2021
“Nataka Kwenda Paradiso”
Machi 2021


“Nataka Kwenda Paradiso”

Niliposali na kumwomba Mungu kuhusu njia hii mpya, nilihisi kushawishika zaidi juu ya ukweli nilioupata.

Picha
sun breaking through clouds

Picha kutoka Getty Images, sura na mwanamitindo

Nilikuwa nimekuwa muumini mwenye msimamo wa kanisa lingine, lakini basi nilianza kujifunza mafundisho yake kuhusu mahali pa mateso ya muda. Dhana hii hufundisha kwamba roho, baada ya kifo cha kimwili, zinaingia katika mahali sawa na gereza, ambapo ni lazima zitakaswe kabla ya kwenda paradiso.

Nilipofikiria kuhusu roho zinazoteseka huko mahali pa kutakaswa dhambi, nikawaza juu ya ubaadae wangu mwenyewe wa kiroho na uhusiano wangu na Yesu Kristo. Nilianza kusali, “je, sharti nifanye nini ili kuepuka tohorani? Nataka kwenda paradiso.”

Kitu cha kwanza kilichoingia akilini mwangu, kilikuwa ni kuishi zile Amri Kumi. Nilihisi kwamba nikifanya hivyo, neema ya Mungu ingeniruhusu kuiepuka gereza ya mateso ya muda. Nikajiwekea sharti la kushika amri na kuanza kipindi kikali cha kufunga, kusali, kujifunza maandiko na kutafakari.

Wakati huu, nilihisi msukumo wa kumuuliza maswali yasiyo ya kawaida daktari katika kliniki ambapo nilikuwa nikifanya kazi kama mhasibu mkuu.

“Dkt. Thibaut,” nilisema, “Bwana Yesu Kristo yupo katika kanisa lako?”

Yeye alieleza kwamba alikuwa wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho. Na kutoka wakati ule na kuendelea, Roho aliongoza majadiliano yetu. Nilimwuliza kuhusu tofauti kati ya kanisa lake na langu. Aliniambia kuhusu Kitabu cha Mormoni. Tulipoendelea na mazungumzo yetu, shangwe ilijaa moyoni mwangu. Nilihisi kupokea majibu ya sala zangu.

Siku mbili baadaye wamisionari walinipatia Kitabu cha Mormoni, ambacho nilikisoma na kujifunza pamoja nao. Nilijisikia vyema kujifunza mambo mapya kutoka kwenye maandiko. Nikaanza kutii Neno la Hekima.

Wakati nilipotambua kwamba nimepoteza hamu na kanisa langu, ambapo nilikuwa nimejihusisha sana, nilijiuliza nini kilikuwa kinatendeka. Nilisali na kumwomba Mungu kuhusu hii njia mpya. Nilipofanya hivyo, nilihisi zaidi kushawishika zaidi juu ya ukweli nilioupata. Niliamua kujiunga na Kanisa, ingawa nilijua ningekabiliwa na mateso.

Mateso yalikuja, lakini Bwana aliniimarisha. Najua kwamba Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho, lilikuwa ndilo jibu la sala yangu ya dhati: “Nataka kwenda paradiso.” Najua ninaweza kwenda huko baada ya kufa, kama nitabaki mwaminifu kwenye amri za Mungu.

Chapisha