Uteuzi kutoka Tafsiri ya Joseph Smith ya Biblia
Zifuatazo ni sehemu zilizo chaguliwa za Tafsiri ya Joseph Smith ya Biblia ya Toleo la King James (TJS). Bwana alimwongoza Nabii Joseph Smith kuurejesha ukweli kwenye maandiko ya Biblia ya King James ambayo yalipotea au kubadilishwa tangu pale maneno ya kwanza yalipoandikwa. Ukweli huu uliorejeshwa ulifafanua mafundisho na kuboresha uelewa wa maandiko.
Kwa sababu Bwana alimfunulia Joseph kweli fulani ambazo mwandishi wa kwanza aliziandika, Tafsiri ya Joseph Smith ni tofauti na tafsiri ya Biblia nyingine yoyote ulimwenguni. Kwa maana hiyo, neno tafsiri linatumika katika mapana na katika njia tofauti kuliko kawaida, kwa maana tafsiri ya Joseph ilikuwa ni ufunuo zaidi ya tafsiri ya kawaida kutoka lugha nyingine.
Tafsiri ya Joseph Smith ya Biblia ya Mfalme James ina mahusiano pamoja au ni imetamkwa katika sehemu za Mafundisho na Maagano (ona sehemu za 37, 45, 73, 76, 77, 86, 91, na 132). Pia, kitabu cha Musa na Joseph Smith—Mathayo ni dondoo kutoka kwa Tafsiri ya Joseph Smith.
Kwa maelezo zaidi juu ya Tafsiri ya Joseph Smith, ona “Tafsiri ya Joseph Smith (TJS)” katika Mwongozo wa Maandiko.
Kielelezo kifuatacho kinaonesha mifano ya uteuzi kutoka Tafsiri ya Joseph Smith:
© 2020 by Intellectual Reserve, Inc. All rights reserved. Source: 5/21