2022
Baraka za Kusoma Kitabu cha Mormoni Kila Siku
Aprili 2022


UJUMBE WA URAIS WA ENEO

Baraka za Kusoma Kitabu cha Mormoni Kila Siku

Kuna ahadi inayohusiana ambayo nimeona kuwa ya kweli katika maisha yangu. Ahadi hii inahusiana na kupokea ufunuo katika maisha yetu ya kila siku.

Mnamo mwaka 2007 Marekani ilikuwa katikati ya mporomoko wa kiuchumi. Kwa sababu ya mdororo huu, baadhi ya wateja wangu katika biashara walianza kufilisika na kufunga biashara zao. Hii ilikuwa ikiumiza biashara yangu. Wakati nilipotafuta kukidhi mahitaji ya familia yangu na kuwasaidia wateja wangu, nilikuwa nikitafuta mwongozo kutoka kwa Baba wa Mbinguni juu ya nini ninapaswa kufanya. Sikuwa nikipata jibu dhahiri na sikujua nini cha kufanya. Asubuhi moja wakati nikiomba na kuvuta taswira juu ya tatizo hili, nilichukua kitabu cha Mormoni na kuanza kusoma. Niliposoma kitabu hiki cha kupendeza, nilihisi mawazo yakinijia akilini juu ya kile ambacho ningeweza kufanya kuwasaidia wateja wangu na kuisaidia biashara yangu. Lilikuwa jibu dhahiri kwa maombi yangu.

Katika utangulizi wa Kitabu cha Mormoni, kuna mwaliko na ahadi. Mwaliko kwa watoto wote wa Mungu ni kukisoma na kutafuta kujua ikiwa ni cha kweli. Ahadi kwa wale wanaopata ushahidi mtakatifu kutoka kwa Roho Mtakatifu kwamba Kitabu cha Mormoni ni cha kweli, ni kuwa watajua pia kutokana na huo uwezo kwamba Yesu Kristo ni Mwokozi wa ulimwengu, kwamba Joseph Smith ni mfunuzi na nabii Wake katika siku hizi za mwisho, na kwamba Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho ni ufalme wa Mungu ulioanzishwa tena duniani, kwa maandalizi ya Ujio wa Pili wa Masiya.

Kuna ahadi nyingine inayohusiana ambayo nimekuta kuwa ni ya kweli kwenye maisha yangu. Ahadi hii inahusika na kupokea ufunuo katika maisha yetu ya kila siku.

Kuhusiana na Kitabu cha Mormoni, Nabii Joseph Smith alisema: “Niliwaambia ndugu kwamba Kitabu cha Mormoni ndicho kitabu sahihi duniani, na ndicho jiwe la katikati la teo la dini yetu, na kuwa mwanadamu angemkaribia Mungu zaidi kwa kufuata mafunzo yake, zaidi ya kitabu kingine.” 1

Tunaposoma Kitabu cha Mormoni kwa kusudi la dhati, si tu tutapata uthibitisho kwamba Yesu Kristo ni Mwokozi wa ulimwengu na kwamba Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho ni ufalme wa Bwana ulioanzishwa tena duniani, lakini pia tunaweza kupokea ufunuo wa ziada katika maisha yetu kuhusu maswali au changamoto tunazokabiliana nazo sasa.

Roho Mtakatifu, mshiriki wa tatu wa Uungu, ana kazi nyingi. Kati ya kazi zake nyingi ni zile za kuwa shahidi wa ukweli, mfunuzi, mfariji, na mwalimu.

Akizungumza juu ya Roho Mtakatifu, Yesu Kristo alifundisha “​Lakini yeye, ​​​huyo Roho wa kweli​ [akimrejelea Roho Mtakatifu], atakapokuja ​​​atawaongoza kwenye kweli yote​: kwa maana hatanena kwa shauri lake, lakini yote atakayoyasikia: na mambo yajayo ​​​atawapasha habari” (Yohana 16:13, msisitizo umeongezwa).

Mwokozi pia alifundisha ukweli huu kuhusu Roho Mtakatifu: “Lakini huyo ​​​Msaidizi​, ​ambaye ni​ Roho Mtakatifu​, ambaye Baba atampeleka kwa jina, ​​langu​​, atawafundisha ​​​yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia” (Yohana 14:26, msisitizo umeongezwa). Zaidi, Kitabu cha Mormoni kinafundisha kwenye Moroni 10:5, “Na kwa uwezo wa Roho Mtakatifu mtajua ukweli wa vitu vyote.”

Mara nyingi tutaomba kwa Mungu kwa ajili ya mwongozo. Tunaweza kuomba mwongozo kuhusiana na masuala ya familia, au mahusiano, au kazi, au kutatua matatizo binafsi tunayokabiliana nayo. Moja ya njia ambazo kwazo Mungu hujibu maombi yetu ni kupitia Roho Mtakatifu.

Katika maisha yangu mwenyewe nimeona kwamba wakati ninaposoma Kitabu cha Mormoni, mara nyingi ninahisi Roho Mtakatifu akishuhudia ukweli wa kile ninachosoma. Na kisha ninapokea baraka za ziada. Kwa sababu ninahisi Roho Mtakatifu akishuhudia kuweli wa maneno katika Kitabu cha Mormoni, wakati akishuhudia juu ya kweli hizi, moyo na akili yangu pia vinafunguka kupokea misukumo mingine kuhusu kile ninachopaswa kufanya katika nyanja zingine za maisha yangu. Roho Mtakatifu hakika “ananiongoza kwenye ukweli,” na “ananifundisha yote, kama jinsi maandiko yanavyoahidi.” Nimepokea mwongozo kwenye masuala ya kazi na masuala ya kifamilia. Nimepokea mwongozo katika miito ya Kanisa na kusaidia kutatua matatizo mengine ninayokabiliana nayo.

Kwangu mimi, ninaposoma Kitabu cha Mormoni, ninafungua mlango kwa ajili ya Roho Mtakatifu kushuhudia juu ya ukweli wa ujumbe wake. Na anaposhudia juu ya ukweli wa ujumbe wake, ikiwa ninasikiliza na kutafuta, mara nyingi ninapokea mwongozo wa ziada juu ya kile ninachopaswa kufanya katika nyanja zingine za maisha.

Katika Kitabu cha Mormoni, tunajifunza juu ya ukweli huu: “Kwani tazama, tena nawaambia kwamba kama mtaingia kwa njia hiyo, na kupokea Roho Mtakatifu, atawaonyesha ​​​vitu vyote ambavyo mnastahili kutenda” (2 Nefi 32:5).

Ninawaalika msome Kitabu cha Mormoni. Kisome kila siku. Pokea ushahidi wa uthibitisho wa ukweli wake kutoka kwa Roho Mtakatifu. Pokea ushahidi wa uthibitisho wa misheni takatifu ya Yesu Kristo na wa ufalme wa Mungu ulioanzishwa tena duniani leo. Na kisha kuwa tayari kupokea mwongozo na mafunzo na usaidizi kutoka kwa Roho Mtakatifu katika maeneo mengine ya maisha yako. Ninatoa ushahidi kwamba utakujia ikiwa utautafuta.

Matthew L. Carpenter aliitwa kama Sabini Mkuu mwenye Mamlaka mnamo Machi 2018. Amemuoa Michelle (Shelly) Kay Brown; wao ni wazazi wa watoto watano.

Muhtasari

  1. Utangulizi: Kitabu cha Mormoni.

Chapisha