani Maombolezo 3:20–33; ona pia Mathayo 5:4; Yakobo 4:8–10; Alma 36:17–20).

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa Ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

Yeremia 31:3.Je! Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wameonyeshaje “upendo Wao wa milele” kwetu? Kuonyesha picha za vitu ambavyo Kristo aliumba kwa ajili yetu au alifanya wakati wa huduma Yake ya mwili inaweza kusaidia familia yako kuhisi “fadhili” Zake.

Yeremia 31: 31–34; 32:38–41.Fikiria kufanya orodha ya vitu katika mistari hii ambavyo Bwana anaahidi wakati tunafanya maagano Naye. Maelezo haya yanatufundisha nini kuhusu umuhimu wa maagano yetu?

Wanafamilia wanaweza pia kuandika (au kuchora) kwenye mioyo ya karatasi kitu ambacho kinaonyesha jinsi wanavyohisi juu ya Mwokozi. Inamaanisha nini kuwa na sheria Yake iliyoandikwa moyoni mwetu? (ona Yeremia 31:33). Je, tunamwonyeshaje Bwana kwamba tunataka kuwa watu Wake?

Yeremia 36.Je! Unaweza kutumia Yeremia 36 kusaidia familia yako kujifunza kuhusu umuhimu wa maandiko? (ona, kwa mfano, mstari wa 1–6, 10, 23–24, 27–28,32). Unaweza kumuomba mwanafamilia mmoja asome mstari kutoka sura hii wakati mwanafamilia mwingine anaiandika, kama Baruku alivyomfanyia Yeremia. Kwa nini tuna shukrani kwa juhudi za watu kama Baruku, ambaye alihifadhi maneno ya manabii? Je, tunaweza kufanya nini kumwonesha Bwana tunathamini maneno Yake katika maandiko?

Maombolezo 3:1–17, 21–25, 31–32.Kama familia, mnaweza kuzungumza jinsi hisia zilivyoelezewa katika Maombolezo 3:1–17 inaweza kuhusiana na hisia tulizonazo tunapotenda dhambi. Je! Ujumbe katika mstari wa 21–25, 31–32 unawezaje kuathiri maisha yetu?

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “I Feel My Savior’s Love,” Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 74–75

Kuboresha Kujifunza Binafsi

Tafuta ufunuo. Unapotafakari kwa siku nzima, unaweza kupokea maoni ya ziada na miongozo juu ya maandiko uliyojifunza. Usifikirie kusoma injili kama shughuli ambayo unaitengea muda bali ni kama vile tu shughuli ambayo unaifanya kila wakati. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 12.)

Picha
Mtu ndani ya pango anaonekana mwenye huzuni wakati jiji linateketeanje.

Yeremia akiomboleza juu ya Uharibifu wa Yerusalemu, na Rembrandt van Rijn

Chapisha