Watoto na Vijana
Mpangilio kwa ajili ya Ukuaji


“Mpangilio kwa ajili ya Ukuaji,” Maendeleo Binafsi: Kitabu cha Mwongozo cha Watoto (2019)

“Mpangilio kwa ajili ya Ukuaji,” Maendeleo Binafsi: Kitabu cha Mwongozo cha Watoto

Mpangilio kwa ajili ya Ukuaji

Mpangilio huu unaweza kukusaidia kukua katika nyanja nne ambazo kwazo Yesu alikua (ona Luka 2:52).

Picha
gundua, panga, tenda, tafakari

Gundua

Picha
kijana akitafiti

Baba wa Mbinguni amekupatia vipawa na talanta. Unaweza kuomba ili kujua vipawa na talanta hizo ni zipi na kipi unaweza kufanyia kazi sasa.

Tafuta mawazo kwenye kurasa 44–61.

Panga

Picha
kijana akitumia ramani

Baada ya kugundua ni kwa jinsi gani unataka kukua, omba na zungumza na familia yako kuhusu jinsi ya kufanya hilo. Tengeneza mpango. Wazazi wako na viongozi wako wanaweza kukusaidia.

Tenda

Picha
kijana akiwa na wazazi

Baada ya kutengeneza mpango, jaribu kuufanyia kazi! Piga hatua ndogo. Jifunze pamoja na wengine kupitia huduma na shughuli. Burudika! Omba kwa ajili ya usaidizi, na badili mpango wako ikiwa unahitaji kufanya hivyo. Endelea kujaribu!

Tafakari

Picha
kijana akitafakari

Fikiria kuhusu kile ulichojifunza na jinsi kilivyokusaidia kumfuata Yesu. Sherehekea! Mshukuru Baba wa Mbinguni kwa ukuaji wako. Tafuta njia za kutumia kile ulichojifunza ili kuwatumikia wengine. Endelea kusonga na wazo hili, au chagua kitu kipya cha kufanyia kazi!

Chapisha