Agano la Kale 2022
Oktoba 24–30. Ezekieli 1–3; 33–34; 36–37; 47: “Nami Nitatia Roho Mpya ndani Yenu”


“Oktoba 24–30. Ezekieli 1–3; 33–34; 36–37; 47: ‘Nami Nitatia Roho Mpya ndani Yenu’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Agano la Kale 2022 (2021)

“Oktoba 24–30. Ezekieli 1–3; 33–34; 36–37; 47,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2022

Picha
Yesu akiongoza kondoo

Njoo, Unifuate, na Scott Sumner

Oktoba 24–30

Ezekieli 1–3; 33–34; 36–37; 47

“Nami Nitatia Roho Mpya ndani Yenu”

Hutakuwa na muda wa kufundisha kila kanuni katika Ezekieli. Tafuta mwongozo wa kiroho kuhusu nini cha kutilia mkazo na wahimize watoto waendelee kujifunza nyumbani.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Waruhusu watoto wachache wafanye zamu kuchora picha ya kitu walichojifunza kutoka kwenye usomaji wa maandiko hivi karibuni. Watoto wengine wanaweza kubashiri ni nini kila mtoto anachora.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

Ezekieli 3:17

Manabii ni kama walinzi ambao hutuonya juu ya hatari.

Ezekieli alikuwa kama mlinzi, akiwaonya Waisraeli juu ya hatari ambazo wao hawakuziona. Wasaidie watoto waone jinsi manabii wetu leo walivyo kama walinzi.

Shughuli Yamkini

  • Wasomee watoto kile Bwana alichomwambia Ezekieli katika Ezekieli 3:17. Waalike wafanye vitendo ambavyo vinaendana na maneno, kama vile kuonesha kwa kidole macho yao, masikio na mdomo wakati ukisoma maneno “mlinzi,” “sikia,” na “kinywa.”

  • Waongoze watoto kupanda mlima kuzunguka chumba. Waonye kuhusu hatari za kusadikika kwenye njia, kama vile mito inayohitaji mtu aruke, matawi yanayohitaji mtu ainame ili apite au wanyama wa kuepuka. Waruhusu watoto wengine wafanye zamu kuwa kiongozi. Zungumza kuhusu jinsi manabii wetu wanavyotuonya sisi juu ya hatari tusizoweza kuziona.

  • Onesha picha ya nabii wa sasa wakati mkiimba pamoja wimbo kuhusu manabii, kama vile mstari wa mwisho wa “Follow the Prophet” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 110–11). Waambie watoto jinsi nabii alivyo kama mlinzi kwako.

Ezekieli 37:15–19

Maandiko yananifundisha kuhusu Yesu Kristo.

Ezekieli alifananisha nyumba ya Israeli na vijiti viwili ambavyo vilikuja kuwa kijiti kimoja. Vijiti hivi pia huwakilisha Biblia na Kitabu cha Mormoni, ambavyo kwa pamoja hushuhudia juu ya Yesu Kristo.

Shughuli Yamkini

  • Wape baadhi ya watoto nakala za Kitabu cha Mormoni; wape wengine nakala za Biblia. Fanya ufupisho wa Ezekieli 37:15–19 kwa kueleza kwamba Bwana alimwambia Ezekieli aandike kwenye vijiti viwili vikiwakilisha Biblia na Kitabu cha Mormoni. Soma mstari wa 17, na mwalike kila mtoto kumtafuta mtu aliye na kitabu cha maandiko tofauti na vyao na “aviunge” pamoja ili kwamba viwe “kimoja katika mikono [yao]” Zungumza kuhusu jinsi vyote Biblia na Kitabu cha Mormoni vinavyotusaidia kuimarisha imani yetu katika Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo.

  • Kwa kutumia picha kutoka Kitabu cha Sanaa ya Injili au kutoka kwenye vitabu vya miaka iliyopita vya Njoo, Unifuate, wasaidie watoto kushiriki hadithi kuhusu Yesu kutoka kwenye Biblia na Kitabu cha Mormoni. Waombe kushiriki ni kwa nini wana shukrani kuwa na vitabu hivi viwili vya maandiko.

Picha
jangwa na Bahari ya Chumvi

Ezekieli aliona katika ono mto ukitiririka kutoka hekaluni na kuiponya Bahari ya Chumvi.

Ezekieli 47:1–12

Baraka kuu huja kutoka hekaluni.

Ono la Ezekieli la mto wa uponyaji ambao ulitiririka nje ya hekalu linaweza kuwasaidia watoto kujifunza kwamba mahekalu yanaleta baraka kwenye maisha yetu.

Shughuli Yamkini

  • Waonyeshe watoto glasi ya maji. Ni jinsi gani maji yanatubariki? Waambie watoto kuhusu ono la Ezekieli la maji yanayotiririka nje ya hekalu (ona Ezekieli 47:1–12). Onesha picha katika muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Watu Binafsi na Familia (ona pia video “And the River Will Grow,” ChurchofJesusChrist.org). Waambie watoto kuhusu baraka unazopokea ambazo, kama vile mto katika ono la Ezekieli, hutiririka kutoka hekaluni.

  • Waalike watoto wajichore picha zao wakienda hekaluni. Imbeni pamoja wimbo unaoelezea baraka za hekaluni, kama vile “Families Can Be Together Forever” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto,188). Je, wimbo huu unafundisha nini kuhusu jinsi mahekalu yanavyotubariki?

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

Ezekieli 2:3–4; 3:7; 36:26–27

Yesu Kristo anaweza kunisaidia kubadili moyo wangu.

Ezekieli alitumia vifungu vya maneno kama “moyo mpya” na “roho mpya” kufundisha kuhusu aina ya badiliko ambalo Mwokozi analeta katika maisha yetu.

Shughuli Yamkini

  • Waombe watoto wachunguze Ezekieli 2:3–4; 3:7 ili kupata maneno ambayo yanawaelezea Waisraeli. Kisha waalike wasome Ezekieli 36:26–27 ili kujifunza jinsi Mwokozi alivyojitolea kuwasaidia wabadilike. Ni maneno gani yangeweza kuelezea “moyo mpya” na “roho mpya” ambayo Yeye hutupatia? (ona, kwa mfano, Mosia 3:19; 5:2).

  • Waalike watoto wafikirie juu ya vitu ambavyo watu wenye “mioyo migumu” au “mioyo yenye ukaidi” (Ezekieli 2:4; 3:7) wangeweza kufanya. Kwa mfano, ni jinsi gani wangeweza kuitikia ushauri kutoka kwa mzazi au nabii? Wangeweza kufanya nini wanapomwona mtu aliye katika shida? Ni kwa jinsi gani tunatenda tofauti pale Mwokozi anapokuwa amelainisha mioyo yetu?

Ezekieli 37:19–23

Biblia na Kitabu cha Mormoni husaidia “kutukusanya” kwa Yesu Kristo.

“Kijiti cha Yuda” (Bibilia) na “kijiti cha Yusufu” (Kitabu cha Mormoni) katika kitabu cha Ezekieli hufanya kazi pamoja ya kukusanya Israeli kwa Mwokozi (ona Ezekieli 37:19).

Shughuli Yamkini

  • Nyanyua juu nakala ya Biblia na Kitabu cha Mormoni, na waulize watoto kwa nini wanaona ni vyema kuwa na vitabu hivi vyote viwili. Wasomee Ezekieli 37:19, na eleza kwamba “kijiti cha Yusufu” humaanisha Kitabu cha Mormoni, ambacho kiliandikwa na uzao wa Yusufu wa Misri na “kijiti cha Yuda” humaanisha Biblia, ambayo iliandikwa kwa sehemu kubwa na Wayahudi. Kisha someni pamoja mistari 21–23 na 2 Nefi 3:12, na orodhesha baraka ambazo huja kutokana na kuwa na vitabu hivi vyote viwili.

  • Weka picha ya Yesu katikati ya chumba na waalike watoto wasogeze viti vyao kwenye maeneo tofauti kuelekea kuta za chumba. Kisha waombe watumie Mwongozo wa Mada kutafuta maandiko katika Biblia na Kitabu cha Mormoni ambayo hufundisha kuhusu Yesu Kristo (ikiwa itahitajika, waoneshe jinsi ya kufanya hili). Baada ya kila mtoto kushiriki andiko, waalike watoto wote wasogeze viti vyao karibu na picha ya Yesu. Endeleeni mpaka kila mtoto awe “amemsogelea” Yesu.

Ezekieli 47:1–12

Baraka za hekalu zinaweza kuponya mioyo yetu na familia zetu.

Maji yanayotiririka kutoka hekaluni katika ono la Ezekieli yalileta uhai kwa kila kitu yalichokigusa. Kadhalika, baraka zinazotiririka kutoka hekaluni zinaweza kutuponya kiroho na kutuletea uzima wa milele.

Shughuli Yamkini

  • Orodhesha ubaoni baadhi ya maneno muhimu yanayohusiana na Ezekieli 47:1–12, kama vile hekalu, mto, jangwa, Bahari ya Chumvi, wingi wa samaki, na mti wa matunda. Mwalike kila mtoto achague moja ya vitu hivi kwa ajili ya kuchora. Kisha someni mistari pamoja na waalike watoto kushiriki michoro yao wakati vipengele vyao vinapotajwa. Ni baraka zipi zilikuja kutokana na mto katika ono hili? (ona mistari 8–9,12). Wasaidie watoto kuona jinsi baraka hizi zinavyofanana na baraka ambazo Baba wa Mbinguni na Mwokozi wanatoa kwa wale wanaoshika maagano ya hekaluni.

  • Onesha video “And the River Will Grow” (ChurchofJesusChrist.org). Au someni pamoja kile Mzee Dale G. Renlund alichofundisha kuhusu ono la Ezekieli katika “Historia ya Familia na Kazi ya Hekaluni: Kuunganishwa na Uponyaji,” (Ensign au Liahona, Mei 2018, 47–48). Waambie watoto jinsi gani kazi ya historia ya familia na hekalu vilivyokuletea uponyaji wa Mwokozi. Waalike watoto kushiriki hisia zao kuhusu hekalu.

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Waalike watoto kushiriki na familia zao kitu kimoja walichojifunza leo na kitu kimoja wanachotaka kujifunza zaidi.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Saidia Kujifunza Nyumbani. “Mojawapo ya malengo yako kama mwalimu ni kuwahimiza wale unaowafundisha kuwa na uzoefu wao wenyewe katika maandiko—wa binafsi na pamoja na familia zao” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 36).

Chapisha