“Wewe ni Mtoto wa Thamani wa Mungu,” Maendeleo Binafsi: Kitabu cha Mwongozo cha Watoto (2019)
“Wewe ni Mtoto wa Thamani wa Mungu,” Maendeleo Binafsi: Kitabu cha Mwongozo cha Watoto
Wewe ni Mtoto wa Thamani wa Mungu
Mwanzo uliishi na Baba wa Mbinguni, ambaye anajua kila kitu na anampenda kila mtu. Yeye anataka wewe uwe kama Yeye! Yeye amekupatia mwili, uwezo, na vipawa vya kiroho. Anataka wewe na watoto Wake wote kugundua na kuendeleza vipawa hivi. Ametupatia mpango ili kutusaidia kuwa na furaha na kuwabariki wengine.
Uliahidi kumfuata Yesu Kristo wakati ulipobatizwa na wakati unapopokea sakramenti.
Unapothibitishwa, unapokea kipawa cha Roho Mtakatifu ili kukuongoza.
Unaweza kupata shangwe na amani wakati unapochagua kuishi kama ambavyo Yesu angeishi.
Unaweza kujifunza na kukua. Unaweza kuwapenda na kuwatumikia wengine, kama ambavyo Yesu angefanya.
Baba wa Mbinguni alimtuma Mwanawe, Yesu Kristo, kuwa mfano na kufanya iwezekane kwako kutubu na kubadilika.
Unaweza kufanya maagano hekaluni ambayo yatakuwezesha kuishi na Baba wa Mbinguni tena.